2022
Maandiko Hugeuza Mioyo Yetu kwa Mungu
Julai/Agosti 2022


“Maandiko Hugeuza Mioyo Yetu kwa Mungu,” Liahona, Julai/Agosti. 2022.

Njoo, Unifuate

2 Wafalme 21–23

Maandiko Hugeuza Mioyo Yetu kwa Mungu

Rais Spencer W. Kimball alisema kwamba hadithi ya Yosia, inayopatikana katika 2 Wafalme 21–23, “ni mojawapo ya hadithi nzuri sana katika maandiko yote” (katika Njoo, Unifuate—Kwa Ajili ya Watu Binafsi na Familia: Agano la Kale 2022, 129).

Jinsi Mfalme Yosia Alivyopata Maandiko

Picha
Mfalme Yosia akiwaelekeza watu kubomoa sanamu

Mfalme Yosia Akitakasa Ardhi ya Sanamu, © Look and Learn / Bridgeman Images

Yosia alikuwa Mfalme wa Yuda alipokuwa na miaka minane tu. Alirithi ufalme wa watu ambao waliamini kwenye miungu ya uongo, lakini alitaka kumfuata Bwana. Katika mwaka wa nane wa utawala wake, aliagiza kwamba madhabahu na sanamu za miungu ya uongo itokomezwe katika Uyahudi yote.

Picha
watu wakisoma maandiko

Yosia, Mfalme wa Yuda, Anarejesha Utamaduni wa Kumwabudu Mungu katika Ufalme Wake, na mwanasanaa asiyejulikana, picha na Stefano Bianchetti / Bridgeman Images

Miaka kumi baadaye, aliwataka watu wake kurejesha hekalu huko Yerusalemu, ambako kuhani mkuu Hilkia alipata maandiko. Mfalme Yosia alipokisoma kitabu, alivuviwa kufuata mafundisho ya kitabu hicho. Kisha alikusanya watu wake na kuwasomea kitabu hicho.

Kwa muda mrefu, watu walikuwa wameshupaza mioyo yao dhidi ya Mungu. Lakini maandiko yalisaidia kugeuza mioyo ya watu kumrudia Mungu. Mfalme Yosia aliwaahidi watu kwamba atatembea katika njia za Bwana na kutii amri.

Chapisha