Seminari na Vyuo
Kwa ajili ya Viongozi—Kuwasaidia Walimu Wafanikiwe


“Kwa Ajili ya Viongozi—Kuwasaidia Walimu Wafanikiwe,” Kufundisha katika Njia ya Mwokozi: Kwa Ajili ya Wote Wanaofundisha Nyumbani na Kanisani (2022)

“Kwa ajili ya Viongozi—Kuwasaidia Walimu Wafanikiwe,” Kufundisha katika Njia ya Mwokozi

Picha
Darasa la shule ya jumapili

Kwa ajili ya Viongozi—Kuwasaidia Walimu Wafanikiwe

Maingiliano na mmoja-mmoja

Mara nyingi njia bora ya kukidhi mahitaji ya kipekee ya walimu ni kukutana mmoja mmoja. Kwa mfano, kama kiongozi, ungeweza kuwa na majadiliano ya muda mfupi na mwalimu kabla au baada ya darasa ili kujadili kanuni za Kufundisha Katika Njia ya Mwokozi,. Ungeweza kujiandaa kwa majadiliano haya kwa kumwangalia mwalimu akifundisha. Tafuta kuelewa vyema nguvu ya huyo mwalimu na gundua njia unazoweza kumpatia msaada.

Kujenga juu ya nguvu za mwalimu ni muhimu kama ilivyo kutambua fursa za kuboresha. Ni ya msaada kuanza majadiliano na walimu kwa kuwaomba wao wenyewe wafikirie kile kinachoenda vyema na wapi wanadhani maboresho yanaweza kufanyika.

Unapokutana na walimu, fikiria njia za kuwaimarisha na kuwatia moyo kwa ukarimu na shukrani kwa ajili ya huduma wanayotoa.

Mikutano ya Baraza la Walimu

Kila kata inapaswa kuwa na mikutano ya baraza la walimu kila robo ya mwaka ambapo walimu wanaweza kushauriana pamoja kuhusu kanuni za kufundisha kama Kristo. Mikutano ya baraza la walimu inaweza pia kufanyika kwa ajili ya wazazi (ona Kitabu cha Maelezo ya Jumla: Kuhudumu katika Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, 13.5, ChurchofJesusChrist.org).

Ni Wakati Gani Mikutano Hii Inapaswa Kufanyika?

Mikutano ya baraza la walimu inafanyika wakati wa darasa la dakika 50 katika ratiba ya Jumapili.

  • Walimu wa Ukuhani, Muungano wa Usaidizi wa Akina Mama, na Wasichana wanaweza kuhudhuria mojawapo ya Jumapili ya kwanza au ya tatu, kama itakavyoamuliwa na viongozi wa eneo hilo.

  • Walimu wa Shule ya Jumapili wanaweza kuhudhuria mojawapo ya Jumapili ya pili au ya nne, kama itakavyoamuliwa na viongozi wa eneo hilo.

  • Walimu wa Msingi wanaweza kuhudhuria Jumapili yoyote, jinsi itakavyoamuliwa na urais wa kata wa Msingi na Shule ya Jumapili. Ikiwa itapendekezwa, Walimu wa Msingi wanaweza kukutana kando na walimu wengine ili washauriane kuhusu mahitaji ya kipekee ya watoto wanaowafundisha. Hii inaweza kutokea wakati wa dakika 20 za wakati wa kuimba, kabla au baada ya mikutano ya kila Jumapili, au katika siku nyingine katika wiki. Zaidi ya mkutano mmoja wa baraza la mwalimu inaweza kufanyika katika robo mwaka kwa ajili ya walimu wa msingi, ili kwamba wote wasije kosa madarasa ya Msingi katika wiki hiyo. (Maelezo: Kama inavyohitajika, urais wa Msingi huwateua walimu mbadala, huunganisha madarasa, au kufanya mipango mingine ili kuwaruhusu walimu wa Msingi kuhudhuria mikutano ya baraza la walimu.)

  • Mikutano ya baraza la mwalimu kwa ajili ya wazazi inaweza kufanyika Jumapili yo yote, kama itaamuliwa na baraza la kata.

Ni Nani Anapaswa Kuhudhuria?

Kila mtu anayefundisha akidi au darasa katika kata anapaswa kuhudhuria, pamoja na angalau mmoja wa viongozi wa ukuhani na kikundi walio na wajibu juu ya akidi au madarasa hayo. Kama itabidi, washiriki wanaweza kugawanywa katika vikundi kulingana na mahitaji ya wale ambao wanawafundisha. Kwa mfano, walimu wa vijana au watoto wanaweza kunufaika kwa kukutana pekee yao mara chache ili kujadili maswala ambayo ni mahususi kwa kufundisha vijana au watoto.

Kwa ajili ya mikutano ya baraza la mwalimu kwa ajili ya wazazi, baraza la kata linaamua kama linawaalika wazazi mahususi au kuweka mahudhurio wazi kwa ye yote anataka kushiriki.

