2022
Je, Tunaweza Kufanya Nini ili “Kuelekeza Sikio [Letu] kwenye Hekima”?
Septemba 2022


Je, Tunaweza Kufanya Nini ili “Kuelekeza Sikio [Letu] kwenye Hekima’?,” Liahona, Sept. 2022.

Njoo, Unifuate

Mithali 1–4; 15–16

Je, Tunaweza Kufanya Nini ili “Kuelekeza Sikio [Letu] kwenye Hekima”?

Picha
mwanamke mwenye kufikiri kwa makini

Pamoja na taarifa nyingi zisizo sahihi ulimwenguni, inaweza kuwa vigumu kuzichambua zote na kupata ukweli wa milele. Baba wa Mbinguni analijua hili, na Yeye anajua kwamba wengi wa watoto Wake wanatafuta majibu. Kwa shukrani, mengi ya majibu kwa maswali magumu zaidi juu ya maisha yanaweza kupatikana katika maandiko, hotuba za mkutano mkuu, au kwa njia ya ufunuo binafsi. Baba wa Mbinguni katu hawezi kutupoteza sisi.

Shughuli

Katika Mithali, mara kwa mara tunasoma kuhusu hekima. Soma sura ya 2 na 3 kibinafsi au kama kikundi na muitambue mistari ambayo inajadili jinsi tunavyotafuta hekima. Kwa mfano, Mithali 1:5 inasema, “mwenye hekima asikie, na kuongezewa elimu; na mwenye ufahamu ayafikie mashauri yenye njia.”

Chapisha