2022
Mungu Anaweza Kutusaidia katika Nyakati Ngumu
Machi 2022


“Mungu Anaweza Kutusaidia Katika Nyakati ngumu,” Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana, Machi 2022.

Mungu Anaweza Kutusaidia katika Nyakati Ngumu

Yesu Kristo anajua jinsi ya kutusaidia kila mmoja wetu, bila kujali majaribu yetu.

Picha
Yesu Kristo

Kristo Alitembea juu ya Maji, na Walter Rane

Nakumbuka jinsi nilivyohisi nilipokuwa kijana, kuishi katika nyakati ambazo zilionekana kuwa ngumu. Palikuwa na vita vya dunia vikiendelea. Vijana wa umri mdogo tu kuliko mimi walikuwa wakiuawa katika vita. Kulikuwa na mapigano ya genge katika vitongoji vya karibu. Mporomoko wa uchumi ulimwenguni ulikuwa haujaisha, na watu wengi walikuwa masikini. Familia yangu na mimi tu ndio tulikuwa Watakatifu wa Siku za Mwisho katika mji tulioishi.

Hata hivyo, nilikuwa na furaha na matumaini. Nilikuwa nimefundishwa, kama ulivyokuwa umejifunza, kwamba majaribu yetu ni baraka inayowezekana ikiwa yatatugeuzia kwa Baba wa Mbinguni na Mwokozi kwa msaada.

Kwa nini Majaribu?

Majaribu yanatupa nafasi nzuri ya kuchagua kutumia imani. Tunaweza kuomba kupitia sala kwa ajili ya msaada kutoka kwa Yesu Kristo, ambaye anajua jinsi ya kutusaidia. Alipata kila jaribu tutakalokabiliana nalo. Anajua kabisa jinsi ya kumsaidia kila mmoja wetu. Na Yeye anatupenda.

Kusudi la changamoto maishani ni kuona ni nini tutakachochagua kufanya. Je! Tutatumia imani kushika amri alizotupatia katika majaribu yoyote tunayokabiliana nayo? Mungu mwenye upendo siku zote hufanya yale ambayo ni bora kwetu. Anaweza kuondoa au kupunguza mtihani wetu ikiwa hiyo itaimarisha imani yetu. Nyakati zingine, Anaweza asifanye hivyo.

Unapojifunza maisha ya kale ya manabii katika Agano la Kale umeona jinsi Bwana anavyotusaidia hatua kwa hatua kuinuka kupitia majaribu magumu. Kwa mfano, njia ya Bwana ya kumsaidia Yusufu na Musa ilinifundisha jinsi ya kuomba na kupokea msaada katika nyakati ngumu.

Majaribu ya Yusufu

Yusufu, mwana mpendwa wa Yakobo, alitupwa ndani ya shimo na ndugu zake na kisha kuuzwa utumwani Misri. Baba yake aliambiwa na ndugu zake kwamba alikuwa ameuawa. Wakati Yusufu akiwa mtumwa, Bwana alimpa uwezo wa kutafsiri ndoto za Farao. Alimwonyesha Yusufu jinsi Misri inavyoweza kukabiliana na njaa hapo baadaye. Alimpa Yusufu nguvu ya maadili ya kupinga jaribu, kuachiliwa kutoka gerezani, na akiwa na umri wa miaka 32 kuinuliwa hadi ofisi ya juu na Farao. Farao alisema juu ya Yusufu, “Je, Tunaweza kupata mtu kama huyu, mtu ambaye Roho wa Mungu yumo ndani yake?”1

Somo kwangu kutoka jinsi Bwana alivyomsaidia Yusufu ni jinsi anavyoweza kutusaidia katika nyakati ngumu. Wakati Yusufu aliendelea kufanya uchaguzi mzuri, Bwana alimtia nguvu Yusufu, akampa nguvu za kiroho, na kulainisha mioyo ya watu walio karibu naye.

