2022
Mbio za Kuni
Julai/Agosti 2022


Mbio za Kuni

Nabii alisema kamwe tusiache kujiandaa.

Picha
boy holding firewood

Miguu ya Luke ilikanyaga chini kwa kishindo. Alitazama nyuma. Robert, kaka yake, alikuwa anamkaribia!

“Tag! Ni zamu yako!” Robert alisema.

Luke alicheka. Alimkimbiza dada yake mkubwa, Mili.

Baada ya mchezo, kila mtu alikaa chini kupumzika.

“Je, Tunaweza kucheza mchezo upi sasa?” Mili aliuliza.

Luke alifurahi kuwa na ndugu wa kucheza nao. Lakini UVIKO-19 ulibadilisha mambo mengi. Hawangeweza kwenda sehemu zenye watu wengi. Na nyakati zingine hawakuruhusiwa hata kuwa nje.

Luke alijaribu kufikiria mchezo ambao wengeweza kuucheza. Kisha akawaza kuhusu kitu fulani alichosikia katika Msingi.

“Nafikiri tunapaswa kufanya kitu fulani ili kujiweka tayari,” Luke alisema.

“Unamaanisha nini?” Mili aliuliza.

Luke alitazama miti ya mipera kuzunguka nyumbani kwao. “Nabii alisema hatupaswi kamwe kuacha kujiandaa. Pengine tunaweza kukusanya kuni leo. Tunaweza kuufanya kuwa mchezo ili kuona nani atakusanya nyingi zaidi!”

Picha
boy and girl running and holding firewood

Luke na ndugu zake walikimbia kuelekea kwenye miti karibu na nyumba yao. Luke alikusanya rundo mikononi mwake na kukimbia kuzipanga kwenye banda. Wakati ndugu zake walipofika hapo, aliwasaidia kupanga kuni zao pia. Walikimbia tena na tena kwenda na kurudi mpaka wakakusanya rundo kubwa.

“Hizi zinatosha kupikia wiki nzima!” Mili alisema.

“Hiyo ilikuwa ya kufurahisha,” Robert alisema. “Ninapenda kujiandaa!

“Mimi pia,” Luke alisema. Alitaka kufanya kitu kiingine ili kujiandaa.

Kilichofuatia yeye, kaka yake na dada yake walipanda bele (mboga za kijani) shambani kwao. Luke alikata miche kutoka kwenye mimea mizee ili waweza kuipanda na kuikuza zaidi.

Walipokuwa wakifanya kazi, babu na bibi pamoja na wazazi wao walikuja nje.

“Je, mmepanda mimea ya bele wenyewe? Babu aliuliza.

“Ndio,” Luke alisema. “Pia tulikushanya kuni!”

“Asanteni,” Baba alisema. “Nilikuwa na shughuli nyingi sana leo. Nisingeweza kutimiza hilo.

Mchana ule, Luke alikaa ndani pamoja na familia yake. Walisikia tangazo kwenye redio kwamba kila mtu angepaswa kukaa nyumbani kwa siku nne ili kuzuia kuenea kwa UVIKO-19. Hakuna mtu aliyeruhusiwa kutoka nyumbani kwao.

“Ni vyema tulikusanya kuni leo. Hatungeweza sasa,” alisema Mili.

Luke alitabasamu. Alikuwa na furaha kwamba walikuwa wamefuata mwaliko wa nabii wa kujiandaa.

Vielelezo na Shawna J. C. Tenney

Chapisha