Seminari na Vyuo
Wasaidie Wanafunzi Kuja kwa Yesu Kristo


“Wasaidie wanafunzi Kuja kwa Kristo,” Kufundisha katika Njia ya Mwokozi: Kwa Ajili ya Wote Wanaofundisha Nyumbani na Kanisani (2022)

“Wasaidie Wanafunzi Kuja kwa Yesu Kristo,” Kufundisha katika Njia ya Mwokozi

Picha
Yesu akiwa ameketi na watoto

Kama walimu wa injili ya Yesu Kristo, tunawasaidia wengine kuelewa na kutegemea mafundisho Yake, nguvu na upendo Wake.

Wasaidie Wanafunzi Kuja kwa Yesu Kristo

Hakuna unachofanya kama mwalimu kitakachowabariki wanafunzi zaidi kuliko kuwasaidia kumjua Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo na Kuhisi upendo Wao (ona Yohana 17:3). Fikiria juu ya matukio ambayo yamekusaidia wewe kuja kumjua na kumpenda Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo. Je, wewe umefanya nini ili kujifunza kuhusu sifa Zao, nguvu na upendo Wao? Ni kwa jinsi gani upendo wako kwa Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo umekuletea furaha? Kisha fikiria juu ya upendo na nguvu Zao zinaweza kufanya nini kwa kwa kila mtu unayemfundisha. (Ona Alma 26:16; Musa 5:11.)

Lengo letu kuu katika maisha haya ni kuwa zaidi kama Baba yetu wa Mbinguni na kurejea Kwake. Njia ya kutimiza lengo hilo ni kwa kuja kwa Kristo (ona Yohana 14:6). Hii ndiyo ni kwa nini, kama vile nabii Nefi alivyofundisha, “tunazungumza kuhusu Kristo, tunashangilia katika Kristo” (2 Nefi 25:26).

Kila mtoto wa Mungu anahitaji nuru na ukweli ambao huja kutoka kwa Mwokozi na kuuchagua. Kuwa mwalimu wa injili ya Yesu Kristo inamaanisha kuwasaidia wengine kuelewa na kuyategemea mafundisho Yake, nguvu ya kukomboa, na upendo mkamilifu. Fikiria jinsi mawazo yafuatayo yanavyoweza kukusaidia kuwashawishi wengine kumjua vyema zaidi Yesu Kristo na kumfuata Yeye.

Wasaidie Wanafunzi Kutambua Upendo, Nguvu na Rehema za Bwana katika Maisha Yao

Ni vizuri kujua kuhusu upendo wa Mwokozi, nguvu, na rehema, lakini pia tunahitaji kupata uzoefu wake. Kuona jinsi alivyowabariki na kuwaponya watu katika maandiko kunatusaidia sisi kukuza imani kubwa zaidi kwamba Yeye anaweza kutubariki na kutuponya. Kwa mfano, kujifunza kuhusu uzoefu wa Danieli haikamiliki kama hayo hautushawishi sisi kumtumainia Bwana tunapokabiliwa na matundu yetu ya simba kistiari.

Unapowasaidia wanafunzi kutambua “huruma nyororo” ya Bwana (1 Nefii 1:20), kote katika maandiko na katika uzoefu wao wenyewe, watahisi na kujua kwamba Bwana yuko pamoja nao na kwa upendo atasimama na wao (ona Mafundisho na Maagano 68:6). Wao wataona na kuhisi uhalisia wa upendo na rehema za Mungu katika shida na hali zao binafsi.

Picha
Kristo akitoa Mahubiri ya Mlimani

Walimu wanaweza kuwasaidia wanafunzi kuguswa na upendo, nguvu na rehema za Mwokozi.

Wasaidie Wanafunzi Kuimarisha Uhusiano Wao na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo

Dhumuni la kufundisha na kujifunza kuhusu Yesu Kristo ni kumsaidia kila mtu kujongea karibu zaidi na Yeye na Baba yetu wa Mbinguni. Wasaidie watu unaowafundisha kamwe wasipoteze dhumuni hilo. Wahimize kuimarisha uhusiano wao na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo kwa kujifunza maandiko, kutubu daima, kuongea na Baba katika sala, na kushuhudia juu ya Baba na Mwana. Wafundishe wanafunzi kwa neno na kwa mfano jinsi ya kufanya na kushika maagano hutuunganisha na Wao. Wasaidie kujua jinsi gani tulivyo wa thamani na wapendwa Kwao. Imarisha imani yao kwamba Yesu Kristo, kwa sababu ya wema wa Upatanisho Wake mkamilifu, ndiye njia pekee ya kurudi kwa Baba yao. Toa fursa kwa wanafunzi kupokea ushahidi kutoka kwa Roho Mtakatifu, “ambaye anawashuhudia Baba na Mwana” (Musa 5:9).

Wasaidie Wanafunzi Kwa Makusudi Kabisa Wajitahidi Kuwa Zaidi kama Yesu Kristo

Hatimaye, kujifunza kuhusu Yesu Kristo kunatushawishi sisi kuwa zaidi kama Yeye alivyo. Lakini kuwa kama Yeye kunatokea tu tunapotenda kwa imani, kote ndani na nje ya darasa, tukifanya chaguzi za makusudi za kufuata mfano Wake na kupokea neema Yake. Waalike wanafunzi kutafuta msaada wa Roho Mtakatifu ili kutambua njia wanazoweza kuwa zaidi kama Mwokozi. Toa mwongozo na msaada wanafunzi wanapofanya jitahidi ya kuwa kama Yeye kuwa ni jambo la maisha yao yote.

Yakobo alifundisha kwamba “vitu vyote vilitolewa na Mungu tangu mwanzo wa dunia” vinaweza kutufundisha kuhusu Yesu Kristo (2 Nefi 11:4). Kufundisha kwako kunaweza kuwa moja ya vitu hivyo. Mweke Yesu Kristo kuwa kitovu cha kila uzoefu wa kufundisha na kujifunza kwako. Wewe na wanafunzi “mnapozungumza kuhusu Kristo, … tunafurahia katika Kristo, … tunahubiri kuhusu Kristo” (2 Nefi 25:26), Roho Mtakatifu anaweza kupanda ushahidi juu ya Mwokozi kwa kina ndani ya akili na moyo wa kila mtu. Unapowasaidia wanafunzi kuja kumjua Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wao wenyewe, watakuwa wanaweza kuwageukia zaidi Wao kwa ajili ya msaada, matumaini na uponyaji katika maisha yao yote.

Chapisha