Njoo, Unifuate
Jumapili ya Pili na ya Tatu


“Mikutano ya Jumapili ya pili na ya tatu,” Njoo, Unifuate—Kwa ajili ya Ukuhani wa Melkizedeki na Muungano wa Usaidizi wa akina Mama (2017)

Mikutano ya Jumapili ya Pili na ya Tatu

Mikutano ya Jumapili ya Pili na ya Tatu

Jumapili ya pili na ya tatu ya kila mwezi, akidi za Ukuhani wa Melkizedeki na Muungano wa Usaidizi wa akina Mama husoma mafunzo ya manabii wanaoishi, Mitume na viongozi wengine wa kanisa kutoka kwenye Mkutano Mkuu wa hivi karibuni. Ujumbe wowote kutoka Mkutano mkuu wa hivi karibuni unaweza kujadiliwa.

Mara nyingi, urais wa akidi, uongozi wa kikundi, au urais wa Usaidizi wa akina Mama watachagua ujumbe wa kusoma wa mkutano kulingana na mahitaji ya washiriki, ingawa askofu au rais wa kigingi anaweza changia. Viongozi wanaweza kuchagua ujumbe unaoshabihiana na mada iliyojadiliwa kwenye Jumapili ya kwanza ya baraza, au wanaweza kuchagua ujumbe mwingine kulingana na uvuvio wa Roho. Viongozi na waalimu hawana budi kupata njia za kuwahimiza washiriki kusoma jumbe teule mapema, na kuja wakiwa wamejiandaa kushiriki mawazo. Mapendekezo yafuatayo ya jinsi ya kujifunza, kulingana na kanuni kutoka Kufundisha katika njia ya Mwokozi, yanaweza kuwashirikisha washiriki katika kujifunza kutoka kwenye jumbe za Mkutanao Mkuu.

Sharon Eubank, “Washeni Taa Zenu

Waulize washiriki wa akidi yako au Muungano wa Usaidizi wa akina Mama kufikiria jinsi gani maisha yao yameshawishiwa kwa wema kupitia mwanamke mwema na muaminifu. Fikiria kuwaalika baadhi ya washiriki kushiriki jinsi gani mwanamke huyu huelezea sifa moja au zaidi ya mwanamke mwema ilivyoelezewa katika ujumbe wa Dada Eubank. Tunajifunza nini kutoka kwa Dada Eubank kuhusu jinsi gani tunaweza “kuwa jeshi muhimu katika ukuaji wa idadi na kiroho wa Kanisa katika siku za mwisho”?

Neill F. Marriott, “Kukaa katika Mungu na kuziba ufa

Ujumbe huu unaweza kuwasaidia washiriki ambao wanaweza kuhisi kutengwa kutoka kwa Baba wa Mbinguni au kutoka kwa wale wanaowazunguka. Nini kingewasaidia wale unaowafundisha kuelewa ufa ni nini? Labda ungeweza kuleta picha za nyufa za aina mbalimbali. Ni kwa namna gani Dada Marriott ameuelezea ufa? Nini kinaweza kusababisha ufa katika uhusiano wetu na Mungu na wengine? Waalike washiriki kutafuta ujumbe wa Dada Marriott kwa ajili ya mapendekezo ya jinsi gani tunaweza kufanya kuziba nyufa katika maisha yetu. Wape washiriki muda wa kuandika kile Roho amewasukuma kufanya kuwa karibu na zaidi na Mungu na wengine.

Joy D. Jones, “Thamani kuzidi kipimo

Baraka zipi hutiririka katika maisha yetu pale tunapoelewa utambulisho wetu wa kitakatifu? Kujibu swali hili, washiriki wa akidi au muungano wa Usaidizi wa akina Mama wangeweza kupitia hadhithi ya Mariama, Renu na Taiana katika ujumbe wa Dada Jones. Ushauri gani Dada Jones anatoa kutusaidia “kukumbuka na kuthamini utambulisho wetu wa kitakatifu”? Waalike washiriki kutafuta na kujadili sehemu ya maandiko matakatifu au nukuu katika ujumbe wa Dada Jones ambayo itawasaidia kuelewa thamani yao halisi kwa Mungu. Waalike kushiriki moja ya maandiko haya matakatifu au nukuu na mtu mwingine amabye anahitaji kukumbushwa thamani yake takatifu.

Dieter F. Uchtdorf, “Dada Watatu

Njia mojawapo ya kupitia ujumbe wa Rais Ucthdorf ingekuwa ni kugawanya akidi au muungano wa Usaidizi wa akina Mama katika makundi madogo. Ungeweza kupangia kila kundi kusoma kuhusu mmoja kati ya dada katika ujumbe wa Rais Uchtdorf. Kila kundi lingeweza kuandika barua kwa dada huyo likifupisha ushauri wa Rais Uchtdorf na kushiriki kile walichoandika na makundi mengine. Tunaweza kufanya nini ili tuweze kuwa zaidi kama dada wa tatu? Tunawezaje kufanya akidi zetu au muungano wa Usaidizi wa akina Mama “nyumba salama” kwa wale wanaosumbuka?

