Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana
Je, Ninaweza Kutumikia Kama Mimi Si Mtu wa Kuchangamana?
Machi 2024


“Je, Ninaweza Kutumikia Kama Mimi Si Mtu wa Kuchangamana?,” Kwa Ajili ya Nguvu ya Vijana, Machi 2024.

Nguvu ya Kuhudumia

Je, Ninaweza Kutumikia Kama Mimi Si Mtu wa Kuchangamana?

Mwokozi anaweza kutuimarisha hata kama tuna wakati mgumu wa kuwafikia watu.

Picha
msichana akitembea barabarani

Nilipokuwa katika shule ya upili, nilifikiri sikuwa mfuasi wa thamani wa Yesu Kristo kwa sababu nilitatizika kuzungumza na watu. Sikuwa tu mzito kujichanganya—nilikuwa mwenye aibu sana! Nilikuwa mwenye aibu sana kiasi kwamba nilikuwa na wakati mgumu kupata marafiki na kuwa mkimya kweli kwa wanafunzi wenzangu shuleni na kanisani.

Kwa sababu hiyo, nilijiepusha na miito katika darasa la Wasichana na nilihisi kama nisingeweza kuwa wa kiroho kama wenzangu ambao walikuwa wazungumzaji zaidi na watu wa kijamii kuliko mimi.

Kwa hivyo nilipohitimu kutoka shule ya upili na kuamua kuhudumu misheni, niliogopa sana!

Nilihisi kama Mungu alitaka nimtumikie, lakini wazo langu la kwanza lilikuwa, “Kwa nini Mungu anataka mtu kama mimi atumikie? Siwezi kuzungumza na watu!”

Lakini kwa uwoga miliokuwa nao, hata hivyo niliamua kumwamini Mungu na kutumikia misheni.

Kutegemea Nguvu za Kristo

Nilipokuwa nikihudumu, mambo yalikuwa magumu mwanzoni, lakini nilipoendelea kujaribu (na kujiruhusu kushindwa), niligundua kwamba Bwana alinitia nguvu ili nifanye kazi aliyoniomba nifanye.

Katika Kitabu cha Mormoni Bwana anasema, “Kama watu watakuja kwangu mimi nitawaonyesha madhaifu yao. Ninawapatia watu udhaifu ili katika udhaifu wao wawe wanyenyekevu; na neema yangu inatosha watu wote ambao hujinyenyekeza mbele yangu; kwani wakijinyenyekeza mbele yangu, na kuwa na imani ndani yangu, ndipo nitafanya vitu dhaifu kuwa vyenye nguvu kwao” (Etheri 12:27).

Katika misheni yangu nilitambua kwamba Yesu Kristo angeweza kufanya mambo ya makubwa pamoja nami si kwa sababu ya nguvu zangu bali kwa sababu ya nguvu Zake. Na pia nilitambua kwamba nguvu Zake hazikuja kwangu kwa sababu tu nilikuwa mmisionari, lakini pia ni kitu ambacho ningeweza kutegemea katika shule ya upili.

Jambo maridadi kuhusu Yesu Kristo ni kwamba hatuhitaji shahada au wasifu wa kina ili kuhudumu katika ufalme Wake na kuwa wanafunzi wenye nguvu! Kama tu wanyenyekevu na waaminifu katika tamaa zetu za kutumikia, Yesu Kristo atatuchukua kama vile tulivyo, mahali tulipo, na kutupa usaidizi unaohitajika na nguvu za kumtumikia Yeye.

Chapisha