2023
Kujiunga na Timu Moja
Julai 2023


“Kujiunga na Moja,” Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana, Julai 2023.

Kujiunga na Timu Moja

Wapinzani hawa wawili shuleni walikuja kuwa marafiki maisha yao yote.

Picha
akina dada wamisionari

Picha na Jeffery Barker Edwards

Dada Dil alibakiwa na wiki sita tu katika misheni yake huko Australia wakati alipogundua kwamba atatumia muda wake uliobakia akihudumu na Dada Tuala!

“Hicho ni kitu cha mwisho kabisa kukikubali kama ningeulizwa,” anasema Dada Dil.

Picha
wasichana wakiwa wamevalia jezi za mpira wa kikapu

Dada Dil na Dada Tuala walikuwa wachezaji waanzishaji kwa timu za shule zao za upili zenye upinzani wa hali ya juu huko Auckland, New Zealand. Walikuwa wapinzani. Mara kwa mara walikuwa wakicheza timu pinzani katika mashindano ya fainali, na haikuwa ya kupendeza.

“Kuiweka katika muktadha sahihi kidogo,” anasema Dada Tuala, “tungetoka uwanjani tukiwa na mikwaruzo na michubuko.”

Picha
wasichana wakicheza mpira wa kikapu

Dada Dil na Dada Tuala walitumia muda wao mwingi wakijifunza na kucheza mpira wa kikapu. “Mpira wa kikapu ulikuwa ndiyo maisha yetu,” anasema Dada Dil.

Baada ya kuhitimu elimu ya shule ya upili wote walihisi kuvutiwa kwenda kuhudumu misheni—ingawa hakuna hata mmoja wao aliyehisi hamu ya kuhudumu kabla.

Kufanya Uchaguzi wa Kuhudumu

Kwa Dada Tuala, ilichukua muda kuoanisha mapenzi yake na mapenzi ya Bwana. “Nilikuwa na umri wa miaka 21 wakati nilipofanya uamuzi wa kutendea kazi msukumo huo,” anasema. “Nilikuwa nikipambana nao hadi nilipokuwa ndani ya ndege.”

Dada Tuala aliwasili kwenye misheni yake huko Australia wakati wa janga la ulimwengu la UVIKO-19, na ingawa ilikuwa vigumu, anashukuru sana kwa kuamua kuhudumu.

“Siwezi kufikiria kuwa Dada Tuala yule yule niliyekuwa nilipokuwa na miaka 21. Hakika ninajiona nimekua.”

Dada Dil alikuwa na msukumo wa “wazi na wa moja kwa moja” wa kuhudumu misheni wakati alipopokea baraka yake ya patriaki. Baada ya muda, aliamua kufuata msukumo wa kuhudumu, kwa sababu “mapenzi ya Bwana daima ndiyo njia sahihi na uchaguzi ulio bora.” Wito ulikuja, na alifungasha mabegi yake kwenda kuhudumu huko Australia.

Kujiunga na Timu Moja … kwa Mbali

Kwa sababu tu Dada Dil na Dada Tuala walihudumu katika misheni moja haikumaanisha kwamba walikuwa marafiki mara moja. Baada ya kuwa wapinzani kwa muda mrefu, Dada Dil na Dada Tuala bado walikuwa na wakati mgumu wa kuangaliana kama kitu kingine chochote.

Ukweli ni kwamba, siku ya kwanza Dada Tuala alipomwona Dada Dil, moja ya wazo lake la kwanza lilikuwa, “sijui kama ninapaswa kumpenda huyu.”

Picha
akina dada wamisionari

Kumaliza Mgogoro

Hivyo wakati Dada Tuala na Dada Dil walipopangiwa kuhudumu pamoja, ilionekana si sawa.

Wote walikuwa na mawazo kuhusu kila mmoja kulingana na vile walivyocheza kwenye uwanja wa mpira wa kikapu. Kila mmoja alidhani mwenzake alikuwa mgomvi, mwenye ushindani, na mkatili.

Lakini mambo yalibadilika kadiri walivyokuwa wakiendelea kufahamiana. Dada Dil alitambua Dada Tuala alikuwa “kinyume kabisa” na jinsi alivyokuwa akimwona siku zote. “Kwa kweli ni mtu mwenye upendo sana—mmoja wa mmisionari mwenza mwenye upendo zaidi niliowahi kuhudumu pamoja nao,” Dada Dil anasema.

Dada Tuala alipata uzoefu sawa na huo. Hakutambua kwamba hisia zake za upinzani kwa Dada Dil zilikuwa “ni mgogoro bila kukusudia” katika maisha yake.

Picha
akina dada wamisionari

Hisia hizo hasi za mgogoro na hukumu zilibadilishwa na upendo na maelewano pale alipoanza kumwona Dada Dil katika uhalisia kama alivyo. Na ingawa Dada Tuala alidhani Dada Dil alikuwa mkimya, aligundua kwamba “Dada Dil anaweza kuzungumza!”

Katika urafiki wao mpya walioupata, Dada Dil na Dada Tuala walitambua kwamba yawezekana hawakutambua kwamba hakika wao kamwe hawakuwahi kuwa maadui.

“Katika mpira wa kikapu unajenga katika akili yako kwamba sisi lazima tushinde, na kila mtu wa timu nyingine ni adui,” anasema Dada Dil. “Na mpira wa kikapu unapomalizika, basi unatambua, ‘Ah, hawa sio maadui tena. Pengine kamwe hawakuwa adui kabisa.’”

Sasa, Dada Dil na Dada Tuala wanaona kwamba wako kwenye “timu” moja—timu ya Mungu.

Picha
Yesu Kristo

Kristo akiwa Katikati, na Judith Mehr

Dhabihu ya Yesu Kristo Ni kwa ajili ya Kila Mtu

Akina dada wote wawili walihisi mkono wa Mungu katika kupangiwa kwao kama wamisionari wenza na wanajua nguvu ya Upatanisho ya Yesu Kristo iliwaruhusu wao kupitia uponyaji na badiliko.

“Yesu Kristo alifanya dhabihu ile ili mambo haya yote yaliyokwenda kombo siku zilizopita yaweze kuponywa, kusahihishwa, na kufanywa bora zaidi,” Dada Dil anasema. “Tunaweza kusamehe. Tunaweza kusahau. Tunaweza kusonga mbele, na mambo yakabadilika.

Siyo tu Dada Tuala na Dada Dil waliponya mgogoro wao, lakini pia walijifunza jinsi ya kuwaona wengine kama Mungu anavyowaona.

“Kuja hapa na kuweza kumwona mwenza wangu na watu wengine katika nuru tofauti, ninatambua kwamba kila hadithi ya mtu ni muhimu,” anasema Dada Tuala. “Na kila mtu anahitaji Upatanisho wa Yesu Kristo.”

Walijifunza kwamba ingawa inaweza kuwa vigumu, inawezekana kwa watu wawili ambao wakati mmoja walikuwa wanaonana kama maadui kuja pamoja kupitia upendo.

“Haijalishi umri ulio nao au kabila lako,” anasema Dada Tuala, “au uwe mpagani au mwenye dini.

Picha
akina dada wamisionari wakisali

“Kama ninaweza kufanya kazi sambamba na mtu ambaye sikuwahi kuwa na uhusiano mkubwa naye, na sisi wawili tunakuja pamoja kwa kusudi moja kuu, basi hata watu wengine wanaweza pia.”

Chapisha