2021
Je, ninawezaje kuacha kutilia shaka ustahiki wangu binafsi?
Julai 2021


“Je, ninawezaje kuacha kutilia shaka ustahiki wangu binafsi?” Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana, Julai 2021, 30–31.

Maswali na Majibu

“Je, ninawezaje kuacha kutilia shaka ustahiki wangu binafsi?”

Kupitia Macho ya Baba wa Mbinguni

Picha
msichana

“Kila siku, ninasali kwa Baba wa Mbinguni na kumwomba anisaidie nijione kama Yeye anavyoniona. Kisha nasikiliza kwa makini sana Roho anaponipa jumbe chanya kutoka kwa Mungu kuhusu ustahiki na utambulisho wangu, na ninajiambia mimi mwenyewe maneno haya kwenye kioo. Shughuli hii rahisi ni njia tunayoweza kujiunganisha na mbingu na kujua kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wanatupenda na wanatuamini.”

Madeleine M., 14, New York, Marekani

Tupende Tofauti Zetu

Picha
msichana

“Daima ninafanya kadiri niwezavyo kukumbuka kwamba mimi ni mtoto mpendwa wa Mungu. Najaribu kutojilinganisha na wengine, kwa sababu hilo linaleta ugumu zaidi kusadiki katika ustahili wangu binafsi. Mungu ametufanya sote kuwa wa kipekee na wazuri katika njia yetu wenyewe, na tofauti hizo ni kitu kizuri.”

Brooke D., 14, Alberta, Kanada

Baraka Iliyofichika

Picha
mvulana

“Mara nyingi sisi tunafikiri kwamba kuwa dhaifu au kuwa na upungufu kunatufanya tusiwe na thamani. Ukweli ni kwamba, tumebarikiwa ili tuweza kuinuka kuyapita hayo na kuwa toleo bora zaidi la sisi wenyewe kupitia unyenyekevu na maboresho binafsi. Kama tutafanyia kazi mambo yaliyo magumu kwetu, Bwana ataziona na kuzipa thawabu jitihada zetu. Ni kuhusu kujaribu tu na pasipo kukata tamaa kamwe.”

Ricardo R., 17, Chihuahua, Mexico

Utambulisho Wetu wa Kiungu

Picha
mvulana

“Hakuna kinacholingana na kutambua kwamba kama watoto wa Mungu aliye hai, tunaweza kuwa kama Yeye alivyo. Inabadilisha kila kitu! Tunapopata mawazo mabaya ambayo yanatufanya tutilie shaka ustahili wetu, kumbuka kwamba mawazo hayo yanatoka kwa Shetani, siyo kwa Mungu. Tunao uwezekano usio na mwisho na asili ya kiungu, kama tu Baba yetu wa Mbinguni. Anatuamini na anampenda kila mmoja wetu kibinafsi.”

Alexandre S., 16, Minas Gerais, Brazil

Wajibu Mkuu

Picha
msichana

“Ninapojitahidi kujifunza na kutafakari maandiko na maneno ya manabii wanaoishi, ninaweza kuhisi Roho Mtakatifu yuko pamoja nami, kitu ambacho kinanikumbusha kwamba mimi ni binti mpendwa wa wazazi wa mbinguni na kwamba Mungu ana mipango mikuu kwa ajili yangu mimi. Rais Nelson daima anatuonyesha majukumu makuu tuliyonayo katika siku hizi za mwisho na kwamba Mungu anatuamini sisi na anajua kile tunachoweza kufanya.”

Mirian P., 16, Paraná, Brazil

Fanya Kitu Unachokipenda

“Tunapoanza kutilia shaka ustahili wetu binafsi, daima tunaweza kuomba msaada kutoka kwa watu wengine. Lakini kwanza, tunaweza kuanza kufanyia kazi mawazo yetu wenyewe. Tunaweza kufanya mazoezi, kuchangamana na marafiki na familia katika njia nzuri, au kufanya shughuli ambayo tunaifurahia. Hii inatusaidia kutambua kwamba sisi ni watoto wa Mungu, ambaye ametupatia thamani na kipaji.”

