Agano Jipya 2023
Julai 24–30. Matendo ya Mitume 16–21: “Bwana Alituita kwa ajili ya Kuhubiri Injili”


“Julai 24–30. Matendo ya Mitume 16–21: ‘Bwana Alituita kwa ajili ya Kuihubiri Injili’” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: Agano Jipya 2023 (2022)

“Julai 24–30. Matendo ya Mitume 16–21,” Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Msingi: 2023

Picha
Paulo akihubiri juu ya kilima

Julai 24–30

Matendo ya Mitume 16–21

“Bwana Alituita kwa ajili ya Kuhubiri Injili””

Baada ya kusoma Matendo 16–21, fuata ushawishi wa Roho na zingatia mawazo katika muhtasari huu unapojiandaa kufundisha. Tafuta ushauri kwenye “Kukidhi Mahitaji ya Watoto Wadogo” katika kitabu hiki cha kiada kwa ajili ya msaada wa ziada.

Picha
ikoni ya kushiriki

Alika Kushiriki

Waalike watoto wakusimulie kile wanachojua kuhusu uzoefu wa Paulo katika kushiriki injili. Wanaweza pia kuzungumzia kuhusu wamisionari wengine wanaowajua au kuhusu uzoefu wao wenyewe katika kumfundisha injili mtu mwingine.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wadogo

Matendo ya Mitume 4:25–34

Wamisionari hufundisha watu kuhusu Yesu.

Je, watoto unaowafundisha wanajua wamisionari wanafanya nini? Unawezaje kuwasaidia watoto kuelewa kwamba wanaweza kushiriki injili na watu wengine?

Shughuli Yamkini

  • Wasaidie watoto kuigiza Matendo ya Mitume16:25–34 unapoifanyia muhtasari hadithi ya Paulo na Sila wakihubiri injili gerezani (ona pia “Sura ya 61: Paulo na Sila Gerezani,” katika Hadithi za Agano Jipya, 158–60, au video inayofanana kwenye ChurchofJesusChrist.org). Eleza kwamba wamisionari leo pia wanafundisha watu kuhusu Yesu na kuwasaidia kujitayarisha ili kubatizwa.

  • Tengeneza vibandiko vya misionari vya jina kwa ajili ya watoto kuvaa, na wasaidie kuandika majina yao kwenye vibandiko. Wafundishe watoto maelezo rahisi ya mafundisho ya injili ili waweze kushiriki pamoja na wengine, kama vile “Mimi ni mtoto wa Mungu. anayetupenda,” “Mungu anasema kupitia nabii anayeishi,” au “Yesu Kristo ni Mwokozi Wetu.” Wakumbushe watoto kwamba hatuhitaji kuwa na vibandiko vya kimisionari vya majina ili kushiriki injili pamoja na wengine.

Matendo ya Mitume 17:10–12

Maandiko yanashuhudia juu ya Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo.

Ingawa baadhi ya watoto unaowafundisha yawezekana wasiweze kusoma bado, unaweza kuwasaidia kukuza upendo kwa maandiko na ona jinsi gani wanaweza kushuhudia juu ya Mwokozi.

Shughuli Yamkini

  • Msaidie mmoja wa watoto kusoma kirai “Wali … yachunguza maandiko kila siku” (Matendo ya Mitume 17:11). Waalike watoto kuonyesha kila siku ya wiki kwenye kalenda wanaporudia kirai hiki pamoja na wewe. Imbeni pamoja wimbo ambao unaofundisha kuhusu baraka za kusoma maandiko, kama vile “Search, Ponder, and Pray” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 109).

  • Ili kufundisha watoto kwamba maandiko yanashuhudia juu ya Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo, wasaidie kufunua kwenye sura katika maandiko, kama Matendo ya Mitume 17 au 18, na kutafuta maneno kama Mungu, Bwana, au Yesu. (Unaweza kutaka kuwekea alama maneno haya ili watoto waweze kuyapata kwa urahisi zaidi.) Kila wakati wanapopata moja ya maneno haya, waalike kuelezea kitu wanachojua kuhusu Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo.

Matendo ya Mitume 17:22–31

Mimi ni mtoto wa Mungu.

Juu ya Kilima cha Maazi, Paulo alifundisha kweli za msingi kuhusu asili ya Mungu, pamoja na kweli kwamba sisi ni watoto Wake na kwamba Yeye “hayuko mbali na kila mmoja wetu” (Matendo ya Mitume 17:27). Unawezaje kuwasaidia watoto kujiona wako karibu na Baba yao wa Mbinguni?

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto kurudia kirai “Sisi tu wazao wa Mungu” (Matendo ya Mitume 17:29), na eleza kwamba wazao maana yake watoto. Toa ushuhuda wako kwa kila mtoto, mmoja mmoja, kwamba yeye ni mtoto wa Mungu. Waalike kushiriki jinsi wanavyohisi kuhusu Baba yao wa Mbinguni.

  • Onyesha picha za watoto pamoja na famila zao (kama inawezekana, jumuisha picha za watoto katika darasa lako). Waombe watoto waoneshe wazazi kwa kidole katika hiyo picha . Eleza kwamba sisi ni watoto wa mama na baba zetu, na pia sisi wote ni watoto wa kiroho wa wazazi wetu wa mbinguni.

