Liahona
Matamanio Halisi ya Nafsi
Mei 2024


Kikao cha Jumamosi Asubuhi

Matamanio Halisi ya Nafsi

Dondoo

Picha
bango

Pakua PDF

Akina kaka na akina dada, ninashuhudia kwamba Mungu husikia kila sala tunayotoa na anajibu kila moja kulingana na njia ambayo Yeye ameibainisha kwa ajili ya ukamilifu wetu. …  Ni kwa sababu zijulikanazo kwa Mungu pekee kwa nini sala hujibiwa kinyume na tunavyotumaini—lakini ninawaahidi zinasikika na zinajibiwa kulingana na upendo Wake usioshindwa na ratiba Yake ya ulimwengu.

Ikiwa “tutasali bila kizuizi,”[2Nefi 4:35] hakuna ukomo kwenye lini, wapi au kuhusu nini tunapaswa kusali juu yake. … 

… Tunapaswa kusali binafsi, katika familia zetu, na katika mikusanyiko ya ukubwa wowote. Tunapaswa kutumia sala kama ngao dhidi ya majaribu, na ikiwa kuna wakati hatuhisi kusali, tunaweza kuwa na uhakika kwamba kusita hakuji kutoka kwa Mungu, ambaye anatamani kuwasiliana na watoto Wake wakati wowote na muda wote. …  Wakati tunapokuwa hatujui jinsi ya kusali au tusali kwa ajili ya kitu gani hasa, tunapaswa kuanza, na kuendelea, hadi Roho Mtakatifu anapotuongoza kwenye sala tunayopaswa kuitoa. … 

Hatimaye, tunaweza kutazama mfano wa Mwokozi, ambaye alisali mara nyingi, nyingi sana. … 

Katika muktadha huo wa ushindi wa Kristo juu ya mauti na zawadi Yake ya hivi karibuni kwangu mimi ya wiki zaidi au miezi zaidi katika maisha haya ya duniani, ninatoa ushahidi wa dhati wa uhalisia wa uzima wa milele na hitaji kwetu la kutokuwa na mzaha katika kuyawekea mpango.

Chapisha