Dieter F. Uchtdorf, “Kutamani nyumbani

Unawezaje kuwasaidia wale unaowafundisha kutambua jinsi gani Mungu huwatumia kuwabariki wengine? Ungeweza kuwaalika kupitia sehemu ya ujumbe wa Rais Uchtdorf wenye kichwa cha habari “Mungu atakutumia,” wakiangalia ahadi zilizotolewa kwa wale wanaojitahidi kumtumikia katika ufalme wa Mungu licha ya mapungufungu. Kusoma ujumbe huu kunaweza kuwakumbusha washiriki uzoefu ambao wangeweza shiriki wakati Mungu alipowatumia kubariki wengine—au alipotumia wengine kuwabariki. Wape washiriki muda wa kutafakari nini wamehisi kuvuviwa kufanya kwa sababu ya majadiliano haya.

Bonnie L. Oscarson, “Wahitaji mbele Zetu

Njia mojawapo ya kuanza majadiliano kuhusu ujumbe wa Dada Oscarson ni kumpa kila mtu kipande cha karatasi na “Nani ananihitaji leo” ikiwa imeandikwa kwa juu. Washiriki wako wa muungano wa Usaidizi wa akina Mama au akidi wangeweza kuchukua dakika chache kutafakari na kusikiliza majibu ya swali hili. Halafu wangeweza kutafuta mawazo kutoka kwenye ujumbe wa Dada Oscarson jinsi gani wangeweza kuwatumikia watu katika orodha zao—au kuongeza majina kadiri wavuviwavyo. Labda wachache wangeshiriki nini wamejifunza.

Dallin H. Oaks, “Mpango na Tangazo

Ni kwa namna gani washiriki wa akidi yako, kikundi au muungano wa Usaidizi wa akina Mama wataitikia mwaliko wa Mzee Oaks “kufundisha [na] kuishi kulingana” na tangazo la familia nyumbani, katika jamii, na kanisani? Waalike kushiriki mawazo yao wao kwa wao. Pia ingeweza kusaidia kutafuta ujumbe kwa ajili ya kauli za mafunzo kutoka kwenye tangazo la familia. NI kwa namna gani kauli hizi hutusaidia kuitikia “chngamaoto zilizopo za familia”? Sehemu ya IV ya ujumbe wa Mzee Oaks imebeba baadhi ya mifano ya kauli hizo.

D. Todd Christofferson, “Mkate Ulio Hai Ambao Ulishuka Kutoka Mbinguni

Haya ni baadhi ya maswali washiriki wa muungano wa Usaidizi wa akina Mama na akidi wangeweza kuwa nayo katika mawazo yao wakati wakipitia ujumbe wa Mzee Christofferson: Utakatifu ni nini? Tunautafutaje utakatifu? NI kwa namna gani kuchukua sakramenti hutusaidia katika juhudi zetu? Washiriki wangeweza kushiriki maneno ya kutoka kwa Mzee Christofferson ambayo yanasaidia kujibu maswali haya. Ni kwa nanmna gani tunasaidiana kama “watakatifu” katika juhudi zetu za kuwa watakatifu zaidi?

Jeffrey R. Holland, “Hatimaye—Muwe Wakamilifu

Baadhi ya wale unaowafundisha wanaweza kuhisi kwamba hawafikii kiwango kinachotakiwa linapokuja suala la kuishi mafundisho ya Kristo. Ni nini Mzee Holland anafundisha ambacho kinaweza kuwafariji na kuwahamasisha wale wanaojisikia namna hii? Ungeweza kuwaalika washiriki wa akidi na muungano wa Usaidizi wa akina Mama kutafuta kitu katika ujumbe huu amabcho wangeweza kushiriki na mwingine ambaye anasumbuliwa kwa kuhisi kuwa “si wazuri vya kutosha.” Au wangeweza kupata kitu katika ujumbe huu ambacho kinawavuvia kuhisi “upendo mkuu na uvutiwaji kwa [Kristo] na hamu kubwa ya kuwa kama Yeye.”

Gary E. Stevenson, “Kupatwa Kiroho

Kuna mshiriki yoyote wa akidi au muungano wa Usaidizi wa akina Mama amewahi kupata uzoefu wa kupatwa kwa jua? Kama ndivyo, ungeweza kumwalika mmoja wao kuelezea analojia ambayo Mzee Stevenson ameshiriki kuhusu “kupatwa kiroho.” Ni vizuizi gani vina “weza kuzuia uwezo, mwangaza na joto la mwanga wa Yesu Kristo na injili Yake’? NI kwa namna gani mitandao ya kijamii hutusonga kutoka kwenye “uzuri, joto, na mwangaza wa kimbingu wa injili”? Ni kwa namna gani tunavaa “miwani za kiinjili” ambazo hutukinga kutokana upofu wa kiroho? Ni nini analogia ya Mzee Stevenson hutufundisha kuhusu kuendelea na mtazamo wa injili?

