2022
Jambo Fulani Kubwa
Julai 2022


“Jambo Fulani Kubwa,” Kwa Ajili ya Nguvu Kwa Vijana, Julai 2022.

Njoo, Unifuate

2 Wafalme 5

Jambo Fulani Kubwa

Inatokea kwamba vitu vidogo na rahisi ni jambo kubwa sana.

Hebu sema una tatizo la afya ambalo halitatoka. Mtu anakuambia kuhusu mwanaume anayeweza kukuponya. Anaishi mbali, lakini unamuandikia ujumbe na kisha unafunga safari ili umuone na usikie anachotaka kusema.

Unapofika nyumbani kwake, msaidizi wake anatoka na kusema kuwa bosi wake anasema nenda kaoge kwenye mto ulio karibu.

Msaidizi anarudi nyuma, na unasalia ukiwa umekata tamaa. Unafikiri, “Nilikuja huku kote kwa ajili hiyo?”

Matarajio

Hiki ni kile kilichomtokea Naamani. Alikuwa nahodha wa Shamu—mtu aliyeheshimiwa sana na mwenye madaraka mengi. Lakini alikuwa na ukoma, ugonjwa mbaya sana wa ngozi.

Ingawa hakuwa Mwisraeli, alikuwa amesikia kuhusu nabii Elisha kwa sababu ya kijakazi kijana kutoka Israeli. Naamani aliamini ushuhuda wake kuhusu Elisha na Mungu wa Israeli. Basi akaenda kumwona Elisha. Naamani alipofika nyumbani kwa Elisha, Elisha alimtuma mjumbe, ambaye alimwambia Naamani aoge katika mto Yordani mara saba ili aponywe.

Picha
Naamani akimsikiliza mtumishi

Vielelezo na Corey Egbert

Naamani alikasirika. Alikuwa amewazia kwamba angekutana na Elisha na kwamba Elisha angeweka mkono wake pale pale kwenye ngozi iliyo na ugonjwa, amwite Mungu, na kuiponya kimuujiza. Hata alifikiri kwamba kulikuwa na mito bora zaidi huko nyumbani ambayo angeweza kuoga ndani yake.

Naamani aliweka matarajio. Yeye alitarajia Elisha angetoka nje na kumwona yeye. Huenda hii ilikuwa kwa sababu Naamani alikuwa na cheo cha juu sana na alizoea kupokea kiasi fulani cha heshima. Pia alitarajia suluhu la kimuujiza au la kuvutia zaidi kwa tatizo lake kuliko alilopewa. Labda hii ilikuwa kwa sababu ya hadithi alizosikia juu ya Elisha. Kwa hivyo uzoefu wake ulimfanya ahisi hasira sana.

Unyenyekevu

Lakini hadithi ya Naamani haiishi hapo. Mmoja wa watumishi wake alimpa ushauri wa busara sana:

“Kama yule nabii angalikuambia kutenda jambo kubwa, usingalilitenda? Je! Si zaidi basi, akikuambia, Jioshe, uwe safi? (2 Wafalme 5:13).

Naamani alitambua kwamba mtumishi huyo alikuwa sahihi. Kama nabii angemwambia afanye jambo kubwa, angalilifanya. Kwa hivyo kwa nini usifanye jambo rahisi? Alijinyenyekeza. Alijiosha mara saba katika Mto Yordani na aliponywa.

Picha
Naamani akioga katika Yordani

Vitu Vidogo na Rahisi

Mara kwa mara Bwana anaweza kumwomba mtu kufanya “jambo fulani kubwa.” Lakini hivyo sio kawaida jinsi Bwana anavyofanya kazi. Mara nyingi Yeye anatumia “vitu vilivyo vidogo na rahisi” ambavyo vinasababisha “mambo makuu” katika maisha yetu(Alma 37:6).

Wakati fulani matarajio yetu au kiburi chetu kinaweza kutufanya tufikiri kwamba njia ya Bwana ni rahisi sana au ndogo sana kustahili wakati wetu (ona 1 Nefi 17:40–41). Lakini Bwana anaweza kutusaidia kushinda hisia hizi na kujinyenyekeza. Anatupenda na anataka kutubariki na kutusaidia kuwa zaidi kama Yeye (ona Musa 1:39).

Hapa kuna mifano michache tu ya mambo madogo na rahisi ambayo Bwana anatutaka tufanye ili kumkaribia Yeye na kupokea baraka Zake.

Pengine unaweza kufikiria zaidi.

Kwa hiyo, unapokutana na kitu kidogo na rahisi, kuwa makini. Inaweza kuwa mwongozo katika kijitabu cha Kwa Ajili ya Nguvu Kwa Vijana ushauri fulani katika hotuba ya mkutano, au jambo ambalo askofu wako amekuomba ufanye. Vyovyote itakavyokuwa, mkumbuke Naamani, na uifanye tu. Inaweza kuwa ndogo, lakini baraka zitakuwa kubwa.

Chapisha