2022
Je, Isaya Alifundisha Nini kuhusu Kukusanywa kwa Israeli?
Septemba 2022


“Je, Isaya Alifundisha Nini kuhusu Kukusanywa kwa Israeli?,” Liahona, Sept. 2022.

Njoo, Unifuate

Isaya 1–12

Je, Isaya Alifundisha Nini kuhusu Kukusanywa kwa Israeli?

Picha
muonekano wa Bonde la Salt Lake

Muonekano wa Jiji la Salt Lake, na James Taylor Harwood

Isaya alitumia ishara ili kufundisha kuhusu kukusanywa kwa Israeli. Fikiria andiko hili: “Na atawainulia mataifa bendera, na kuwakusanya watu wa Israeli waliofukuzwa, na kuwakusanya pamoja wale waliotawanywa wa Yuda kutoka pembe nne za dunia”(11:12).

Ensign ni bendera au kiwango. Mzee Jeffrey R. Holland wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili alishiriki hadithi ya jinsi viongozi wa Kanisa katika zama za uanzilishi walitengeneza bendera, “bendera ya muda, wakitamka juu ya bonde la Great Salt Lake na milima inayolizunguka bonde hilo kama ndipo mahali palipotolewa unabii kwamba kutoka hapo neno la Bwana lingetoka katika siku za mwisho.”1

Je, ni ishara na utambuzi gani unaohusiana na kutawanywa na kukusanywa kwa Israeli unaweza kupata katika sura ya Isaya 2, 5, na 11?

Je, ni kwa jinsi gani manabii wa leo wametusaidia sisi kuelewa vyema zaidi juu ya kuikusanya Israeli.

Inaweza kuwa ya msaada kujifunza kile ambacho manabii wa sasa wamesema kuhusu mafundisho ya Isaya na kukusanywa kwa Israeli. Fikiria kuzipitia mojawapo ya hotuba za mkutano mkuu za Rais Russell M. Nelson na orodhesha njia ambazo wewe unaweza kusaidia kukusanya Israeli.

Muhtasari

  1. Jeffrey R. Holland, “Bendera kwa Mataifa,” Liahona, Mei 2011, 111.

Chapisha