Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana
Wewe na Mwokozi dhidi ya Ulimwengu
Machi 2024


“Wewe na Mwokozi dhidi ya Ulimwengu,” Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana, Machi 2024.

Nguvu ya Kuushinda Ulimwengu

Wewe na Mwokozi dhidi ya Ulimwengu

Vikengeusha fikra, majaribu, mateso—Yesu Kristo ameshinda mambo ya ulimwengu huu na anaweza kukuimarisha wewe kuyashinda pia.

Picha
mwanamke akiwa ameshika dunia mabegani mwake, huku mikono ya Bwana ikimfikia

Kielelezo na Alex Nabaum

Yesu Kristo aliushinda ulimwengu, na anatualika sisi kufanya vivyo hivyo. Lakini “ulimwengu” ni nini,” na ina maana gani kwetu kuushinda?

Rais Russell M. Nelson aliiweka hivi: “[Kuushinda ulimwengu] inamaanisha kushinda vishawishi vya kujali zaidi kuhusu mambo ya ulimwengu kuliko mambo ya Mungu.”1

“Vitu vya ulimwengu huu” vinaweza kujumuisha mali, umaarufu, mamlaka, sifa, raha au kitu kingine chochote ambacho mwanadamu wa asili anafurahia kama sehemu ya maisha ya duniani. Hata kama baadhi ya mambo haya si mabaya kila mara, tunapopoteza mwelekeo wetu kwa Mungu kwa sababu ya kujali zaidi mambo ya kilimwengu, tunaingia kwenye matatizo ya muda mrefu.

Yesu Kristo alifundisha kwamba tutakabiliana na upinzani na mateso tunauposhinda ulimwengu (ona Yohana 15:18–21) Lakini bado tunaweza kupata amani na “kuwa na moyo mkuu” kwa sababu Yeye aliushinda ulimwengu kwanza (Yohana 16:33).

Vijana hawa walipata nguvu katika Yesu Kristo kushinda vikwazo vya kidunia, na wewe pia unaweza!

Uharibifu wa Kidunia

Picha
msichana

Nilitumia saa nyingi kucheza michezo ya kompyuta kila siku kwa miaka mingi. Nilipata marafiki, na nilijiona kuwa muhimu. Lakini baada ya kucheza, nilihisi mtupu, kana kwamba kuna kitu kinakosekana. Sikuwa na furaha kabisa.

Nilitaka kufokasi kwenye mambo ambayo kwa kweli yangenifanya niwe na furaha na kunisaidia kuwa bora. Nilianza kusali mara kwa mara. Nilipoeleza kile kilichokuwa moyoni mwangu kwa Baba wa Mbinguni, nilihisi hisia zenye nguvu za upendo.

Nilitaka kufanya mambo ambayo yangenifanya niwe karibu zaidi na Kristo, kwa hivyo nilizingatia mambo rahisi kama vile kusoma maandiko kila siku na kusali, kutumia muda na watu waliokuwa na Roho Mtakatifu, na kujaribu kutokengeushwa na mambo ambayo yangemfanya Roho Mtakatifu kuondoka. Maisha yangu yalibadilika Ni furaha zaidi kwangu.

Ninapomkaribia Kristo, ninajua kwamba kuna mambo muhimu zaidi kuliko michezo ya kompyuta ikiwa ninataka kuwa na furaha ya kweli. Kuna mambo ambayo ni ya milele

Alina U., 18, Lithuania

Hali za Kidunia

Picha
msichana

Shuleni, nilinyanyaswa na kudhihakiwa kwa sababu ya imani yangu. Kwa sababu ya hilo na changamoto nyinginezo, nilihisi kama ulimwengu unaniangukia. Lakini mama yangu alinitia moyo kutegemea Upatanisho wa Yesu Kristo kwa sababu Yeye anaelewa maumivu yangu na anaweza kuniletea amani na faraja (ona Mafundisho na Maagano 19:23).

Niliamua kumuahidi Baba wa Mbinguni kwamba nitafunga mara kwa mara. Nilimwomba anisaidie katika udhaifu na mapambano yangu na amekuwa akifanya hivyo tangu wakati huo.

Kufunga kumenileta karibu na Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo. Ninajua Wako kando yangu kila wakati, wakinipa nguvu za kushinda changamoto zangu na kupata furaha ya kweli. Yesu Kristo anaponya majeraha yangu na kunisaidia kurudi kwa Baba yangu wa Mbinguni.

Vera R., 17, Brasília, Brazil

Chapisha