2023
Ninawezaje kuwasaidia vyema marafiki zangu ambao hawashiriki kikamilifu Kanisani kuimarisha shuhuda zao?
Machi 2023


“Ninawezaje kuwasaidia vyema marafiki zangu ambao hawashiriki kikamilifu Kanisani kuimarisha shuhuda zao?,” Kwa Ajili ya Nguvu Kwa Vijana, Machi 2023.

Maswali na Majibu

“Ninawezaje kuwasaidia vyema marafiki zangu ambao hawashiriki kikamilifu Kanisani kuimarisha shuhuda zao?”

Kuwa Baraka kwa Wengine

Picha
msichana

“Wakati nikijaribu kumsaidia rafiki kuimarisha ushuhuda wake binafsi, ninajaribu kuwa baraka na msaada katika maisha yake. Ninajaribu kuwa mfano na kumwonyesha kwamba injili ya Yesu Kristo inaweza kuimarisha urafiki wake na mahusiano ya kifamilia kama atajitahidi kuwa mtiifu na mwenye haki. Ninapenda kumsaidia yeye ili ajisikie kuwa anapendwa.

Selina O., 19, Bolivia

Siku zote Alika

“Unaweza kuwafundisha marafiki zako kuhusu upendo na rehema ya Yesu Kristo na jinsi Yeye anavyoweza kuwasaidia. Waalike kwenda kanisani na kuhudhuria madarasa ya vijana pamoja nawe. Hii inaweza kuwasaidia kukuza ushuhuda imara juu ya Yesu Kristo.”

Shara R., 12, Colombia

Kuwa Rafiki Yao Kwanza

Picha
msichana

“Mimi daima ninajaribu kuwajumuisha na kuhakikisha marafiki zangu wanajua kwamba ninawafikiria wao. Ninajua ninaweza kuwa nuru kwa ajili yao ninapodumisha urafiki wetu na upendo. Ninaweza kuwaalika marafiki zangu kwenye shughuli za Kanisa, lakini daima mimi ni rafiki yao wa kweli kwanza. Marafiki zako wataimarisha shuhuda zao wanapoona mfano wako wa upendo wako na urafiki wenye msaada.”

Mia D., 19, Florida, Marekani

Kristo Atakusaidia

“Inaweza kuwa vigumu kuwa na marafiki ambao hawahudhurii kikamilifu, lakini ninapenda kuwaalika marafiki zangu kwenye shughuli za vijana au kanisani wakati ninapotoa hotuba. Kama wanaonyesha kupendelea, ninawapa Kitabu cha Mormoni kikiwa na ushuhuda wangu na mistari iliyowekwa alama ambayo ina umuhimu wa kipekee kwangu. Kumbuka, Kristo atakusaidia katika hali yoyote ile.

Elizabeth B., 15, Florida, Marekani

Kuwa Mkarimu Tu

Picha
mvulana

“Nilimuuliza mwalimu wangu wa seminari swali hili. Alisema, ‘Kuwa mkarimu tu, Jordan. Tayari unafanya jambo sahihi.’ Mwanzoni, nilifikiria, ‘Kuwa mkarimu tu haitoshi.’ Lakini baadaye nilifikiria kuhusu rafiki yangu ambaye alihitaji urafiki na mfano wangu. Roho alinisaidia kuwa mkarimu na kujua kitu cha kusema. Sasa, anataka siku moja aje kubatizwa!”

Jordan S.,17, Utah, Marekani

Chapisha