2023
Njia 4 Ambazo Yesu Kristo Anakuimarisha Wewe
Januari 2023


“Njia 4 Ambazo Yesu Kristo Anakuimarisha Wewe,” Kwa Ajili ya Nguvu Kwa Vijana, Jan. 2023.

Njia 4 Ambazo Yesu Kristo Kristo Anakuimarisha Wewe

Nayaweza mambo yote katika Kristo.
Wafilipi 4:13

Picha
mawe yaliyobebana

Ulimwenguni kote, Wakristo wanashangilia katika andiko hili: “Nayaweza mambo yote katika Kristo anitiaye nguvu” (Wafilipi 4:13).

Watu wanaposikia hii, baadhi yao wanaweza kufikiri inamaanisha wao wanaweza kufaulu kila mtihani, kushinda kila mchezo na kila watakalo linaweza kuja kuwa kweli. Lakini hicho siyo kitu kinachofundishwa na andiko hili.

Liliandikwa na Mtume Paulo wakati akiwa gerezani. Kama mfungwa, palikuwa na mengi ambayo Paulo hakuweza kufanya, lakini alijua kwamba Yesu Kristo angeweza kumuimarisha yeye kufanya kile kilichokuwa muhimu zaidi.

Hilo pia ni kweli kwako wewe!

1 Kristo Anakuimarisha Wewe ili Ujue

Yesu Kristo amekupa njia kadhaa muhimu unazoweza kuja kujua kile kilicho cha kweli. Yeye ametufundisha sisi sote kusali daima (ona 3 Nefi 18:18) na kuomba kujua kile kilicho cha kweli (ona Moroni 10:4–5). Pia unaweza kutafuta na kujua kile kilicho cha kweli kupitia kujifunza kwako maandiko.

Sala na kujifunza maandiko vinamleta Roho katika maisha yako. Roho anaweza kunena na “akili yako na … moyo wako” (Mafundisho na Maagano 8:2), “ataijaza nafsi yako kwa shangwe,” na “kuiangaza akili yako” (Mafundisho na Maagano 11:13).

Katika njia hizi, unaweza “kumsikia Yeye”—kusikia maneno ya Mwokozi na kufuata kile ambacho Yeye amesema. Rais Russell M. Nelson amefundisha kwamba huu ndiyo “mpangilio wa mafanikio, furaha na shangwe katika maisha haya.”1

2 Kristo Anakuimarisha Wewe ili Ufanye

Nguvu inakuja kwako kadiri unavyojitahidi kushika amri na kufanya chaguzi zilizo nzuri ambazo zinakuongoza kwenye amani na furaha. Yesu Kristo anakuimarisha wewe ili ufanye hili hata wakati chaguzi hizo ni ngumu kuzifanya. Nyakati zingine unaweza kufanya uchaguzi mbaya. Kwa shukrani, Upatanisho wa Mwokozi unafanya toba iwezekane. Kwa sababu ya Yesu Kristo, wewe unaweza kuwa safi na kupata shangwe. Yeye anaweza kukuimarisha ili “ufanye vizuri zaidi na kuwa bora zaidi”2 kila siku.

3 Kristo Anakuimarisha Wewe ili Ushinde

Wakati akiwa gerezani, Paulo aliandika: “Nimejifunza, kuwa radhi katika hali yoyote niliyonayo.

“Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa: katika hali yoyote, na katika mambo yote nimefundishwa” (Wafilipi 4:11–12).

Kwa maneno mengine, Paulo alijifunza kwamba, kupitia Kristo, yeye anaweza kushinda na kujifunza kutokana na majaribu na changamoto zake. Yesu Kristo anaweza kukuimarisha wewe ili ufanye vivyo hivyo.

Mwokozi aliteseka “maumivu na masumbuko na majaribu ya kila aina.” Alijichukulia juu yake unyonge wetu ili “ajue … jinsi ya kuwasaidia [ikimaanisha kuwapa msaada] watu wake kulingana na unyonge wao” (Alma 7:11–12). Bila kujali unachokabiliana nacho, Yesu Kristo anaweza kukuimarisha wewe ili ustahimili na kukamilisha mambo ambayo usingeweza kuyafanya peke yako.

4 Kristo Anakuimarisha Wewe ili Uwe

Yesu Kristo amefanya ufufuko kuwa uhalisia kwetu sisi sote na anafanya uzima wa milele uwezekane kwa wale wenye kutubu, kupokea ibada muhimu na kufanya na kushika maagano yanayohusiana na ibada hizo. Bila Kristo, sisi tusingeweza kutimiza kile Baba wa Mbinguni anachokitaka zaidi—ili sisi tuweze kuwa zaidi kama Yeye na Mwanawe, Yesu Kristo na kuishi pamoja Nao milele.

Picha
Yesu Kristo

Unaweza kuwa zaidi kama Yesu Kristo, unapojifunza juu Yake, unapomtegemea na kumtumaini Yeye na kufuata mfano Wake. Hii itakuongoza wewe kuishi kwa imani zaidi, tumaini, hisani, uvumilivu, unyenyekevu, usafi na utiifu zaidi. Hizi zote ni sifa za Mwokozi.

Unapojitahidi kumfuata Yesu Kristo, Yeye atakuwa ndiye tumaini lako na nuru yako ambayo itakuongoza wewe kuwa vyote ambavyo Yeye anajua kuwa unaweza kuwa. Na, pamoja na Paulo, utaweza kusema, “Nayaweza mambo yote katika Kristo anitiaye nguvu.”

Chapisha