Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana
Nani mwingine aliona bamba za dhahabu tofauti na Joseph Smith?
Januari 2024


“Nani mwingine aliona bamba za dhahabu tofauti na Joseph Smith?,” Kwa Ajili ya Nguvu Kwa Vijana, Jan. 2024.

Kwenye Hoja

Nani mwingine aliona bamba za dhahabu tofauti na Joseph Smith?

Picha
Mary Whitmer anaona mabamba ya dhahabu

Vielelezo na Steve Nethercott

Zaidi ya Joseph Smith, watu hawa 12 waliona mabamba ya dhahabu:

Mashahidi Watatu: Oliver Cowdery, David Whitmer and Martin Harris. Malaika Moroni aliwaonyesha bamba, aliwashuhudia, na kuwaamuru wanaume watatu kutoa ushuhuda wake.1

Mashahidi nane: Christian Whitmer, Jacob Whitmer, Peter Whitmer Jr., John Whitmer, Hiram Page, Joseph Smith Sr., Hyrum Smith, and Samuel H. Smith. Joseph Smith aliwaonyesha mabamba na kuwaruhusu kuyashika.2

Mary Whitmer: Malaika Moroni alimuonyesha bamba na kumfariji kwa sababu ya mizigo aliyopaswa kubeba katika kutunza watoto nane na wageni watatu nyumbani wakati Kitabu cha Mormoni kikitafsiriwa nyumbani kwake.3

Josiah Stowell aliona pembe ya bamba. Na angalau wengine wanne walinyanyua bamba za dhahabu wakati bamba zilipokuwa katika kasha au zimefunikwa: Lucy Mack Smith, Emma Smith, William Smith na Katharine Smith.4

Hakuna kati ya hawa watu 17 aliyewahi kukana walichokiona na kukipitia.

Chapisha