2023
Tunaweza Kutubu
Machi 2023


“Tunaweza Kutubu,” Kwa Ajili ya Nguvu Kwa Vijana, Machi 2023.

Nayaweza Mambo Yote katika Kristo

Vijana wanashiriki jinsi Kristo alivyowaimarisha wao kufanya vitu vigumu (ona Wafilipi 4:13).

Tunaweza Kutubu

Picha
mvulana

Ingawa nilibatizwa nikiwa na umri wa miaka minane, sikuwa daima nikifanya mambo yaliyo sahihi. Nilipokuwa kijana, nilianza kujiunga na kikundi cha vijana na kuanza kujiingiza katika mambo ambayo nilijua hayakuwa mazuri.

Baada ya dada yangu kuolewa, alinisaidia kurudi Kanisani. Nimejifunza kuhusu umuhimu wa Neno la Hekima na kuutendea vizuri mwili wangu.

Lakini siku moja, nilitenda dhambi nyingine kubwa. Nilihisi kuwa nisingeweza kuwa na Roho au nguvu ya ukuhani. Nilihisi nisiye na thamani na sikufikiria kama ningeweza kutimiza majukumu yangu kanisani, kama vile kubariki na kupitisha sakramenti.

Lakini injili imenifundisha kwamba ninaweza kutubu kila siku. Ilikuwa vigumu kwenda kumwona askofu wangu na kuungama dhambi yangu. Ilikuwa vigumu kujua kwamba watu wangeweza kuniona nikiingia katika ofisi ya askofu. Lakini mimi nilitaka amani ya Bwana na nilitaka kutubu.

Askofu wangu alisema sala pamoja nami na kuniambia kwamba Bwana daima ni mwenye rehema kwa wale ambao wanatafuta kutubu na kwamba ningeweza kupona kutokana na makosa yangu. Sasa nimeanza kusoma maandiko na kusali na najua inanisaidia kukinza majaribu.

Kama mchakato wa toba ni mgumu kwako, unapaswa daima kukumbuka zawadi ya Yesu Kristo na Upatanisho Wake wa kimuujiza. Sisi sote tunatenda dhambi na kufanya makosa na hatuwezi kupata ukamilifu katika maisha haya. Lakini kupitia Upatanisho wa Yesu Kristo, na kwa damu ambayo Yeye alimwaga kwa ajili yetu, siku zote tunaweza kutubu. Kwa msaada wa Bwana, tunaweza kusonga mbele kuelekea ukamilifu.

Kenneth B., Tonga

Chapisha