2023
Kuhudumu kwa Subira
Septemba 2023


“Kuhudumu kwa Subira,” Liahona, Sept. 2023.

Kanuni za Kuhudumu

Kuhudumu kwa Subira

Tunaweza kukuza uwezo wa kuwa na subira zaidi, katika maisha na katika kuwatumikia wengine.

Picha
wanawake watatu wakitembea pamoja

Katika 2 Wakorintho 12:7–8, Paulo anasimulia juu ya kusali mara tatu ili “mwiba katika mwili” uondolewe. Lakini sala zake hazikujibiwa kwa changamoto kuondolewa. Badala yake, Bwana alimwambia, “Neema yangu yakutosha.” Paulo alionyesha subira na imani katika jinsi alivyojibu: “Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu” (mstari wa 9).

Bwana pia alimfunza Moroni kwamba kupitia neema ya Yesu Kristo, tunaweza kujifunza na kukua katika uwezo: “Na ikiwa watu watakuja kwangu nitawaonyesha udhaifu wao. Ninawapatia watu udhaifu ili katika udhaifu wao wawe wanyenyekevu; na neema yangu inatosha watu wote ambao hujinyenyekeza mbele yangu; kwani wakijinyenyekeza mbele yangu, na kuwa na imani ndani yangu, ndipo nitafanya vitu dhaifu kuwa vyenye nguvu kwao” (Etheri 12:27).

Kuhudumu kwa Subira

Kana Paulo, wengi wetu wamesali kwa ajili ya ahueni kwa mambo mengi katika maisha yetu—wakati mwingine mara nyingi zaidi ya mara tatu. Wakati mwingine ni wakati muafaka kwa ajili ya baraka kutolewa, na wakati mwingine sisi, kama Paulo, tunafunzwa na kuimarishwa. Kwenye nyakati hizi, tunajifunza subira na kujifunza kusubiria wakati wa Bwana.

Tunahitaji sifa kama ya Kristo ya subira pale tunapohudumia pia. Tunaweza kuwahudumia watu ambao wana changamoto za aina nyingi na viwango vya uelewa wa injili, na inahitaji subira na upendo ili kuwahudumia watu ambao yaweza kuwa hawataipokea.

Picha
mwanamke kichwa kilichoinuliwa

Picha kupitia Getty Images

Kukuza Subira

Tunapokuja kumjua Mwokozi, tutajua vizuri zaidi nini Yeye angefanya ili kuhudumu katika nafasi zetu. Ni kwa jinsi gani tunaweza kukuza sifa kama ya Kristo ya subira?

  • Tambua kwamba maisha ya kufa yamejaa hali ambazo zitajaribu subira yetu na ni kawaida kuhisi kukata tamaa nyakati zingine. Kumbuka kwamba kwa mazoezi na imani katika Bwana, tunaweza kuboresha mjibizo wetu kwa hali za shinikizo. Kuwa na subira na juhudi zako ili kuwa na subira zaidi!

  • Muombe Mungu msaada wakati unapohisi unataabika kuwa na subira. Kuvuta pumzi ndefu na sala kunaweza kukusaidia kuleta utulivu na amani.

  • Kusikiliza muziki wa kuinua kiroho ambao huleta hali ya amani kunaweza kukusaidia ushinde hisia za kukosa subira.

  • Kutambua wakati wa Bwana katika maisha yako. Mapenzi yetu na tamaa zetu vinapaswa kurekebishwa kufuata ratiba Yake.

  • Kuwa na subira ni mtazamo akilini. Kumbuka kwamba kuhisi wayowayo au kuwa kila mara katika hali ya haraka mara chache sana huboresha maisha yetu.

Mawazo ya Kuhudumu kwa Subira

Wakati mwingine kazi yetu ya uhudumiaji ni kuwasaidia wengine kuwa na subira wakati wa majaribu. Hapa kuna baadhi ya njia tunazoweza kusaidia:

  • Kumwonesha mtu au familia kwamba tunawapenda na kuwajali licha ya changamoto wanazokabiliana nazo, hata kama wanafikiria, kwa sababu zozote zile, kwamba hawawezi kupendeka.

  • Shiriki nao uzoefu wakati ambapo ilibidi ujifunze subira na kwamba unahusisha na jinsi inavyoweza kuwa vigumu. Wasaidie wao wahisi kwamba hawako peke yao ikiwa wanahisi kukosa subira au kukatishwa tamaa.

  • Sali kwa ajili yao ili waweze kuwa na subira wakati wa majaribu magumu na waruhusu wajue kwamba Baba wa Mbinguni atasikia sala zao ili waweze kuhisi nguvu hizo.

  • Kuwa sikio la kusikiliza wanapohitaji mtu wa kuzungumza naye. Kuwa na rafiki anayeelewa ni mojawapo ya njia bora za kuvumilia jaribu gumu au hali ngumu.

Chapisha