Kusaidia Kama Yesu
Yesu Aliwasaidia Watu wenye Uhitaji
Picha
Jesus helping up a sick man
Alipokuwa duniani, Yesu aliwaponya watu walio kuwa wagonjwa. Aliwalisha wale waliokuwa na njaa. Aliwafariji watu waliojisikia kuwa wapweke.
Yesu pia aliwafundisha wanafunzi Wake kuwasaidia wengine. Alisema wanapaswa kuwapa chakula, maji, na mavazi wale waliohitaji. Aliwaambia wawatembelee watu waliokuwa wapweke. Yesu alisema kwamba wakati wakiwatumikia wengine, ni kama wanamtumikia Yeye.
Picha
boy carrying firewood
Familia yangu inamtumikia Dada Rosa. Dada Rosa ana umri wa miaka 90, hivyo hawezi kutoka nje ya nyumba yake. Ninamsaidia Baba kupakia na kusafirisha kuni kwa ajili ya Rosa.
Ignacio G., umri miaka 9, Canelones Department, Uruguai.
Picha
Page from the January/February 2022 Friend Magazine.
Vielelezo na Sarah Keele