Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana
Tofauti Chanya ambayo Neema ya Kristo Inaweza Kufanya
Machi 2024


Tofauti Chanya ambayo Neema ya Kristo Inaweza Kufanya,” Kwa Ajili ya Nguvu ya Vijana, Machi 2024.

Nguvu ya Kuishinda Dhambi

Tofauti Chanya ambayo Neema ya Kristo Inaweza Kuleta

Tunapoelewa kwamba neema ya Mwokozi haitafutwi na kwamba inapatikana kila mara, mambo mazuri yanaweza kutokea katika maisha yetu.

Picha
mvulana akiwa ndani ya mzingile

Vielelezo na Jarom Vogeln

Nilipohudumu kama askofu, ilikuwa ya kupendeza kuona auheni waliyohisi vijana walipokutana nami kukiri dhambi kama sehemu ya toba yao. Bado, sikuweza kujizuia kuona mtindo unaojirudia: vijana wangeungama, wajisikie vizuri, kisha—licha ya nia yao nzuri—walikosea tena. Kisha wangekiri, kuhisi vizuri, na kukosea tena. Baada ya mara tatu au nne kupitia mzunguko huo, mara nyingi walikata tamaa.

Nilishukuru kwamba vijana hawa walikuwa wamefundishwa kwamba Yesu Kristo, kupitia Upatanisho Wake, anawapa nafasi ya kutubu na kuanza tena. Hata hivyo, nilikuwa na wasiwasi kwamba labda hawakuelewa vya kutosha kuhusu baraka nyingine ambayo Mwokozi hutoa: Neema Yake—nguvu iwezeshayo1, usaidizi wa kiungu na “majaliwa ya nguvu ambayo kwayo tunakua kutoka kwa viumbe wenye kasoro na wenye mipaka wa sasa tunakuwa viumbe vilivyoinuliwa.”2

Niliazimia kufundisha kwa uwazi zaidi, kama vile Rais Russell M. Nelson amefundisha, kwamba “toba … ni mchakato”3 ambao mara nyingi huchukua muda na juhudi za mara kwa mara.4 Nilitaka waumini wa kata yangu wajue Mungu hukutana nasi pale tulipo na hutoa neema ya kutusaidia katika mchakato mzima wa ukamilifu, bila kujali ni muda kiasi gani itachukua.

Jinsi Kuielewa Neema Inavyokusaidia

Miaka michache iliyopita, uchunguzi wa zaidi ya vijana 600 katika Chuo Kikuu cha Brigham Young ulionyesha kwamba wale waliojua na kuelewa kuhusu neema waliripoti viwango vya chini vya mfadhaiko, wasiwasi, aibu na ukamilifu.5 Uchunguzi wa ufuatiliaji ulionyesha kwamba imani katika neema ilihusishwa na viwango vya juu vya shukrani, kujiheshimu, maana ya maisha, kuridhika na maisha, na matumaini.6

Kwa maneno mengine, watu huhisi aibu kidogo na kujiheshimu zaidi wanapoelewa kuwa neema inapatikana hapa na sasa hivi—sio baada ya kuitafuta au kustahili. Tunapojua kwamba Mungu anatusaidia haijalishi ni nini tumefanya au ni mara ngapi tunahisi kwamba tumemwangusha, tunahisi kuchochewa kuendelea kujaribu.7

“Nimemwangusha Baba wa Mbinguni”

Hivi majuzi mmisionari mmoja alijeruhiwa wakati wa shughuli ya siku ya maandalizi na akarudishwa nyumbani ili kujiuguza. Alikuwa na malengo ya juu ya kupata msaada wa kimwili aliohitaji na kisha kurudi kwenye misheni yake. Hata hivyo, muda mwingi usio na mpangilio pekee ulisababisha kurudia mazoea ya zamani.