Quentin L. Cook, “Kila Siku ya Milele

Ujumbe wa Mzee Cook unatukumbusha juu ya umuhimu wa kujitahidi kuwa wanyenyekevu katika njia mbalimbali. Njia mojawapo ya ujadili kile anachofundisha ni kuwagawanya washiriki katika makundi. Uliza kundi moja kutafuta mapendekezo kutoka Ujumbe wa Mzee Cook ambayo yangeweza kutusaidia kutengeneza unyenyekevu, na kundi jingine kutafuta njia ambazo watu hudhihirisha kujikweza. Alika kila kundi kushiriki maelezo yao na kundi lingine. Pia washiriki wangeweza kushiriki njia ambazo wanaweza kuonyesha “unyenyekevu wa kila siku” katika maisha yao na kufikiria jinsi gani unyenyekevu ungeweza kusaidia kuwaandaa kukutana na Mungu.

Ronald A. Rasband, “Kwa Mpango Mtakatifu

Ili kuhamasisha majadiliano juu ya ujumbe wa Mzee Rasband, ingeweza kusaidia kuwaalika washiriki wachache kuleta sehemu iliyofumwa, muswada au kiamba upishi na ujumbe kuhusu kwa nini hivi husaidia. NI mifano gani au mafunzo kutoka kwenye ujumbe wa Mzee Rsaband huvuvia washiriki kutambua mpango wa Mungu kwa ajili ya maisha yao? Labda washiriki wa darasa wangeweza kushiriki uzoefu ambao waliona Bwana alikuwa akiongoza maisha yao. Wamefanya nini kuonyesha kuwa “wanatahmini” uelekezi wake? Kwa nini Kwa nini ni muhimu kutambua “mpango mtakatifu” wa Mungu?

Russell M. Nelson, “Kitabu cha Mormoni: Bila hicho Maisha Yako Yangekuwaje?

Rais Nelson aliwaalika washiriki kufikiria kuhusu maswali matatu: (1) “maisha yako yangekuwaje bila Kitabu cha Mormoni?” (2) “ungekuwa hujui nini?” (3) “ungekuwa huna nini?” Waalike washiriki wa akidi, kundi, au muungano wa Usaidizi wa akina Mama kutafakari maswali haya na kushiriki ni kwa namna gani wangeyajibu. Nini wanapata kutoka kwenye ujumbe huu ambacho kinawavuvia kuthamini zaidi Kitabu cha Mormoni kuliko “almasi au rubi”?

Dale G. Renlund, “Ukuhani na Nguvu ya Upatanisho wa Mwokozi

Ni kwa namna gani unaweza kuwasaidia washiriki wa akidi yako au muungano wa Usaidizi wa akina Mama kuelewa ni kwa namna gani ukuhani husaidia kufanya baraka za Upatanisho wa Kristo kupatikana kwao? Ungeweza kuandika vichwa vya habari hivi viwili ubaoni: “Kwa nini tunahitaji upatanisho wa Yesu Kristo” Ni kwa namna gani ukuhani ‘huleta’ kwetu baraka za Upatanisho. Kisha waalike washiriki kutafuta ujumbe wa Mzee Renlund, wakiangalia maneno ya kuandika chini ya kila kichwa cha habari. NI kwa naman gani ukuhani na ibada zake husaidia kutimiza lengo la Baba wa Minguni kwa watoto Wake?

Dieter F. Uchtdorf, “Wabebao Mwangaza wa Kimbingu

Waalike washiriki kutafuta ujumbe wa Rais Uchtdorf na kubaini ni kwa namna gani uwepo au kutokuwepo kwa mwangaza wa kitukufu kunaweza kuathiri maish yetu. Ungeweza kuwaalika washiriki kusoma baadhi ya maandiko ambayo Rais Uchtdorf ameyarejea na kubaini kweli zinazohusiana na mwangaza wa kiroho. Ni nini metamofosisi ya kupatwa kwa jua hutufundisha kuhusu kazi ya uhuru wa kuchagua katika kutafuta mwangaza wa kiroho? Tunaweza kufanya nini ili kushiriki Mwangaza mtakatifu wa Kristo na wengine, hasa na familia zetu na “vijana wetu ambao wanatafuta mwangaza”?

