Liahona
Mambo Yote kwa Faida Yetu
Mei 2024


Kikao cha Jumamosi Mchana

Mambo Yote kwa Faida Yetu

Dondoo

Picha
bango

Pakua PDF

Bado, katika ulimwengu huu wa dhiki, “tunajua kwamba mambo yote yatafanyika pamoja kwa faida yao wanaompenda Mungu.”2

Ni ahadi ya kupendeza iliyoje! Hakikisho la faraja kutoka kwa Mungu mwenyewe!

… Tukiishi kwa imani, majaribu na dhabihu ambazo kamwe hatutovichagua vinaweza kutubariki sisi na wengine katika njia ambazo hatujawahi kufikiria.

Tunaongeza imani na tumaini katika Bwana kwamba mambo yote yatafanyika pamoja kwa faida yetu pale tunapopata mtazamo wa milele; tunapoelewa majaribu yetu yanaweza kuwa “lakini kwa muda mfupi”; tukitambua mateso yanaweza kuwekwa wakfu kwa faida yetu; tukitambua ajali, kifo kisichotarajiwa, maradhi yanayodhoofisha na magonjwa ni sehemu ya maisha ya duniani; na kumtumaini Baba yetu mpendwa wa Mbinguni kwamba hatupi majaribu ili kutuadhibu au kutuhukumu.

… Mambo hufanyika pamoja kwa faida tunapotumikia kama ambavyo Yesu Kristo angefanya.

Baba aliyepangiwa pamoja na mwanawe wa umri wa mwalimu kama wahudumu wenza alielezea, “Uhudumiaji ni wakati tunapokuwa si tu majirani wenye kuleta biskuti kwa marafiki wenye kuaminika, bali waitikiaji wa kwanza wa kiroho.” Kuwa wa sehemu ya agano katika Yesu Kristo kunafariji, huunganisha, huweka wakfu. … 

Kitabu cha Mormoni ni ushahidi tunaoweza kuushikilia mkononi mwetu kwamba Yesu ndiye Kristo na Mungu anatimiza ahadi Zake. … 

Kadiri mahekalu yanavyokuja karibu na sisi katika maeneo mengi, dhabihu ya hekaluni tunayoweza kutoa ni kutafuta utakatifu katika nyumba ya Bwana mara nyingi zaidi. … 

Kwa muda na milele, dhumuni la Uumbaji na asili ya Mungu Mwenyewe ni kuvileta vitu vyote pamoja kwa faida yetu.

Hili ndilo dhumuni la milele la Bwana. Ndio mtazamo Wake wa milele. Ndio ahadi Yake ya milele. … 

… Njoo kwa Mungu Baba yetu na Yesu Kristo. Amini kwamba Wako hai, wanakupenda, na wanataka mambo yote kwa faida yako

Chapisha