2022
Harriet Anakutana na Wamisionari
Mei/Juni 2022


Waasisi katika Kila Nchi

Harriet Anakutana na Wamisionari

Je, anaweza kuwa na Baba tena?

Picha
girl talking to missionaries

Harriet aliitazama picha ya Baba iliyokuwa ukutani. Ilikuwa imepita miezi minane tangu alipofariki. Alijiuliza ikiwa angemwona tena. Alimkumbuka sana.

Hodi, hodi, hodi.

Harriet alifungua mlango wa nyumba yao ndogo. Vijana wawili walisimama nje.

Siku Njema! Habari! Sisi ni wamisionari kutoka Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho. Tungependa kuzungumza na familia yako kuhusu Yesu Kristo.”

Harriet alitabasamu. Jambo fulani kuhusu mambo waliyosema lilimfanya ajihisi vizuri. “Nitamuuliza Mutti (Mama).”

Harriet alimwendea Mutti. “Wamisionari wako mlangoni,” alisema. “Wanataka kuzungumza nasi kuhusu Yesu.”

Mutti akakunja uso. “Waambie hatuna muda.”

“Lakini wanaonekana kuwa wema sana,” Harriet alisema. “Haitachukua muda mrefu.”

Mutti alitazama saa. “Sawa. Kwa dakika chache.”

Wamisionari waliingia na kuzungumza na Mutti, Harriet, na dada yake Harriet, Carmen. Waliwaambia kuhusu Yesu na kitabu kiitwacho das Buch Mormon, Kitabu cha Mormoni. Kisha wakawapa familia ya Harriet nakala wasome.

“Nadhani tunaweza kusoma kurasa chache,” Mutti alisema, huku akifungua kitabu. Katika siku chache zilizofuata, Mutti aliendelea kusoma na kusoma. Alisoma sehemu kwa sauti kwa Harriet na Carmen.

Natamani Papa angeweza kusoma hii. Angekipenda, Harriet aliwaza.

Wakati wamisionari waliporudi, walifundisha kuhusu mpango wa Mungu. “Tuliishi na Mungu kabla hatujazaliwa. Tulikuja duniani kujifunza na kuwa kama Yeye. Tunapokufa, tunaweza kuwa Naye tena.”

Vipi kuhusu Baba? Harriet aliuliza.

Mmisionari alimtazama Harriet. “Kwa sababu Yesu alikufa na kuishi tena, tunaweza kuwa na familia zetu milele. Hata na wapendwa waliokufa.”

Harriet alihisi mtiririko wa tumaini. Anaweza kuwa na Baba tena! Mutti alikuwa na tabasamu kubwa pia—la kwanza baada ya muda mrefu.

Harriet, Mutti, na Carmen waliendelea kujifunza kutoka kwa wamisionari. Walienda kanisani. Harriet akawa rafiki na mvulana mzuri aitwaye Dieter.

Sasa nyumba ya Harriet ilihisi kama kuna mwanga wa jua katika kila chumba. Punde si punde, Harriet na familia yake waliamua kubatizwa.

Usiku kabla ya ubatizo wao, Harriet alipiga magoti pamoja na Mutti na Carmen kusali. “Baba wa Mbinguni,” Harriet alisema, “tunashukuru sana kwa wamisionari, injili, na familia yetu. Hatuwezi kusubiri kubatizwa.”

Harriet alipofumbua macho yake, aliitazama picha ya Baba na kutabasamu. Hakuweza kusubiri kumuona tena siku moja.

Kuna mahekalu mawili nchini Ujerumani.

Theluthi moja ya Ujerumani imefunikwa na misitu.

Ujerumani inashiriki mpaka wake pamoja na nchi tisa.

Harriet alipokua, aliolewa na mvulana mzuri aitwaye Dieter.

Dieter sasa ni mmoja wa Mitume—Mzee Dieter F. Uchtdorf!

Mzee Uchtdorf anasema Harriet ni “mwanga wa jua wa maisha [yake].”

Picha
PDF of story

Vielelezo na Giovanni Abeille

Chapisha