Seminari na Vyuo
Madhumuni ya Kufundisha katika Njia ya Mwokozi


“Madhumuni ya Kufundisha katika Njia ya Mwokozi,” Kufundisha katika Njia ya Mwokozi: Kwa Ajili ya Wote Wanaofundisha Nyumbani na Kanisani (2022)

“Madhumuni ya Kufundisha katika Njia ya Mwokozi,” Kufundisha katika Njia ya Mwokozi

Madhumuni ya Kufundisha katika Njia ya Mwokozi

Kanuni ambazo zimeelezwa katika nyenzo hii zinaweza kumsaidia kila mwalimu wa injili kufundisha katika njia ya Mwokozi. Hiyo inajumuisha wazazi, akina kaka na akina dada wahudumiaji, wamisionari, walimu wa seminari na chuo, na mtu yeyote ambaye wito wa Kanisa unampa fursa ya kufundisha.

Unaweza kujifunza nyenzo hii wewe mwenyewe au kuitumia ili kuongoza majadiliano na wengine kuhusu jinsi ya kuwa mwalimu bora. Kwa mfano, nyenzo hii ingeweza kutumika katika jioni za nyumbani, mikutano ya urais, mikutano ya baraza la kata au kigingi, mikutano ya mafunzo kwa ajili ya walimu wa seminari na chuo, na mikutano ya baraza la mwalimu (ona “Kwa Ajili ya Viongozi—Kuwasaidia Walimu Wafanikiwe”).

Jinsi Nyenzo Hii Ilivyoundwa

Sehemu ya 1 inasisitiza umuhimu wa kufokasi juu ya Yesu Kristo wakati wo wote tunapofundisha kanuni za injili Yake. Sehemu hii inaelezea kile tunachofundisha.

Sehemu ya 2: inasisitiza Kanuni za Kufundisha Kama Kristo Sehemu hii inaelezea jinsi tunavyofundisha.

Sehemu ya 3 inatoa mapendekezo yanayofaa ili kuwasaidia walimu kutumia kanuni hizo za kufundisha kama Kristo.

Muhtasari wa Kufundisha kama Kristo

Jedwali zifuatazo zinatoa muhtasari wa kanuni zilizofundishwa katika nyenzo hii.

Picha
Mfano wa Muhtasari wa Kupanga-Somo

Chapisha