2021
Mgeni Mashuhuri
Septemba 2021


Mgeni Mashuhuri

Waandishi wanaishi Dar Es Salaam, Tanzania, na Utah, Marekani.

Ni kwa jinsi gani Amoni angeweza kusaidia familia yake kumkaribisha mgeni wao mashuhuri?

“Ijengeni nyumba … nyumba ya utaratibu, nyumba ya Mungu” (Mafundisho na Maagano 88:119).

Picha
a boy picking up laundry

Ilikuwa Jumamosi alasiri. Amoni alikuwa anataka kupata burudani.

“Mama,” alisema, “naomba niende nje kucheza?”

“Lazima usafishe chumba chako kwanza,” Mama alisema.

“Lakini, Mama,” Amoni alisema, “chumba changu hakiwezi kusubiri?”

“Tunataka kumwalika mtu muhimu kuwa mgeni wetu. Kwa hiyo tunataka nyumba yetu iwe safi na maridadi.”

“Mgeni Mashuhuri?” Amoni alisema. Nyumbani mwetu?

“Ndiyo, na wewe unaweza kusaidia kumwalika,” Mama alisema. “Kwa hiyo nenda na ukasafishe chuma chako.”

Amoni alisisimka. Alipenda kuwa na wageni. Alijiuliza huyu mgeni angekuwa nani. Meya? Mkuu wa shule? Labda angekuwa askofu!

Amoni alikwenda chumbani kwake. Kwanza aliona soksi zake chafu sakafuni Aliziweke kwenye kapu la nguo za kuoshwa. Kisha Amoni akapanga vitabu vyake vya shule mezani. Alitaka mgeni ajue yeye alipendelea kujifunza mambo mapya.

Dada mkubwa wa Amoni, Angel, alikuja chumbani kwake. “Unafanya nini?” aliuliza.

“Mama alisema tutakuwa na mgeni mashuhuri,” Amoni alisema. “Aliomba kumsaidia kujitayarisha.”

Wote walitazama na kumwona Mama mlangoni.

“Tunaweza kufanya nini kingine ili kujitayarisha?” Amoni alisema. “Tunataka mgeni wetu mashuhuri ajisikie kukaribishwa.”

“Je, una mawazo gani?” Mama aliuliza.

“Tunaweza kusema karibu,” Amoni alisema. Kwa Kiswahili hiyo humaanisha, “Unakaribishwa katika nyumba yetu. Unakaribishwa kuzungumza.”

“Sisi tunaweza kusikiliza,” Angel alisema. “Ni muhimu kusikiliza.”

“Hayo ni mawazo mazuri,” Mama alisema. “Acha tuone kile Baba (Dad) atasema anapofika nyumbani.”

Baada ya takribani saa moja, Baba akawasili.

Amoni alikuwa anangojea. “Mama amesema tunamwalika mgeni maalumu nyumbani mwetu. Tumekuwa tunajitayarisha.”

Baba alitabasamu. “Nashukuru. Njooni. Ketini. Tuongee. Angel, tafadhali njoo pia.”

Wote walipokuwa pamoja, Baba akasema, “Mama pamoja nami tumekuwa tukizungumza kuhusu mgeni wetu maalumu na kile tunachoweza kufanya kumfanya ajisikie kukaribishwa. Kwanza, nitawaambia mgeni wetu ni nani. Ni Roho Mtakatifu. Yeye ni mmoja wa wageni mashuhuri kati ya wote.”

Amoni na Angel waliangaliana. Hicho si kile Amoni alikuwa anatarajia!

“Na Yeye ndiye mgeni tunayeweza kumkaribisha kuwa nasi wakati wote.” Mama alisema. “Angel, baada ya wewe kubatizwa, ulithibitishwa. Na ukapatiwa kipawa. Je! Unakumbuka kile Baba alisema katika baraka hizo?”

“Yeye aliniambia nimpokee Roho Mtakatifu.”

“Hiyo ni sawa,” Mama alisema. “Ulialikwa kumpokea Roho Mtakatifu. Kwa hiyo, Amoni, niliposema wewe unaweza kusaidia kumwalika Yeye, nilimaanisha nini?”

Amoni akafikiria. Yeye alikuwa amepanga kutengeneza kadi li kumwalika mgeni wao. Lakini ni kwa jinsi gani angeweza kumwalika Roho Mtakatifu? “Mimi nadhani kwamba kwa kufanya mambo yatakayomfanya Yeye ajisikie kukaribishwa, mimi namwalika Yeye,” Amoni alisema.

“Hiyo ni sawa!” Baba alisema. “Njia mojawapo tunayoweza kumwalika Yeye katika nyumba yetu ni kuifanya iwe maridadi na safi.”

“Hiyo ndio sababu Mama alitutaka sisi tusafishe vyumba vyetu?” Amoni aliuliza.

“Ndiyo!” Mama alisema. “Tunaweza kufanya nini kingine ili kumwalika Yeye kuwa pamoja nasi?

“Tunaweza kusali,” Amosi alisema. “Na kusoma maandiko.”

“Tunaweza kusikiliza muziki mzuri,” Angel alisema. “Tunaweza kuimba nyimbo za dini pamoja.”

“Tunaweza kuwa wapole na kutopigana,” Amoni alisema.

“Hiyo ni sawa,” Baba alisema. “Tunapojaribu kufanya kile Yesu Kristo alifundisha, tunamwalika Roho Mtakatifu kuwa pamoja nasi. Na Yeye atasaidia nyumba yetu kuwa mahali tunapoweza kuhisi upendo na amani.”

Amoni alifikiria kwa dakika chache. “Unasema kweli, Baba. Roho Mtakatifu ni mmoja wa wageni mashuhuri kati ya wote!”

Picha
Friend Magazine, 2021/09-10 Sep/Oct Tier 2

Vielelezo na Mark Jarman

Chapisha