2022
Je, Isaya Alifundisha Nini kuhusu Kuwa Mtumishi wa Bwana?
Septemba 2022


“Je, Isaya alifundisha Nini kuhusu Kuwa Mtumishi wa Bwana?,” Liahona, Sept. 2022.

Njoo, Unifuate

Isaya 40–49

Je, Isaya Alifundisha Nini kuhusu Kuwa Mtumishi wa Bwana?

Bwana mara nyingi anawataja wafuasi Wake kama watumishi au mashahidi Wake. Maneno hayo yanapatikana kote kwenye maandiko, na kitabu cha Isaya hakina tofauti. Katika nyakati za Agano la Kale, kama vile leo, Bwana aliwapa watu fursa za kumhudumia Yeye na kuwa mashahidi Wake.

  • Unaposoma Isaya sura ya 40–49, angalia nyakati ambapo Bwana anasema “mtumishi” au “shahidi.” Yeye anamrejelea nani? Angalia mistari ambayo inafundisha jinsi wewe unavyoweza kuwa shahidi kwa Bwana, kama vile Isaya 44:2.

    Picha
    Joseph Smith akihubiri

    Joseph Smith Akihubiri, na Sam Lawlor © 2001

  • Kisha, unaposoma sura ya 41–44, unaweza kufikiria ni mstari gani unaweza kutumika kwenye wito au utumishi wako. Bwana anakutaka wewe ufanye nini, na ni kwa namna gani Yeye atakusaidia wewe?

    Picha
    wanawake watatu wakitabasamu
  • Je, ni fursa gani wewe umepewa ili uwe mtumishi au shahidi wa Bwana? Mifano inaweza kuwa wito, misheni, kuifundisha familia yako, au huduma nyingine. Unaweza kuandika uzoefu huo katika shajara yako. Je, umejifunza nini kutokana na hivyo? Je, Bwana alikusaidiaje?

    Picha
    wamisionari wakihudumu

Chapisha