Miito ya Misheni
Sura ya 3: Jifunze na Fundisha Injili ya Yesu Kristo


“Sura ya 3: Jifunze na Fundisha Injili ya Yesu Kristo,” Hubiri Injili Yangu: Mwongozo wa Kushiriki Injili ya Yesu Kristo (2023)

“Jifunze na Fundisha Injili ya Yesu Kristo,” Hubiri Injili Yangu

Picha
Ubatizo wa Kristo, na Joseph Brickey

Sura ya 3

Jifunze na Fundisha Injili ya Yesu Kristo

Masomo katika sura hii yana mafundisho, kanuni, na amri muhimu za injili ya Yesu Kristo. Masomo haya ndiyo kile ambacho manabii na mitume walio hai, wameelekeza wewe ujifunze na kufundisha. Yametolewa ili kwamba uweze kuwasaidia wengine waelewe wazi mafundisho ya Kristo.

Sehemu ya kwanza katika sura hii ni mwaliko wa ubatizo. Sehemu iliyobaki ya sura hii ina masomo manne:

Jifunze maandiko na thamini mafundisho katika kila somo. Unapofanya hivyo, Roho atatoa ushahidi wa kweli unazojifunza. Yeye atakusaidia ujue nini cha kusema na kufanya ili kuwasaidia wengine wapokee ushahidi wa ukweli. (Ona Mafundisho na Maagano 84:85.)

Watu watakuja kumjua Mwokozi kikamilifu zaidi pale wanapofanya kile ambacho Yeye amewaalika wafanye. Toa mialiko katika kila somo, na wasidie watu waweke ahadi zao. Watu wanapotimiza ahadi, wanaanza kuishi injili ya Yesu Kristo na kujiandaa kufanya upya maagano na Mungu.

Fundisha masomo yote kabla na baada ya ubatizo. Wamisionari wa muda wote wanaongoza katika kufundisha masomo nyakati zote. Wamisionari wa kata au waumini wengine wanashiriki inapowezekana. Ona sura ya 10 na 13 kwa maelezo kuhusu kuwajumuisha waumini katika kufundisha.

Jitayarishe Kufundisha

Unapojiandaa kufundisha, pitia tena taarifa za kila mtu katika app ya Hubiri Injili Yangu. Tengeneza mpango wa somo kulingana na mahitaji ya mtu. Fikiria kile ambacho yeye anapaswa kujua na kuhisi wakati wa matembezi yenu ya kufundisha. Roho ataongeza juhudi zako wakati unapotenga muda kujiandaa na kupanga.

Haya ni baadhi ya maswali kwa ajili yako na mwenza wako kuyafikiria wakati mnapojiandaa kufundisha.

  • Ni mwaliko upi tutautoa ili kumsaidia mtu ajenge imani katika Kristo na apige hatua? Mialiko ndiyo jinsi unavyowasaidia watu watubu na wapate uzoefu wa “nguvu za Mkombozi” (Helamani 5:11). Fikiria maendeleo, hali, na mahitaji ya mtu. Kisha jumuisha mwaliko mmoja au miwili katika mpango wako wa somo.

  • Ni mafundisho na kanuni zipi zitamsaidia mtu atimize ahadi tuliyomwalika aiweke? Kwa maombi amua ni mafudisho yapi na kanuni zipi zitawasaidia watu waelewe kwa nini kuweka ahadi yao ni muhimu kwa ajili yao na kwa Bwana.

  • Ni kwa jinsi gani tutamsaidia mtu ajifunze mafundisho? Kujiandaa kufundisha mafundisho, panga na fanya muhtasari wa kile utakachofundisha ukitumia somo la 1–4. Tambua maswali, maandiko, mifano, na vyombo vya habari vinavyofaa ambavyo vitamsaidia mtu aelewe kile unachofundisha. Ona sura ya 10 kwa ajili ya maelezo kuhusu jinsi ya kuboresha ufundishaji wako.

  • Ni baraka zipi ambazo Mungu ameahidi kwa ajili ya kukubali na kutimiza ahadi? Unapojifunza mafundisho, tambua baraka za Mungu zilizoahidiwa. Unapofundisha, ahidi baraka na utoe ushuhuda kwao.

  • Waumini gani wangepaswa kushiriki? Katika mkutano wa uratibu wa kila wiki, amua ni waumini gani wangepaswa kukusaidia kufundisha na kumsaidia mtu huyu. Kabla ya somo, jadili ushiriki wao. Ona sura ya 10.

