2022
Kujiandaa kwa ajili ya Hekalu la Dubai
Julai 2022


“Kujiandaa kwa ajili ya Hekalu la Dubai,” Kwa ajili ya Nguvu kwa Vijana, Julai 2022.

Kujiandaa kwa ajili ya Hekalu la Dubai

Vijana huko Dubai na Qatar wanashiriki upendo wao wa hekalu na msisimko wao kuhusu hekalu linalojengwa karibu yao.

Picha
mvulana

Picha za Saajan na Carla Nacario

Ni maneno machache tu rahisi, lakini yanabadilisha maisha yako yanaponenwa na nabii wa Mungu. Wakati wa mkutano mkuu, washiriki wa Kanisa kote ulimwenguni husikiliza kwa shauku matangazo mapya ya hekalu. Na kwa Sajaan na Gwen, mara Rais Russell M. Nelson alipozungumza maneno, “Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu,” katika mkutano mkuu wa Aprili 2020, vijana hawa wawili walijua maisha yao kamwe vile vile.1

Kutana na Saajan kutoka Dubai

Saajan mwenye umri wa miaka kumi na mbili hajawahi kuona hekalu ana kwa ana.

“Mama yangu daima alikuwa na lengo la kwenda hekaluni siku moja,” Saajan alisema. Upendo wake kwa hekalu unaambukiza. Sasa lengo langu maishani ni kutembelea hekalu.”

Saajan alizaliwa India, lakini wazazi wake walipotalikiana, alihama na mama yake hadi Umoja wa Falme za Kiarabu. “Mama yangu anafanya kazi kwa bidii sana. Yeye ni kama shujaa kwangu. Hata katika nyakati ngumu, hakati tamaa kamwe.”

Picha
mvulana na mama

Mama na bibi yake Saajan walijiunga na Kanisa nchini India miaka michache kabla hajazaliwa. Wanasoma Kitabu cha Mormoni na walijua kilikuwa ni jibu la maombi yao. Saajan alikua akienda kanisani na mama yake, na alibatizwa hivi majuzi baada ya kungoja ruhusa ya baba yake.

“Kubatizwa lilikuwa mojawapo ya maamuzi bora zaidi ambayo nimewahi kufanya,” akasema. “Na nilipopokea kipawa cha Roho Mtakatifu, nilihisi joto na furaha ndani.”

Sasa Saajan anapitisha sakramenti kwa kata yake na kujiandaa kuingia hekaluni. Alipokea kibali chake cha hekalu, na hawezi kusubiri kuingia katika Hekalu la Dubai United Arab Emirates litakapokamilika.

“Niliposikia kwamba walitangaza hekalu, mimi binafsi nilihisi ni kwa ajili yangu,” Saajan alisema. “Lilikuwa ni jibu la maombi yetu. Nilishtuka kwa sababu wanaijenga pale tunapoishi! Nitaweza kupanda treni moja kwa moja hadi hekaluni na kwenda mara nyingi nipendavyo. Pia nina furaha kwa Hekalu la Bengaluru India ambalo babu na nyanya yangu wataweza kutembelea.”

Picha
kijana akishikilia picha ya babu na bibi

Sajaan anafuraha kwa babu zake kwa kuwa na Hekalu la Bengaluru, India karibu nao.

Saajan anataka kufanya kazi ya hekalu kwa ajili ya mababu zake wengine pia.

Picha
mvulana na mama kwenye kompyuta

“Ninajitayarisha mimi mwenyewe ili niweze kustahili kuingia hekaluni. Ninataka kufanya niwezavyo kuwasaidia mababu zangu wote. Nina nafasi ya kusisimua sana ya kumtumikia Bwana na kufanya mambo yanayohusu ufalme wa Mungu.”

Kutana na Gwen kutoka Qatar

Picha
msichana

Picha ya Gwen na Christina Smith na kwa hisani ya familia yake

Katika miaka yake 18 ya kwanza ya maisha, Gwen ameishi katika nchi tano tofauti: Scotland, Angola, Uingereza, Kazakhstan, na Qatar. Kazi ya baba yake imewapeleka duniani kote, lakini hivi karibuni, Mashariki ya Kati.

