2023
“Omba, Helamán”
Januari 2023


“Omba, Helamán”

Picha
Miguel and his friends blessing their food at school.

Ilikuwa ni siku ya kwanza ya Helamán shuleni. Alivalia shati yake aliyoipenda, na alikuwa na penseli mpya. Mwalimu wake mpya alimpangia kuwa meza moja na rafiki zake Sylvester, Jorge na Miguel. Ilikuwa siku zuri.

“Wekeni vitu vyenu kando,” alisema Bi. Martínez. “Ni muda wa kula chakula cha mchana.”

Familia ya Helamán daima iliomba pamoja kabla ya mlo. Yeye alinyosha mkono wake. “Bi. Martínez, tutaomba kabla ya sisi kula?”

Bi. Martínez alimtabasamia Helamán. “Unaweza kuomba kwa ajili ya chakula chako kama unapenda.”

Helamán na marafiki zake walifungua vyakula vyao.

“Maombi ni nini?” aliuliza Sylvester.

“Ni mazungumzo na Baba wa Mbinguni,” alisema Helamán. “Ni njia ya kumshukuru Yeye kwa ajili ya chakula chetu.”

“Unaweza kuomba kwa ajili yetu sote?” alisema Miguel.

Helamán alikunja mikono. Marafiki zake watatu walikunja mikono yao. Helamán alifunga macho yake na kuinamisha kichwa chake. Marafiki zake wakafanya vivyo hivyo.

Kisha Helamán akaomba, kama vile tu familia yake ilifanya. Alimshukuru Baba wa Mbinguni kwa ajili ya siku nzuri waliyokuwa nayo na chakula chao. Aliombea baraka juu ya chakula chao. Alimalizia na katika jina Jina la Yesu Kristo, “Amina”.

Sylvester, Jorge na Miguel walitazama juu.

“Mnaweza kusema amina pia,” alisema Helamán.

Marafiki zake walitabasamu na kusema, “Amina.”

Siku iliyofuata muda wa chakula, Sylvester alisema, “Omba, Helamán.”

“Ndio, omba, Helamán,” alisema Miguel. Jorge aliitikia kwa kichwa.

Kwa hiyo Helamán aliomba tena. Wakati huu alisema alikuwa na shukrani sana kwamba mama yake kwa kumtengenezea sandwichi ya nyama na jibini, anayoipenda sana. Alimuomba Baba wa Mbinguni kuwasaidia kujifunza katika darasa siku hiyo.

Kila siku wakati wa chakula cha mchana, marafiki wa Helamán walisema, “Omba, Helamán.” Na kila siku, Helamán aliomba. Aliomba pamoja na marafiki zake kila siku ya wiki.

Jumatatu iliyofuata, Miguel alisema, “Leo nitaomba.”

Picha
Close up of two boys, Miguel and Helaman saying a prayer.

Helamán alishangaa. Alikunja mikono yake, akafunga macho yake, akainamisha kichwa na kumsikiliza Miguel akiomba.

Miguel alianza kwa kusema “Mpendwa Baba wa Mbinguni.” Alimshukuru Yeye kwa ajili ya chakula chao na aliomuomba Yeye kukibariki. Alimalizia katika jina Jina la Yesu Kristo, “Amina”.

“Amina!” alisema Helamán na Jorge.

“Amina,” alisema Sylvester. “Sikujua ungeweza kuomba.”

“Nimejifunza kwa kumsikiliza Helamán,” alisema Miguel. “Niliwaomba wazazi wangu kama ningeweza kuombea chakula chetu nyumbani. Kisha walisema ndio, kwa hiyo niliomba vile Helamán alivyofanya.”

“Lo,” alisema Sylvester. “Nafikiria nitawaomba wazazi wangu kama ninaweza kuombea chakula chetu pia.”

“Mimi pia,” alisema Jorge.

Picha
Miguel smiling as he thinks about sitting with his family at dinner. Miguel is saying a prayer for their dinner.

Helamán alitabasamu. Alishukuru aliweza kuwasaidia marafiki zake kujifunza kuomba ili kuzungumza na Baba wa Mbinguni. Alijua Baba wa Mbinguni anampenda na Baba wa Mbinguni anawapenda marafiki zake pia.

Chapisha