Alijiingiza katika dhambi ambayo alifikiri ameitubu na kuiacha kabla ya misheni yake. Alivunjika moyo na kukasirishwa na ukosefu wake wa kujisimamia. Kadiri alivyovunjika moyo zaidi, ndivyo alivyozidi kutafuta njia ya kuepuka mazoea hayo mabaya. Ilikuwa ni mzunguko wa kushuka chini ambao ulikuwa haumfikishi popote kwa haraka.

“Ninahisi kama nimemwangusha Baba wa Mbinguni,” kijana huyo alimwambia kiongozi wake wa ukuhani. “Nilitubu jambo hili hapo awali, na Mungu akanisamehe. Niliahidi kutofanya hivyo tena, na bado niko hapa kana kwamba sikuwahi kutubu hapo kwanza. Sistahili msamaha au msaada wa Mungu. Sio kwa sasa. Si milele.”

Kiongozi wake wa ukuhani alisema, “Hufurahii kujua kwamba neema ni zawadi? Hauhitaji kuitafuta au kuistahili. Unahitaji tu kuchagua kuipokea kwa kuwa tayari kuendelea kujaribu na kutokata tamaa.”8 Kiongozi kisha alishiriki maneno haya ya Mzee Neil L. Andersen wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili: “Tunaweza kushindwa nyakati zingine, lakini acha kwa haraka na kwa unyenyekevu turudi magotini mwetu na kusonga tena kwenye uelekeo sahihi.”9

Picha
mvulana akiwa anaondoka kwenye mzingile

Kwa mara nyingine tena, yule kijana aligeukia mbinguni, na Mwokozi alikuwa pale kusaidia. Sio tu jeraha la kijana huyo lilipona, lakini pia moyo wake. Lengo moja dogo kwa wakati mmoja, na kwa neema iliyowezeshwa na Yesu Kristo, alianza kuimarika. Punde alirudi kwenye misheni yake akiwa amejaa shukrani, kujistahi, hali ya maana, kuridhika na maisha, na matumaini. Hiyo ndiyo tofauti ambayo neema ya Kristo inaweza kuleta.

Muhtasari

  1. Mwongozo kwenye Maandiko, “Neema,” scriptures.ChurchofJesusChrist.org.

  2. Dieter F. Uchtdorf, “Kipawa cha Neema,” Apr. 2015 mkutano mkuu (Ensign au Liahona, Mei 2015, 107); ona pia 2 Nefi 2:6; Yakobo 4:7. Rais Russell M. Nelson alisema “Bwana hahitaji imani kamilifu kwetu kuweza kufikia nguvu Zake kamili” (“Kristo Amefufuka; Imani Katika Yeye Itahamisha Milima,” mkutano mkuu wa Aprili. 2021 [Liahona, Mei 2021, 102]).

  3. Russell M. Nelson, “Tunaweza Kufanya Vizuri Zaidi na Kuwa Wazuri Zaidi,” mkutano mkuu wa Apr. 2019 (Ensign au Liahona, Mei 2019, 67).

  4. Ona Mosia 26:30; Moroni 6:8; Mafundisho na Maagano 1:31–32.

  5. Ona Daniel K. Judd, W. Justin Dyer, and Justin B. Top, “Grace, Legalism, and Mental Health: Examining Direct and Mediating Relationships,” Psychology of Religion and Spirituality, vol. 12, no. 1 (Feb. 2020), 26–35; see also Daniel K. Judd and W. Justin Dyer, “Grace, Legalism, and Mental Health among the Latter-day Saints,” BYU Studies, vol. 59, no. 1 (2020), 5–23.

  6. Ona Justin Brent Top, “Grace, Legalism, and Life Outlook in LDS Students” Ph.D dissertation, May 14, 2021, scholarsarchive.byu.edu/etd/9505.

  7. Ona D. Todd Christofferson, mkutano mkuu wa Okt 2014 (Ensign au Liahona, Nov 2014, 19).

  8. Ona Steven J. Lund, “Kwa Nguvu Tunayoiita Neema,” Kwa Ajili ya Nguvu Kwa Vijana, Julai 2022, 13.

  9. Neil L. Andersen, Zawadi Takatifu ya Msamaha (2019), 208.

Chapisha