Liahona
Ujasiri wa Agano kupitia Yesu Kristo
Mei 2024


Kikao cha Jumamosi Asubuhi

Ujasiri wa Agano kupitia Yesu Kristo

Dondoo

Picha
bango

Pakua PDF

Wapendwa akina kaka na akina dada, wale wanaopata ujasiri kwa dhati katika maagano yaliyofanywa katika nyumba ya Bwana kupitia Yesu Kristo wana miliki nguvu nyingi ambazo sisi tunaweza kuzifikia katika maisha haya. …

Ni kwa jinsi gani tunapata ujasiri kama huo kupitia Yesu Kristo? Huja kupitia unyenyekevu, kuweka kiini cha maisha yetu kwa Mwokozi, kuishi kwa kanuni za injili ya Yesu Kristo, kupokea ibada za wokovu na kuinuliwa, na kuheshimu maagano tunayofanya na Mungu katika nyumba Yake takatifu. …

… Ninajua kwamba wakati Bwana anapoona hata cheche ya tamanio au chembe ya juhudi za haki katika utayari wetu wa kumweka Yeye kuwa kiini cha maisha yetu na kwenye ibada na maagano tunayofanya katika nyumba Yake, Yeye atatubariki, katika njia Yake kamilifu, kwa miujiza na huruma nyororo tunazohitaji.

Nyumba ya Bwana ni mahali ambapo tunaweza kubadilishwa kwa njia za juu na takatifu zaidi. … Ninawahakikishieni kwamba kuwa na Roho wa nyumba ya Bwana ndani yetu kunatubadilisha, kabisa. …

Ujenzi unaoendelea na wenye kasi wa mahekalu utaendelea kusisimua, kutia msukumo, na kutubariki. Hata hivyo muhimu zaidi, tunapobadilisha maandalizi yetu ya kuingia hekaluni, tutabadilisha uzoefu wetu hekaluni, ambao utabadilisha maisha yetu nje ya hekalu. Na badiliko hili litujaze ujasiri katika maagano yetu matakatifu yaliyofanywa na Mungu kupitia Yesu Kristo.

Chapisha