2022
Ninajua Nitamwona Yeye Tena
Julai 2022


“Ninajua Nitamwona Yeye Tena,” Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana, Julai 2022.

Dhima na Mimi

Vijana wakielezea jinsi wanavyoishi maneno ya Dhima ya Wasichana na ya Akidi ya Ukuhani wa Haruni

Ninajua Nitamwona Yeye Tena

“Nitastahili kupokea baraka za hekaluni na furaha ya kudumu ya injili.”

Picha
mvulana

Ninaamini Bwana alitupatia familia ili tuweze kusaidia kuimarishana na kusaidiana. Bwana pia alitupa familia ili tusiwe peke yetu. Lakini baba yangu alipofariki, nilijihisi mpweke sana. Baba yangu na mimi tulikuwa karibu, na nilikuwa nimepoteza mfano wake wa kudumu. Nilihisi kama nilichoweza kufanya ni kulia tu.

Lakini usiku mmoja niliamua kuomba. Moyoni mwangu nilihisi Roho akiniambia kwamba sikuwa peke yangu. Ninajua mpango wa wokovu. Kwa sababu ya Upatanisho wa Yesu Kristo, nitamwona tena baba yangu. Elimu kwamba familia zinaweza kuwa pamoja milele ni muhimu sana kwangu. Na ninajua kwamba tunaweza kuwa familia ya milele kwa sababu wazazi wangu walikuwa wameunganishwa hekaluni.

Nilipofikisha umri wa miaka 12, nilikuwa nikipanga kuhudhuria hekalu ili kufanya ubatizo kwa ajili ya wafu kwa mara ya kwanza. Lakini wakati huo mahekalu yalifungwa kwa sababu ya janga. Ninatazamia sana kuwa ndani ya hekalu kwa mara ya kwanza ili kuhisi furaha huko.

Wakati kaka yangu alipounganishwa kwa mke wake, nilibaki nje ya hekalu. Lakini hata kutoka nje, nilihisi hisia nzuri moyoni mwangu. Kwa hivyo ninaweza kufikiria ni jinsi gani hisia za ndani zilivyo. Familia yangu iliniambia kwamba hekalu ni mahali ambapo tunaweza kufurahia mpango mkamilifu ambao Mungu ametuandalia.

Pia nimejifunza kutoka kwenye mafundisho ya manabii kwamba ninaweza kufanya maagano matakatifu katika hekalu. Kila agano tunalofanya hekaluni ni muhimu sana. Nilipokea kibali changu cha hekalu, na siwezi kusubiri kukitumia. Na ninajua kwamba siku moja nitakapounganishwa na mke wangu wa baadaye, nitaweza kuwa na familia yangu ya milele.

Mtunzi anaishi Culiacan, Mexico.

Chapisha