Ni Nani Huongoza Mikutano Hii?

Baraza la kata, pamoja na usaidizi kutoka kwa urais wa Shule ya Jumapili, husimamia mikutano ya baraza la walimu. Wanashauriana pamoja kuhusu mahitaji ya walimu na wanafunzi kutokana na kile walichokiona darasani na mikutanoni. Wanafanya kazi pamoja kuamua ni kanuni gani na desturi kutoka katika Kufundisha katika Njia ya Mwokozi zitakidhi vyema mahitaji waliyoyaona.

Kwa kawaida, rais wa Shule ya Jumapili, huongoza mikutano ya baraza la walimu. Hata hivyo, washiriki wengine wa kata wanaweza kupangiwa kuongoza mikutano hiyo mara moja moja. Urais wa akidi na kikundi husisitiza kwa pamoja na walimu wao kanuni na desturi zilizojadiliwa katika mkutano.

Ni Nini Kinapaswa Kutendeka katika Mkutano wa Baraza la Walimu?

Mkutano wa baraza la walimu unapaswa kufuata utaratibu huu:

  • Shiriki na mshauriane kwa pamoja. Alika walimu waelezee uzoefu wa kufundisha wa hivi karibuni, uliza maswali yanayohusiana na kufundisha, na elezea mawazo juu ya kushinda changamoto. Sehemu hii ya mkutano inaweza kujumuisha marejeo ya kanuni zilizojadiliwa katika mikutano iliyopita.

  • Jifunzeni Pamoja. Waalike walimu kujadili moja wapo ya kanuni zifuatazo zilizowasilishwa katika kitabu hiki: fokasi juu ya Yesu Kristo, wapende wale unaowafundisha, fundisha kupitia Roho, fundisha mafundisho rasmi, na alika kujifunza kwa bidii. Kanuni zinaweza kushughulikiwa kwa mpangilio wowote, na isipokuwa ielekezwe vinginevyo na baraza la kata, washiriki katika mkutano wanaweza kuchagua kanuni itakayojadiliwa. Unaweza ukatumia zaidi ya mkutano mmoja kujadili kanuni moja ikibidi.

  • Panga na Ualike. Wasaidie walimu kupanga namna watakavyo zitumia kanuni walizozijadili. Kama inavyofaa, mngeweza pia kufanyia mazoezi kwa pamoja ujuzi mlioujadili. Waalike kuandika na kutenda juu ya misukumo yoyote ambayo wanapokea kuhusu jinsi ya kutumia kanuni katika kufundisha kwao—ikiwa ni pamoja na juhudi zao katika kufundisha majumbani mwao. Wahimize waanze kusoma kanuni inayofuata itakayojadiliwa.

Kadiri iwezekanavyo, mikutano ya baraza la walimu inapaswa kuwa mfano wa kanuni ambazo zinajadiliwa.

Picha
wasichana wakikumbatiana

Mikutano ya baraza la walimu inaweza kuwasaidia walimu kuelewa vyema kutumia kanuni za kufundisha kama Kristo.

Kuwaelekeza Walimu Wapya Walioitwa

Kama kiongozi, unalo jukumu la “kukutana na walimu wapya walioitwa” katika kikundi chako na “kuwasaidia kujianda kwa ajili ya miito yao” (Kitabu cha Maelezo ya Jumla, 17.3, ChurchofJesusChrist.org). Mikutano hii ni fursa ya kuwatambulisha walimu wageni kwa miito yao mitakatifu na kuwahamasisha na ono la maana ya kufundisha katika njia ya Mwokozi. Kama kiongozi, unaweza kuwasaidia walimu wageni kujiandaa kuhudumu kwa kufanya mambo yafuatayo:

  • Elezea kujiamini kwamba Mwokozi atawasaidia katika wito wao (ona Mafundisho na Maagano 88:78).

  • Wape walimu wapya nakala ya nyenzo hii, na watie moyo kutafuta njia za kutumia kanuni zake katika kufundisha.

  • Shiriki na walimu wapya kitu cho chote kuhusu kikundi chako ambacho kitakuwa msaada kwao kujua.

  • Kama inavyohitajika, mwambie mwalimu mgeni ni chumba gani atakachotumia kufundisha na somo atakaloanza nalo. Toa taarifa yo yote wanayohitaji kuhusu darasa na washiriki wa darasa.

  • Waelezee walimu wapya kwamba unaweza kuwasaidia katika wito wao. Toa msaada darasani na kwa upatikanaji wa nyenzo kama itahitajika.

  • Jitolee kuangalia darasa mara kwa mara, na toa mrejesho kama utakavyoongozwa na Roho.

  • Waalike walimu kushiriki katika mikutano ya robo mwaka ya baraza la walimu.

Chapisha