Henry B. Eyring, “Bwana Anaongoza Kanisa Lake

Waalike washiriki wa akidi yako na muungano wa Usaidizi wa akina Mama kushiriki uzoefu ambao kwayo walihitaji kujenga imani kwamba wito wao au wito wa mwingine ulitoka kwa Mungu. Ni kwa namna gani walitumia imani? Ni kwa namna gani walikuja kujifunza kwamba wito wao ulitooka kwa Mungu? Waalike washiriki kutafuta ujumbe wa Rais Eyring na kubaini kweli alizojifunza kupitia uzoefu wake binafsi ambao unaweza kutusaidia kuamnini na kuwa wavumilivu kwetu sisi wenyewe na kwa wenzetu ambao Bwana amewaita.

Jean B. Bingham, “Kwamba Shangwe Yenu Iwe Timilifu

Ujumbe wa Dada Bingham unaweza kuwasaidia washiriki usaidizi wa akina Mama na akidi kuelewa jinsi ya kupata shangwe, tunapokuja kwa Kristo, licha ya magumu ya kimaisha. Njia mojawapo ya kujadili ujumbe wake ingeweza kuwa ni kuchora njia ubaoni ikilelekea kwenye neno shangwe Waalike washiriki kadhaa kuandika kuandika njia mapendekezo kutoka kwenye ujumbe wa Dada Bimgham ambayo hupelekea shangwe ya kweli. Wahamasishe washiriki kufikiria njia ambazo wanaweza kuitikia ushauri wa Dada Bingham. Waalike baadhi ya washiriki kushiriki mawazo yao.

David A. Bednar, “Ahadi za Thamani na Kuu sana

Ili kuwasaidia washiriki wa Usaidizi wa akina Mamana au akidi kujadili ujumbe wa Mzee Bednarr, ungeweza kuweka picha kwenye ubao zikiwakilisha Sabato, Hekalu, na nyumba zetu. Waalike washiriki kusoma sehemu inayoendana na ujumbe wa Mzee Bednar na andika ubaoni ni kwa naman gani siku ya Sabato, Hekalu, na nyumba zetu hutusaidia kulenga katika ahadi za Mungu kwetu. Ni vitu vipi katika maisha yetu vinavyoweza kuvuta nathari yetu kutoka kwenye ahadi hizi? Ni hatua gani tunazoweza kuchukua ikuhakikisha kuwa tunamkumbuka?

Henry B. Eyring, “Usiogope Kutenda Mema

Ujumbe wa Rais Eyring unaweza kuwasaidia wale unaowafundisha kupata hamasa na imani kufanya yaliyo mema duniani. Ungeweza kuwaalika washiriki wachache kufupisha mifano ya watu waaminifu anaoshiriki Rais Eyring. Ni nini mifano hii inatufundisha kuhusu namna ya kuwatumikia wengine? Ni nini mifano hii inapendekeza kuhusu njia ambazo tunaweza kutumikia kama akidi au muungano wa Usaidizi wa akina Mama

Njia nyingine ya kushiriki ujumbe huu ni kuzipitia baraka ambazo Rais Eyring aliziona kwa kufuata ushauri wa Rais Thomas S. Monson wa kujifunza Kitabu cha Mormoni. Ni baraka gani tumeziona kwa kujifunza Kitabu cha Mormoni?

M. Russell Ballard, “Safari Inaendelea!

Ili kuanza majadiliano kuhusu ujumbe wa Mzee Ballard, ungeweza kumwalika mtu fulani kushiriki uzoefu wakati walikuwa na sehemu ya kufikia lakini wakagundua walikuwa kwenye njia isiyo sahihi. Ni kwa namna gani mifano kama hii hufananishwa na “safari” yetu ya kurudi kwa Baba wa Mbinguni? Washiriki wangeweza kutafuta ushauri na maonyo ambayo Mzee Ballard anatoa ambayo yanaweza kutusaidia kama tunaelekea katika uelekeo sahihi katika maisha yetu. Wape washiriki muda wa kutafakari njia zao wenyewe na kujadili njia ambazo tunaweza kuwasaidia na kuwatia moyo wengine katika “safari” ya kurudi kwa Baba wa Mbinguni.

Neil L. Andersen, “Sauti ya Bwana

Labda washiriki wa akidi yako au muungano wa Usaidizi wa akina Mama wangeweza kushiriki uzoefu ambao kwayo walihisi ujumbe wa mkutano mkuu ulikuwa wa maana hususan kwao. Kwa nini jumbe hizi zilikuwa za maana? NI nini Mzee Anderson anafundisha kuhusu umuhimu wa jumbe za mkutano mkuu na juhudi na mchakato unaohusika katika kuziandaa? Ni kwa nanma gani uelewa huu huathiri uahraka wetu wa kujifunza na kuitikia maneno haya? Fikiria kutengeneza orodha ya mialiko kutoka kwenye mkutano wa hivi karibuni. Tumefanya nini kuitikia mialiko hiyo?

Chapisha