2021
Pishi Jipya la Winfred
Julai/Agosti 2021


Pishi Jipya la Winfred

“Tuliishi kwa furaha” (2 Nefi 5:27).

Je, Winfred angeweka nini kwenye pishi lake?

Picha
girl praying

Winfred alikuwa akimsaidia Jajja (Bibi) kutayarisha chakula cha jioni.

Mmm, ninapenda matoke,” Jajja alisema.

“Mimi pia,” Winfred alisema. “Hiyo ni moja kati ya milo ninayoipenda! Ninapenda ndizi za kijani. Na pilipili na nyanya. Lakini sehemu nzuri zaidi ni mchuzi.”

“Hiyo ni kwa sababu mchuzi unachanganya ladha zote kuwa moja,” Jajja alisema.

Waliendelea kukata mboga. Kisha Winfred akavuta pumzi.

“Jajja,” alisema, “ni kwa vipi wewe huwa mwenye furaha wakati wote?”

“Ninajaribu,” Jajja alisema. “Lakini sina furaha wakati wote. Huzuni ni sehemu ya maisha. Je, una huzuni sasa hivi?”

Winfred alikubali kwa kichwa. “Ninamkosa Taata (Baba), kwa sababu anafanya kazi mbali sana. Na ninakumbuka shuleni, kwa sababu hatuwezi kwenda sasa hivi. Na ninawakosa marafiki zangu wa kanisani.”

“Ni Sawa kuhisi huzuni kuhusu mambo hayo,” Jajja alisema. “Maisha si rahisi wakati wote.” Lakini ninapokuwa na huzuni, ninajaribu kufuata pishi langu la kuleta furaha.”

“Pishi lako?”

“Kama jinsi nilivyo na namna ya upishi wa matoke, nina pishi kwa ajili ya furaha. Wakati mwingine huzuni ni kubwa sana kuweza kutoweka mara moja.” Lakini mara nyingi ninakuta kuwa pishi langu ndilo tu nililohitaji ili kuhisi vizuri.”

“Pishi lako ni lipi?”

Jajja alitabasamu. “Kwa nini usijaribu kuona kama unaweza kujitengenezea pishi lako mwenyewe? Kisha unaweza kuniambia kuhusu hilo.”

Usiku huo wakati Winfred akisali, alijua Baba wa Mbinguni alikuwa akisikiliza. Alitambua kwamba sala ilimfanya kuwa mwenye furaha! Alichukua karatasi na kuandika, Pishi la Winfred kwa ajili ya Furaha. 1. Sali. Kisha akaenda kulala.

Asubuhi iliyofuata alisoma Kitabu cha Mormoni. Kusoma maandiko kulimfanya kuwa na furaha pia. Alitafuta karatasi yake na kuandika, 2. Soma maandiko. Kisha aliangalia maandiko aliyokuwa amefungua: “Mwamini Kristo” (2 Nefi 33:10).

Winfred aliongeza dokezo jingine: 3. Kuwa na imani katika Yesu Kristo.

Winfred alifikiria kuhusu jinsi Jajja alivyokuwa mwema kumruhusu kumtembelea. Winfred alimwambia Jajja, “Asante kwa kuniruhusu kukaa nawe.”

Kusema asante kulimfanya Winfred kuhisi vizuri. Aliandika kwenye karatasi yake tena. 4. Kuwa na shukrani.

Kisha Winfred akawauliza jirani zake ikiwa watoto wangeweza kuja na kucheza. Alimleta dada yake mdogo, Milfred na kaka yake mdogo, Alfred. Walipomaliza kucheza, aliwaalika watoto kusoma pamoja naye. Jajja alikata tikitimaji ili kila mmoja ale.

Baadaye Winfred alienda kumtembelea rafiki yake anayeitwa Happy. Kwa pamoja, waliosha vyombo vya mama wa Happy. Kisha wakafagia sakafu. Ilikuwa raha sana kusaidia!

Jioni ilipofika, Winfred aliwasaidia ndugu zake kazi ya ziada ya shuleni. Alisoma alfabeti pamoja na Milfred. Alimsaidia Alfred hisabati yake.

Usiku huo, Winfred alizungumza na Jajja tena.

“Ninahisi vizuri zaidi leo! Nadhani nilipata pishi langu kwa ajili ya furaha.”

“Vizuri! Niambie,” alisema Jajja.

“Pishi la Winfred kwa ajili ya Furaha,” alisoma. “1. Sali. 2. Soma maandiko. 3. Kuwa na imani katika Yesu Kristo. 4. Kuwa na shukrani.”

“Hilo ni pishi zuri sana,” Jajja alisema. “Lakini ninadhani huenda umesahau kitu. Je, ni nini kingine kilichokufurahisha leo?”

Winfred alifikiri kwa dakika moja. “Vema, niliburudika kucheza na watoto. Na kumsaidia Happy na mama yake. Na kusoma pamoja na Milfred na Alfred. Subiri … ni hivyo tu! Kuwasaidia wengine ni kiamba upishi cha mwisho.”

“Hiyo ni sahihi,” Jajja alisema. “Kuwatumikia wengine ni kama mchuzi—huchanganya mambo mengine yote mazuri kuwa kitu kimoja.”

“Hilo ni pishi zuri.” Winfred alitabasamu. “Ninataka kulijaribu tena kesho.”

Hadithi hii ilitokea huko Kampala, Uganda

Picha
Friend, July 2021 Tier 2

Vielelezo na Hollie Hibbert

Chapisha