  • Tunaweza kufanya kipi ili tuwasaidie watu watimize ahadi zao baada ya sisi kuondoka? Fuatilia kwa kufanya mawasiliano mafupi kila siku ili kuwasaidia watu watimize ahadi zao. Tafuta njia za kuwajumuisha waumini katika kuwasaida wale unao wafundisha kuweka ahadi zao. Mawasiliano haya yangeweza kujumuisha kusoma sura kutoka katika Kitabu cha Mormoni au maandiko mengine. Kama mtu hatimizi ahadi ya awali, inaweza kuwa vyema kumsaidia kwenye hilo kabla ya kumpa mwaliko wa ahadi nyingine. Ona sura ya 11.

  • Ni kwa jinsi gani tunaweza kuwasaidia vyema wakati ujao? Baada ya kila hali ya kufundisha, tathmini uzoefu wa watu unaowafundisha. Je, imani yao katika Kristo inakua? Je, wanamhisi Roho? Je, wanatubu na kuweka na kutimiza ahadi? Je, wanasali, wanajifunza Kitabu cha Mormoni, na kuhudhuria kanisa? Tengeneza mipango ya kuwasaidia.

Fundisha kutoka Moyoni Mwako kama Unavyoongozwa na Roho

Wakizungumza na wazee na akina dada wote, Urais wa Kwanza na Akidi ya Mitume Kumi na Wawili walinena:

“Dhumuni letu ni kufunza ujumbe wa injili ya urejesho kwa njia ambayo itaruhusu Roho kuwaongoza wote, wamisionari na wale wanaofunzwa. Ni muhimu kujifunza dhana za [masomo], lakini dhana hizi hazifai kufunzwa kwa mawasilisho ya kukariri. Mmisionari anapaswa kuhisi kuwa huru kutumia maneno yake binafsi kama anavyoshawishiwa na Roho. Hapaswi kutoa masimulizi ya kukariri, bali kuzungumza kutoka moyoni kwa ufafanuzi wake mwenyewe. Anaweza kutoka nje kidogo ya mpangilio wa masomo, akitoa kile ambacho amesukumwa kutenda, kulingana na mapendeleo na mahitaji ya [mtu]. Kuzungumza kutokana na msukumo wake wenyewe na kwa maneno yake mwenyewe, anapaswa kutoa ushuhuda wa ukweli wa mafundisho yake.”

Picha
wamisionari wakikutana na mwanamume

Fundisha na alika kulingana na Mahitaji ya Mtu Binafsi

Una uhuru wa kufundisha masomo katika njia yoyote ambayo inawasaidia watu wajiandae kikamilifu kwa ajili ya ubatizo na uthibitisho wao. Somo lipi unafundisha, wakati gani unalifundisha na muda kiasi gani unalipa vinaamuliwa vyema na mahitaji ya mtu unayemfundisha na mwongozo wa Roho. Kwa mfano, unapowafundisha watu ambao hawana asili ya Ukristo, ungeweza kuanza kwa kuwasaidia wajenge muunganiko mkubwa na Baba wa Mbinguni na uelewa wa mpango Wake (ona “Kuwafundisha Watu Ambao Hawana Asili ua Ukristo” katika sura ya 10).

Acha Roho akuongoze kwenye mialiko ipi ya kutoa na wakati gani itolewe. Mwaliko sahihi katika wakati mwafaka unaweza kuwasukuma watu kufanya mambo ambayo yatajenga imani yao. Matendo haya yanaweza kuongoza kwenye badiliko kuu la moyo (ona Mosia 5:2; Alma 5:12–14).

Fundisha masomo ambayo ni rahisi, ya wazi na mafupi. Kwa kawaida, matembezi ya kufundisha hayapaswi kuzidi dakika 30, na unaweza kumfundisha mtu katika dakika chache kama dakika 5 tu.

Kwa kawaida utahitaji mikutano mingi kufundisha kanuni zilizo katika somo moja. Watu mara nyingi wataelewa vyema ujumbe wako kama utafundisha masomo mafupi, kufundisha mara nyingi, na kufundisha sehemu ndogo ya nyenzo.

Kujifunza Maandiko

Ni kipi unaelekezwa kufundisha?

Kwa nini ni muhimu kujifunza mafundisho katika masomo?

Chapisha