Picha
Bwana anamtokea Musa

Musa Anamwona Yehova, na Joseph Brickey

Majaribu ya Musa

Vivyo hivyo, msaada wa Bwana kwa Musa katika majaribu yake ulikuwa sawa na msaada Wake kwa Yusufu. Majaribu ya Musa pia yalianza katika ujana wake. Musa alitengwa toka kwa wazazi wake. Jaribio lake la mwanzo lilikuwa la kulelewa na binti wa Farao. Katika kumtetea Mwisraeli, alimuua Mmisri na ilimbidi akimbilie jangwani.

Bwana alimtokea Musa na kumwita awatoe watoto wa Israeli kutoka utumwani Misri. Jukumu hilo lililonekana kuwa haliwezekani lilikuwa jaribio ambalo Musa alihisi lilikuwa nje ya uwezo wake. Majaribu magumu na majaribio ya maisha yako yanaweza kuja wakati unapewa kazi na Bwana ambayo inaonekana kuwa ngumu sana na unahisi kuwa unahitaji msaada wa Mungu.

Bwana alianza kwa kumpa Musa msaada utakaouhitaji. Alimwambia Musa kuwa atakuwa ni Yeye ambaye angemtia nguvu kupita majaribu mbele yake.

“Mimi ndimi nilivyo: na… ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli, Mimi ndimi amenituma kwenu.2 Kwa hakikisho hilo, Musa alipata imani na nguvu kwa mfululizo wa majaribio mbele yake katika kazi yake aliyopewa. Sio tu kwamba Bwana alimwita lakini Bwana angeenda mbele ya uso wake kwa njia zinazoonekana za kimiujiza.

Picha
Yesu Kristo

Nuru ya Ulimwengu, na Walter Rane

Majaribu Yako

Nyakati ngumu ambazo mimi na wewe tutakutana nazo zitakuwa za kipekee. Watu wawili hawawezi kuwa sawa. Majaribu huwekwa kuendana na kila mmoja wetu kwa ruhusa ya Baba wa Mbinguni mwenye upendo na Mwanawe Mpendwa, Yesu Kristo. Njia ambayo Wanajibu maombi yetu ya kutaka msaada itakuwa ni kila kitu kinachofaa kwetu. Kwa wengine inaweza kutuimarisha, na kwa wengine inaweza kutupatia furaha tunapopambana katika imani.

Kwa sisi sote, msaada tunaohitaji zaidi tunapojaribiwa, kwa njia zozote na kwa muda mrefu, ni imani mahiri katika Yesu Kristo. Ilikuwa imani hiyo ambayo ilimruhusu Yusufu kutafsiri ndoto huko Misri. Ilikuwa imani ya kweli kwa Yesu Kristo ambayo ilimtia nguvu na kumuimarisha Musa katika kazi yake ngumu kumsaidia Bwana kuwakomboa watu Wake.

Katika ujana wako, tayari umejaribiwa na nyakati ngumu, kama ilivyokuwa kwangu. Lakini kama mimi, umefundishwa kumtumaini Yesu Kristo. Natambua sasa kwa nini nilihisi matumaini na hata furaha wakati nikiwa mdogo. Sio kwamba nilitarajia nyakati ziwe bora au rahisi. Ilikuwa kwamba nilihisi ujasiri kwamba ikiwa ningemwamini na kumtumikia, yote yangekuwa sawa.

Bibi yangu alimuomba baba yangu aimbe naye njiani wakirudi nyumbani kutoka kuambiwa angekufa hivi karibuni kutokana na saratani: “Na ikiwa tunakufa kabla ya safari yetu, … Yote ni sawa! Yote ni sawa”3 Ninatoa ushuhuda kwamba Yesu Kristo aliyefufuka anajua jinsi ya kutusaidia kila mmoja wetu, bila kujali majaribu yetu. Tunahitaji tu kumuomba kwa imani Kwake.

Yesu Kristo anakupenda na atakusaidia, wakati wote, na kulingana na kilicho bora kwako. Nashuhudia hivyo, nikiwa na upendo kwenu, na Kwake, katika jina la Yesu Kristo, amina.

Chapisha