Carlos V., Mexico

Jitambue

“Nimegundua kwamba ni rahisi zaidi kujipenda mimi mwenyewe kwa sababu nilitenga muda wa kutafuta kujua mimi ni nani. Babu yangu wakati mmoja aliniambia, “Unatakiwa kuishi na nafsi yako milele, hivyo wewe unaweza ukawa mtu fulani unayetaka kuishi naye.” Nilifuata ushauri huo na kujaribu kuwa toleo bora la mimi mwenyewe. Sasa najisikia kujiamini zaidi kwa sababu ninajua kile ninachotaka, kile ninachofanya vizuri, na kile ninachosimamia. Ninajisikia furaha ninapojaribu kuwa mtu yule Baba wa Mbinguni ananitaka niwe.”

Sarah Nielson, Utah, Marekani

Kumbuka Wewe Ni Nani

“Ninafikiria juu ya wimbo wa Msingi “Mimi ni Mwana wa Mungu.” Unanikumbusha kuwa nimepewa vipawa na vipaji ili kuuandaa ulimwengu kwa ajili ya Ujio wa Pili wa Bwana. Sehemu ya kila mmoja wetu ni ya kipekee na muhimu, na sisi sote ni miujiza katika maisha ya kila mtu mwingine. Wewe ni muujiza katika maisha ya kila mmoja anayekuzunguka. Ikiwa utasahau hilo, fikiria kuhusu mambo yote ambayo Yesu aliyafanya Duniani na jaribu kufuata mfano Wake. Wakati wowote unapojisikia huzuni au usiye na thamani, mtafute mtu anayejisikia vivyo hivyo, nawe utajisikia umeinuliwa.”

Brigham M., Mexico

Idhini ya Kiungu

“Ninapomsikiliza Mungu, Yeye ananisaidia kuacha kutilia shaka ustahili wangu binafsi. Watu wengi hawawezi kuelewa kikamilifu thamani yangu, lakini Mungu anaelewa na ninamwamini Yeye. Kama nitaacha watu wanaonizunguka waamue thamani yangu, yote nitakayofanya ni kukaa juu ya maneno yao na kujifikiria vibaya kuhusu mimi mwenyewe. Lakini kama nitachilia maneno yao hasi, sihitaji tena kutilia shaka ustahili wangu binafsi. Nimejifunza kwamba sihitaji idhini yao tena. Kila mmoja wetu anao ustahili wa kurithi kama watoto wa Baba wa Mbinguni. Tunahitaji kujikumbusha wenyewe juu ya hilo, hasa kama hakuna mtu mwingine anayefanya hivyo.”

Anna G., 23, Ufaransa

Kujiamini katika Injili

“Kwenye mitandao ya kijamii, ninaona watu wa aina zote wanaoonekana wakamilifu, au angalau bora kuliko mimi. Kuishi injili kunanisaidia mimi kukuza mtazamo wa shukrani kuhusu mimi ni nani. Ninapoishi kanuni za Injili kama vile imani, toba, na kuyatafakari maandiko, ninajisikia wa kipekee. Sihisi haja ya kujilinganisha mimi mwenyewe na wengine, na hatimaye, ninajiamini zaidi.

Alexandra R., Mexico

Jisamehe Mwenyewe

“Sisi daima hatufikiri kuwa tunastahili msamaha, kwa sababu tunajua makosa tuliyofanya. Lakini sisi ni wanadamu—tunafanya makosa na tutaendelea kuyafanya. Tunahitaji kuwa wenye kujisamehe, kwa sababu kila mmoja anastahili nafasi nyingine. Tunahitaji kujiona kupitia macho ya watu ambao wanatupenda. Tutamwona mtu wa kipekee na wa kushangaza sana ambaye anastahili upendo usio na masharti bila kujali lolote.

Valerie J., Mexico

Chapisha