Liahona
Maneno ni Muhimu
Mei 2024


Kikao cha Jumapili Asubuhi

Maneno ni Muhimu

Dondoo

Picha
bango

Pakua PDF

Maneno ni muhimu!

Kwa bahati mbaya, maneno yanaweza kuwa ya kipumbavu, makali na yenye kuumiza. …

Kwa upande mwingine, maneno yanaweza kusherehekea ushindi, kuwa ya matumaini na kutia moyo. Yanaweza kutuchochea kufikiria tena, kuanza upya, na kugeuza tena mwelekeo wetu. Maneno yanaweza kufungua akili zetu kwenye ukweli.

Hiyo ndiyo kwa nini, kwanza kabisa, maneno ya Bwana ni ya muhimu. …

Kuamini na kutilia maanani neno la Mungu kutatuleta karibu zaidi na Yeye. …

Pili, maneno ya manabii ni muhimu.

Manabii wanashuhudia juu ya uungu wa Yesu Kristo. Wanafundisha injili Yake na kuonyesha upendo Wake kwa wote. …

… Maneno ya nabii ni muhimu kwa Bwana na kwetu sisi.

Tatu, na ya muhimu sana, ni maneno yetu wenyewe. …

… Kwa hiyo kuwa makini kwa kile unachosema na jinsi unavyokisema. Katika familia zetu, hususani waume, wake, na watoto, maneno yetu yanaweza kutuleta pamoja au kuleta uhasama kati yetu.

Acha nipendekeze virai vitatu rahisi ambavyo tunaweza kutumia ili kuondoa magumu na tofauti, kuinua na kuhakikishiana sisi kwa sisi:

“Asante.”

“Samahani.”

Na “ninakupenda.”

Ninaahidi kwamba kama “tutasherehekea maneno ya Kristo”[2Nefi 32:3] ambayo huongoza kwenye wokovu, maneno ya nabii wetu ambayo yanatuongoza na kutuhimiza, na maneno yetu wenyewe ambayo yanazungumza sisi ni kina nani na kile tunachokipenda sana, nguvu za mbinguni zitatiririka juu yetu.

Chapisha