Ndugu wakubwa wa Gwen wote wamehama, kwa hivyo anaishi Qatar na mama na baba yake. Mojawapo ya matukio yake aliyoyapenda sana yalikuwa ni kusafiri na vijana katika kata yake kwa safari ya hekalu hadi Hekalu la Kiev Ukraine. Hakuna hekalu karibu, kwa hivyo Watakatifu katika Mashariki ya Kati wanapaswa kusafiri kwa ndege kutembelea mahekalu katika nchi zingine.

“Nilifurahia sana safari yetu, na nilitaka kuleta majina ya familia,” alisema. “Kila siku nilikuwa nikipata majina ya familia kwenye simu yangu nikiwa njiani kuelekea na kurudi shuleni. Nilipata majina karibu 200. Nilihisi niko tayari sana kwenda!

Picha
kadi za hekaluni

Lakini kulikuwa na shida moja ndogo ambayo hangeweza kujiandaa.

Janga la kimataifa.

Ndege ya Gwen ilitua Ukraine mnamo Machi 2020—walipoanza kusikia zaidi juu ya kuenea kwa virusi vya UVIKO-19. Kwa usaidizi wa mbinguni, walifika hekaluni na kuweza kufanya ubatizo kwa majina ya familia ambayo Gwen alikuwa ametayarisha.

Picha
kundi la wasichana

“Kulikuwa na muujiza baada ya muujiza baada ya muujiza,” alisema. “Katika safari yetu ya kwenda hekaluni, nilikuwa na wasiwasi kuhusu janga hili. Lakini katika hekalu nilihisi tu amani na faraja nyingi. Na tuliweza kusafiri kwa ndege kurudi Qatar kabla ya mipaka kufungwa.

Picha
Wasichana wawili

Lakini mama yake Gwen, ambaye alikuwa ameenda kumtembelea mmoja wa ndugu za Gwen huko Marekani, hakuweza kurudi Qatar. Gwen na baba yake walikuwa wametengwa nyumbani wakati baba yake aliambukizwa UVIKO. “Kwa muda alikuwa mgonjwa sana na hakuweza kutembea sana,” Gwen alisema. Nilijihisi mpweke sana. Mama yangu alikuwa bado hayupo, na sikujua jinsi ya kutengeneza chakula kingine zaidi ya sandwichi ya jibini iliyochomwa.”

Lakini Gwen alipata tukio maalum alipokuwa akiendesha kanisa nyumbani na baba yake.

“Ilihisi kama watu ambao tulikuwa tumepeleka majina yao hekaluni walikuwa pamoja nami na baba yangu,” alisema. “Sikuhisi kuwa peke yangu tena. Ulikuwa ni uzoefu mzuri. Kutembelea hekalu kabla ya janga hilo ilikuwa baraka sana.

Picha
kundi la wavulana wakiwa mbele ya hekalu

Hekalu la Dubai United Arab Emirates lilitangazwa mwezi mmoja tu baada ya safari yake ya hekalu huko Ukraini. Gwen alifurahi sana! Na anajua jinsi jambo hilo litakavyokuwa na maana kwa watu wa eneo lake.

“Ninajua kuna watu katika eneo langu ambao hawana uwezo wa kusafiri kwa ndege hadi hekalu lingine huko Ulaya. Wamekuwa wakingoja kuunganishwa kama familia za milele. Inanionyesha kwamba mkusanyiko unafanyika kweli. Tunatayarisha njia kwa ajili ya Kristo kuja tena.

Baraka za Hekaluni

Jambo moja ambalo Gwen na Saajan wanalo sawa ni kwamba hekalu tayari linabariki maisha yao. Rais Nelson alisema, “Mahekalu ni sehemu ya kilele ya Urejesho wa utimilifu wa injili ya Yesu Kristo. Katika wema na ukarimu wa Mungu, anasogeza baraka za hekalu karibu na watoto Wake kila mahali.”2

Muhtasari

  1. Russell M. Nelson, “Songa Mbele kwa Imani,” mkutano mkuu wa Aprili 2020 (Ensign au Liahona,, Mei 2020, 115).

  2. Russsell M. Nelson, “Songa Mbele kwa Imani,” Mkutano mkuu wa Aprili 2020 (115–16).

Chapisha