Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana
Penda Kujifunza, Penda Kushiriki
Julai 2024


“Penda Kujifunza, Penda Kushiriki,” Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana,, Julai 2024.

Penda Kujifunza, Penda Kushiriki

Kwa Liam N. kutoka Denmark, injili ni sehemu ya maisha ya kufurahisha na kuridhisha.

Picha
mvulana akipiga gitaa

Picha na Ashlee Larsen

Kuwahudumia wengine kunaweza kuonekana kama ni vitu vingi tofauti. Njia moja ambayo Liam anapenda kutumikia ni kuwapigia wengine muziki.

Shule au burudani? Kazi au burudani? Labda kuna swali bora zaidi: Kwa nini uridhike na kimoja tu? Anapoweza, Liam N. mwenye umri wa miaka 14 kutoka Denmark hujaribu kupata uwiano.

“Ninapenda kupiga muziki,” anasema. “Mimi ninapiga gitaa, ngoma, besi, kinanda na ukulele. Nadhani kupiga muziki ni njia nzuri ya kuelezea hisia zangu. Pia napenda kuwapigia wengine ili kuwafurahisha.”

Wakati haburudiki na muziki, unaweza kumkuta Liam akicheza soka, mpira wa vikapu au chesi na marafiki zake. “Pia napenda sayansi na unajimu,” anasema. “Inapendeza kuona jinsi kila kitu kinavyounganishwa. Mungu ameviumba vyote, na ni vya ajabu.”

Picha
mvulana anayecheza mpira wa kikapu
Picha
wavulana wakicheza chesi

Mbali na mambo yake ya kufurahisha, Liam hupata wakati wa kufanya kazi kwa bidii, iwe ni kufikisha magazeti karibu na mtaa wake au kujisomea kwa ajili ya shule.

Picha
wanandugu wakiendesha baiskeli

Liam anajifunza kuwekea uwiano mambo anayohitaji na anayotaka kufanya. Anaweza kuwa na shughuli nyingi, lakini kuna jambo moja analitengea muda kwa ajili yake kila siku—injili ya Yesu Kristo.

Picha
familia

Liam anaishi kwenye peninsula kuu ya Denmark na wazazi wake na ndugu zake wawili, Filippa na Max.

Bao la Dakika Tano

“Hivi majuzi niliamua kwamba ningesoma angalau sura moja ya Kitabu cha Mormoni—sura moja tu—kila siku moja,” Liam anasema. “Inanichukua labda dakika tano. Lakini inanipa nguvu zaidi, kwa hivyo niko tayari kuchukua changamoto hiyo.

Kusoma maandiko kila siku kumemsaidia Liam zaidi ya vile alivyofikiri ingemsaidia. “Nyakati zingine ninapokuwa na siku mbaya, kusoma jambo la kufariji kunaweza kunifanya nirudi kwenye hali nzuri tena. Lakini ikiwa imekuwa siku nzuri, inaweza pia kunikumbusha kushukuru kwamba mambo yanakwenda vizuri. Ninafurahi kwamba nimeweza kushikamana na lengo langu.”

Picha
mvulana akisoma maandiko

Liam ana shughuli nyingi anazopendelea kufanya na majukumu mengi. Lakini kutenga muda kila siku kusoma Kitabu cha Mormoni kumebariki maisha yake.

“Nani Hataki Shangwe?”

Liam anashukuru kwa usaidizi anapojaribu kutenga muda kwa ajili ya injili. “Ndugu zangu na mimi ndio waumini pekee wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho katika shule yetu, hivyo marafiki zangu wengi wa karibu sio wauminii. Lakini nadhani kuna jumuiya nzuri sana katika Kanisa la Denmark. Kila mtu anamjua mwenzake angalau kidogo, na inapendeza tunapokutana sote.”

Kuwa na marafiki wenye viwango tofauti kunaweza kuwa vigumu nyakati fulani. “Denmark ni nchi ambayo vijana wengi hunywa pombe tangu wakiwa wadogo,” Liam anaeleza. “Inaweza kuwa vigumu kwa kijana kukataa mambo kama hayo.” Lakini Liam anajaribu kuwa wazi kuhusu kile anachokiamini ili wengine waweze kuelewa vyema chaguzi zake.

Picha
mvulana akicheza gitaa la besi

Kuwahudumia wengine kunaweza kuonekana kama mchanganyiko wa vitu vingi tofauti. Njia moja ambayo Liam anapenda kutumikia ni kuwapigia wengine muziki.

“Wakati fulani shuleni tunapokuwa na masomo kuhusu Ukristo, walimu au marafiki wameniuliza kuhusu imani yangu. Nimejaribu kueleza vizuri kadiri niwezavyo,” Liam anasema. “Pia nilimwalika mmoja wa marafiki zangu wa karibu kwenye ubatizo wangu. Nilimpa yeye na mama yake Kitabu cha Mormoni na kuzungumza nao kuhusu baadhi ya mambo ninayoyaamini. Ni juu yao kuamua wanachofanya na hicho kitabu. Nilihisi kwamba nilifanya jambo sahihi kuwaalika wengine wahisi shangwe ile ile ninayoihisi, kwa sababu ni nani asiyetaka shangwe?”

Picha
ndugu

Liam na kaka zake ndio waumini pekee wa Kanisa shuleni kwao. Wana nafasi nyingi za kuwa vielelezo vyema vya wanafunzi wa Kristo.

Kuanza na Urafiki

Liam anajua kwamba kueleza kile anachokiamini au kumpa rafiki Kitabu cha Mormoni sio njia pekee ya kuwa mwanafunzi wa Yesu Kristo. Wakati mwingine kuwaalika wengine kuhisi shangwe ya injili huanza tu na urafiki wa kweli na upendo.

“Ninapenda sana hadithi ya Amoni katika Kitabu cha Mormoni,” Liam anasema. “Nadhani inavutia kwamba haendi moja kwa moja kwa Mfalme Lamoni na kusema, ‘Utasikiliza kile ninachoamini,’ badala yake yeye anakuwa rafiki yake kimya kimya hadi mfalme anapomuuliza Amoni, ‘Unawezaje kuwa mtu mzuri hivi?’”

“Tunaweza kujenga uhusiano na wengine pia,” Liam anasema. “Labda watakuja kwetu na kuuliza ni nini kinachotupa nguvu zetu za ziada.”

Picha
ndugu

Baraka kwa ajili ya Maisha

Liam kwa kweli anahisi kama kuishi injili kumempa nguvu zaidi. Kumebariki maisha yake hata zaidi ya chess, muziki, michezo au mambo mengine yoyote mazuri anayotumia muda wake kuyafanya.

“Ninashukuru kuwa na injili katika maisha yangu kwa sababu sifikirii kama ningekuwa mtu yule yule bila hiyo,” anasema. “Ninahisi kwamba Bwana ananijua vyema zaidi kuliko ninavyojijua mwenyewe. Ninajua kwamba Mungu na Kristo wako hai. Wanatuonyesha njia tunayopaswa kwenda na kutusaidia tuwe bora zaidi.”

Chapisha