Liahona
“Tulieni na Jueni Kuwa Mimi ni Mungu”
Mei 2024


Kikao cha Jumamosi Mchana

“Tulieni na Jueni Kuwa Mimi ni Mungu”

Dondoo

Picha
bango

Pakua PDF

Kila mara kwa uaminifu tunapopokea, kurejelea, kukumbuka na kufanya upya maagano matakatifu, nanga zetu za kiroho zinaimarishwa hata kuwa imara zaidi na thabiti kwenye “mwamba” wa Yesu Kristo.

… Wakati msingi wa maisha yetu unapojengwa juu ya Mwokozi, tunabarikiwa kuwa “watulivu”—kuwa na uhakika kiroho kwamba Mungu ni Baba yetu wa Mbinguni, sisi ni watoto Wake na Yesu Kristo ni Mwokozi wetu.

… Kwa mfano, Siku ya Sabato ni siku ya Mungu, wakati mtakatifu uliotengwa ili kumkumbuka na kumwabudu Baba katika jina la Mwanawe, kushiriki katika ibada za ukuhani na kupokea na kufanya upya maagano matakatifu. …

… “Nyumba za sala” ambamo ndani yake tunakusanyika siku ya Sabato ni nyumba za mikutano na sehemu nyinginezo zilizoidhinishwa—mahali pa takatifu pa utulivu, kuabudu na kujifunza. …

Hekalu ni mahali pengine patakatifu palipotengwa mahususi kwa ajili ya kumwabudu na kumtumikia Mungu na kujifunza kweli za milele. …

… Nyumba zetu zapaswa kuwa mchanganyiko wa zote mbili wakati mtakatifu na mahali patakatifu ambamo ndani yake watu binafsi na familia wanaweza “kutulia” na kujua kwamba Mungu ni Baba yetu wa Mbinguni, sisi ni watoto Wake, na Yesu Kristo ni Mwokozi wetu. …

Ninatoa ahadi kwamba wakati tunapojenga msingi wa maisha yetu kwenye “mwamba” wa Yesu Kristo, tunaweza kubarikiwa kwa Roho Mtakatifu kwa kupokea utulivu binafsi na wa kiroho wa nafsi ambao hutuwezesha kujua na kukumbuka kwamba Mungu ni Baba yetu wa Mbinguni, sisi ni watoto Wake, Yesu Kristo ni Mwokozi wetu, na tunaweza kubarikiwa kufanya na kushinda mambo magumu.

Chapisha