  • Imbeni wimbo kuhusu Baba wa Mbinguni, kama vile “I KNow My Father Lives” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 5). Kwa msaada kutoka kwa watoto, andika maneno au chora picha ubaoni ambazo zinaonesha vitu tunavyojifunza kuhusu Baba wa Mbinguni kutoka kwenye wimbo huu.

  • Wasomee watoto maneno haya kutoka Matendo ya Mitume 17:27: “Ijapokuwa hawi mbali na kila mmoja wetu.” Zungumzia kuhusu wakati ulipojiona uko karibu na Baba wa Mbinguni, na waalike watoto wafanye vivyo hivyo.

Picha
mtu akimshika msichana mdogo

Kila mtu ni mtoto wa Mungu.

Picha
ikoni ya kufundisha

Fundisha Mafundisho: Watoto Wakubwa

Matendo ya Mitume 16:14–15, 25–34; 18:7–8, 24–28

Ninaweza kuwa mmisionari sasa.

Unawezaje kuwasaidia watoto kuwa kama Paulo na kushiriki na wengine kile wanachojifunza kuhusu injili?

Shughuli Yamkini

  • Waalike watoto wasome Matendo ya Mitume 16:14–15, 25–34; 18:7–8, 24–28 na tengeneza orodha ya watu Paulo na Apolo walioshiriki injili pamoja nao. Kisha waalike watengeneze orodha ya watu wanaoweza kushiriki nao injili. Waache watoto waigize jinsi ambavyo wangeweza kuwaambia watu hawa kuhusu Yesu Kristo au kuwaalika Kanisani. Ungeweza pia kuwaalika watoto kuandika maneno machache yanayobeba ushuhuda wa ukweli wa injili kwa watu hawa.

  • Waalike wamisionari, wamisionari waliorudi kutoka misheni zao, au wamisionari wa kata kutembelea darasa na kuzungumza kuhusu uzoefu wao kuhusu kuhubiri injili. Wahimize watoto kuuliza maswali kuhusu jinsi wanavyoweza kushiriki injili pamoja na wengine.

Matendo ya Mitume 17:2–4, 10–12; 18–28

Maandiko yanashuhudia juu ya Yesu Kristo.

Manabii wote washuhudia juu ya Yesu Kristo. Unawezaje kuwafundisha watoto kumtafuta Yeye katika maandiko, hata kama hakutajwa kwa jina?

Shughuli Yamkini

  • Wasaidie watoto kusoma Matendo ya Mitume 17:2–4, 10–12; 18–28, na waalike kutafuta kitu gani kinafanana katika vifungu hivi. Kulingana na aya hizi, nini kiliwasaidia watu kuamini injili ya Yesu Kristo? Waalike watoto kushiriki hadithi zao wanazozipenda kuhusu Yesu ambazo wamejifunza kutoka kwenye maandiko.

  • Kwenye vipande vya karatasi, andika marejeleo ya maandiko ambayo yanafundisha kuhusu Mwokozi (unaweza kupata baadhi katika Mwongozo wa Maandiko, “Yesu Kristo,” scriptures.ChurchofJesusChrist.org). Ficha karatasi hizo humo chumbani na waalike watoto wazitafute. Wasaidie watoto kuyaangalia marejeo wanayoyapata, na waombe kushiriki wao kwa wao kile kila andiko hufundisha kuhusu Yesu.

Matendo ya Mitume 17:22–31

Mimi ni mtoto wa Mungu.

Unawezaje kuwasaidia watoto kukumbuka kwamba wao ni watoto wa Mungu?

Shughuli Yamkini

  • Waonyeshe watoto jiwe, na eleza kwamba katika siku za Paulo, watu waliabudu miungu waliyoitengeneza kutoka kwenye jiwe na vitu vingine. Waombe watoto kusoma Matendo ya Mitume 17: 27–29. Tunajifunza nini kuhusu Mungu kutoka aya hizi? Elezea kwamba wazao humaanisha watoto. Waulize watoto jinsi inavyowafanya wajisikie kujua kwamba wao ni watoto wa Mungu.

  • Waombe watoto kusoma Matendo ya Mitume 17: 27. Waalike watoto kuandika kuhusu au kuchora picha ya njia ambazo wanaweza “kutamani kumtafuta” au kuwa karibu zaidi na Mungu. Ni lini wamehisi kwamba Yeye “hayupo mbali [nao]”?

Picha
ikoni ya kujifunza

Himiza Kujifunza Nyumbani

Wahimize watoto kutafuta maandiko wiki hii ambayo yanafundisha kuhusu Yesu Kristo (hii inaweza kutokea katika wakati wao wa kujifunza maandiko binafsi au kifamilia). Wiki ijayo, waalike kushiriki kile walichokipata.

Kuboresha Ufundishaji Wetu

Wasaidie watoto kuwa wanafunzi wazuri. Madhumuni yako katika kuwafundisha watoto sio tu kuwapa wao ukweli. Unapaswa pia kuwasaidia kukua na kuwa watafutaji wa ukweli wanaojitegemea. Kwa mfano, badala ya kuwaambia tu watoto hadithi ya Paulo akihubiri juu ya Kilima Maazi, ungeweza kupanga shughuli, kama hizo zilizopendekezwa katika muhtasari huu, ambazo zitawasaidia kugundua ukweli katika hadithi wao wenyewe.

Chapisha