Kadi za Historia ya Kanisa
Kata na ziondoe kadi, zikunje kwa kufuata mistari ya nukta, na zifunge kwa kuzigundisha kwa tepu.
Sagwitch Timbimboo
1822–1887
“Ninataka kuwa na amani na watu wote.”
-
Alikuwa mtemi wa Shoshone katika kile ambapo sasa ni Utah kaskazini, Marekani.
-
Yeye na wengi wa watu wake walibatizwa mwaka wa 1873.
-
Yeye na mke wake walikuwa baadhi ya Wahindi wa Kiamerika wa kwanza kuunganishwa hekaluni.
-
Yeye na watu wake walisaidia kujenga Hekalu la Logan Utah. Baadaye walifanya kazi ya hekaluni kwa ajili ya watu wao waliofariki.
Anna Gaarden Widtsoe
1849–1919
Naichukulia kuwa jambo la heshima kubwa … kusaidia katika [uenezaji] wa injili.”
-
Aliishi Norway. Alikuwa mjane, na aliwalea wana wawili.
-
Alijifunza injili kutoka kwa fundi viatu. Alipokuwa anashona viatu vyake, aliweka kipeperushi cha Kanisa katika kila kiatu. Alibatizwa baharini.
-
Alihudumu misheni huko Skandinavia. Mwanae John alikuja kuwa Mtume.
Vielelezo na Brooke Smart