2022
Naijua Thamani Yangu
Januari 2022


“Naijua Thamani Yangu,” Kwa Ajili ya Nguvu Kwa Vijana, Jan. 2022.

Dhima na Mimi

Vijana wakielezea jinsi wanavyoishi maneno ya Dhima ya Wasichana na ya Akidi ya Ukuhani wa Haruni

Naijua Thamani Yangu

“Mimi ni binti mpendwa wa wazazi wa mbinguni.”

Picha
msichana

Picha na Christina Smith

Katika sehemu nyingi za Jamaika, wanafunzi kama mimi wanapaswa kufanya mtihani ili kuingia katika shule ya sekondari wanayoitaka. Mimi na rafiki zangu tulisoma kwa bidii ili sote tuweze kuingia katika shule bora ya sekondari. Wakati nilipoanza kutia shaka kama ningeweza, mama yangu daima alinitia moyo. Alinikumbusha kwamba mimi ni mmoja wa watoto wa Baba wa Mbinguni na kwamba Atanisaidia kutembea katika njia sahihi.

Matokeo yangu ya mitihani yalipotoka, nilipata daraja la juu zaidi nililoweza kupata! Nilifurahia sana kwa sababu hiyo ilimaanisha ningeweza kuwa na marafiki zangu wote!

Lakini punde nilikuja kujua kwamba mmoja wa marafiki zangu hakuweza kupata alama za juu za kutosha. Sote tulihuzunika kuwa hakuweza kuja na sisi. Lakini nilipata shangwe katika kukumbuka kile mama yangu alichonifundisha. Rafiki yangu pia alikuwa binti mzuri wa Baba wa Mbinguni, na kwamba Mungu atamsaidia na yeye pia, bila kujali alama zake za mtihani.

Furaha yangu ilififia pale rafiki yangu alipoanza kumwambia kila mtu kwamba mimi sikustahili kuingia katika shule ile ya sekondari—kwamba yeye ndiye alipaswa kuingia badala yangu. Wengi wa marafiki zangu wakawa upande wake na wakaacha kucheza na mimi. Nilianza kujitilia shaka mimi mwenyewe. Je, mimi nilistahili kuingia?

Nilifikiria kile mama yangu alilonifundisha, kwamba mimi ni mtoto wa kipekee katika sura ya Baba wa Mbinguni.

Sasa mimi niko kwenye shule mpya, na nimepata marafiki wapya. Wananisaidia na kunikumbusha juu ya thamani yangu. Nimejifunza kwamba haijalishi kile wengine wasemacho kuhusu mimi. Nina furaha ninapojaribu kuwa yule ambaye Mungu anataka mimi niwe—kwa sababu huyo ndiye mimi ninataka niwe.

Mwandishi anaishi huko Jamaika.

Chapisha