2023
Nyaraka za Mtume Paulo
Septemba 2023


“Nyaraka za Mtume Paulo, Sehemu ya 2,” Liahona, Sept. 2023.

Njoo, Unifuate

Nyaraka za Mtume Paulo

Sehemu ya 2

Picha
ngozi pamoja na bakuli la wino na kifaa cha kuandika

Kielelezo na Bill Young

Waefeso

  • Kwa waumini wa Kanisa katika Efeso (mji katika Uturuki ya sasa)

  • Uliandikwa kutoka Rumi karibia 60–62 BK

  • Dhumuni: Kuwafundisha waongofu, kuhamasisha umoja, na kuwatia moyo Watakatifu kuvumilia dhidi ya uovu.

  • Mafundisho muhimu: Kipindi cha ujalivu wa nyakati, wokovu kwa neema, kuanzisha na dhumuni la Kanisa, na utaratibu katika maisha ya familia

Wafilipi

  • Kwa waumini wa Filipi (mji katika Ugiriki ya sasa)

  • Uliandikwa kutoka Rumi karibia 60–62 BK

  • Dhumuni: Kuwasifia Watakatifu kwa ajili ya imani yao na dhabihu na kuwaonya Wakristo mafisadi.

  • Mafundisho muhimu: Kanuni za kuishi kwa haki, kumtegemea Kristo kwa ajili ya wokovu, na kufanya dhabihu kwa ajili ya injili

Wakolosai

  • Kwa waumini katika Kolosai (mji katika Uturuki ya sasa)

  • Uliandikwa kutoka Rumi karibia 60–62 BK

  • Dhumuni: Kuwaonya wenye kiburi na kutilia mkazo kwamba ukombozi huja kupitia Kristo

  • Mafundisho muhimu: Asili ya Kristo, kujenga msingi juu Yake na kukuza sifa kama za Kristo.

1 Wathesalonike

  • Kwa waumini katika Thesalonike (mji katika Ugiriki ya sasa)

  • Uliandikwa kutoka Korintho (mji katika Ugiriki ya sasa)

  • Dhumuni: Kutoa himizo na kujibu maswali kuhusu Ujio wa Pili

  • Mafundisho muhimu: Kupendana, Ufufuko, na Ujio wa Pili

2 Wathesalonike

  • Kwa waumini katika Thesalonike (mji katika Ugiriki ya sasa)

  • Uliandikwa kutoka Korintho (mji katika Ugiriki ya sasa)

  • Dhumuni: Kuimarisha imani na kufafanua kutoeleweka kwa Ujio wa Pili

  • Mafundisho muhimu: Hatima ya waovu, Ukengeufu Mkuu na umuhimu wa kufanya kazi kukidhi mahitaji ya kimwili

Chapisha