Seminari na Vyuo
Fundisha kuhusu Yesu Kristo Bila KujalI Kitu Unachofundisha


“Fundisha kuhusu Yesu Kristo Bila KujalI Kitu Unachofundisha,” Kufundisha katika Njia ya Mwokozi: Kwa Ajili ya Wote Wanaofundisha Nyumbani na Kanisani (2022)

“Fundisha Kuhusu Yesu Kristo Bila KujalI Kitu Unachofundisha,” Kufundisha katika Njia ya Mwokozi

Picha
Yesu na Wanafunzi Wake katika Karamu ya Mwisho

Amani Nawapeni, na Walter Rane

Fundisha kuhusu Yesu Kristo Bila KujalI Kitu Unachofundisha

Kuna mambo mengi ya kufundisha katika injili ya urejesho ya Yesu Kristo—kanuni, amri, unabii, na hadithi za maandiko. Lakini haya yote ni matawi ya mti huo huo, kwa sababu vyote hivi vina dhumuni moja: kuwasaidia watu wote kuja kwa Kristo na wakamilishwe ndani Yake (ona Yaromu 1:11; Moroni 10:32). Hivyo basi, bila kujali unalofundisha, kumbuka kwamba hakika wewe unafundisha kuhusu Yesu Kristo na jinsi ya kuwa jinsi Yeye Alivyo. Roho Mtakatifu anaweza kukusaidia kujifunza kutambua kweli kuhusu Mwokozi na nguvu Yake ya kukomboa katika kila kanuni ya injili, amri, na mafundisho ya kinabii (ona Yakobo 7:10–11).

Je, unafundisha kuhusu dhabihu? Jaribu kuchunguza pamoja na wanafunzi jinsi gani dhabihu tunazofanya huzielekeza nafsi zetu kwenye dhabihu iliyo “kuu na ya mwisho” (Alma 34:10). Je, unafundisha kuhusu umoja? Fikiria kujadili umoja Yesu Kristo alioupata pamoja na Baba Yake na mwaliko Wake kwetu wa kuwa wamoja pamoja Nao (ona Yohana 17). Ona kila mada ya injili kama ni fursa ya kufundisha na kujifunza kuhusu Yesu Kristo.

Kila amri pia inatoa fursa hii. Usifokasi tu juu ya sheria za injili—jifunze pia kuhusu Mtoa Sheria huyo. Kama mnajadili Neno la Hekima na mkasimama katika ya kufanya na yasiyo ya kufanya juu ya maisha bora, unakosa fursa ya kutafakari jinsi gani Yesu Kristo anajali kutuhusu sisi—vyote ustawi wetu wa kimwili na wa kiroho—hata akatupatia sisi sheria hii. Fokasi juu ya jinsi gani Mwokozi alivyo tayari na mwenye shauku ya kutubariki sisi kwa nguvu Yake ili kutusaidia kuishi sheria Zake. Kila sheria Yeye anayotupatia inafunua kitu fulani kuhusu mawazo, mapenzi, na moyo Wake—tafuteni shangwe katika kugundua hili pamoja!

Sisitiza Mfano wa Yesu Kristo

Tunaweza kumweka Yesu Kristo kwenye kitovu cha kufundisha na kujifunza kwa kutambua na kusisitiza kwamba Yeye ni mfano mkamilifu wa kanuni zote za injili. Kama wafuasi, hatufuati tu kanuni—tunamfuata Yesu Kristo. Tunapofokasi juu ya mfano mkamilifu wa Mwokozi, Roho Mtakatifu atashuhudia juu Yake na kutushawishi tumfuate Yeye.

Tafakari kwa dakika chache kwamba unafundisha kanuni ya kuvumilia hadi mwisho. Mjadala kuhusu jinsi gani Mwokozi ni mfano wa kuvumilia hadi mwisho kungeweza kuleta hisia unyenyekevu mtamu Kwake Yeye. Wale unaowafundisha wanaweza kujifunza na kuhisi nini kutokana na mfano Wake?

Picha
Mwokozi akimponya mtu aliyelala chini

Mwokozi aliweka mfano mkamilifu kwa ajili ya sisi sote. Aliwaponya Wote, na Michael Malm

Fundisha kuhusu Majina, Wajibu, na Sifa za Yesu Kristo

Yesu Kristo ana majina mengi katika maandiko. Kila moja linaakisi moja ya Wajibu Wake katika mpango wa Mungu na linatufundisha sisi kuhusu sifa Zake za kiungu. Unaweza kufikiria kuchunguza pamoja na wanafunzi majina kama Kondoo wa Mungu, Mwombezi, Mtimizaji wa Imani Yetu, na Nuru ya Ulimwengu yanatufundisha nini kuhusu Yesu Kristo. Pia, unapowasaidia wanafunzi kuja kujua zaidi kuhusu Mwokozi, nenda mbali zaidi ya kile alichosema na kufanya kwamba Yeye ni nani na wajibu gani anaotaka kufanya katika maisha yetu. Mnapojifunza pamoja kuhusu sifa na tabia za Mwokozi, Roho Mtakatifu atazamisha kwa kina uelewa wako juu Yake na upendo wako kwake Yeye.

Tafuta Alama Ambazo Hushuhudia juu Yesu Kristo

“Vitu vyote,” Bwana alitangaza, “vimeumbwa na kutengenezwa ili vinishuhudie mimi” (Musa 6:63; ona pia 2 Nefi 11:4). Tukiwa na ukweli huu akilini, tunaweza kujifunza kuona wingi wa alama katika maandiko ambazo zinashuhudia juu ya Mwokozi. Alama hizi zinajumuisha vitu kama mkate, maji, na nuru. Mara tunapokuwa tumeelewa jinsi gani vitu hivi vinahusiana na Mwokozi, vinaweza kutufundisha juu ya nguvu Zake na sifa Zake. Unaweza hata kuona mifanano ya maisha ya Mwokozi katika maisha ya manabii na watu wengine wake kwa waume walio waaminifu katika maandiko Kuzitafuta alama kunafunua kweli kuhusu Mwokozi katika mahali ambapo vinginevyo ungepasahau.

Chapisha