2023
Unganika
Septemba 2023


“Unganika,” Kwa Ajili ya Nguvu kwa Vijana, Septemba 2023

Unganika

Sisekelo Q.

15, Afrika Kusini

Picha
msichana

Picha na Ntebaleng Twala

“Daima mimi husali kwa ajili ya mafanikio na ustawi wa familia yangu. Lakini baadhi ya vitu bado havijatoa ufumbuzi jinsi nilivyo tegemea. Nilianza kujiuliza ikiwa Mungu alikuwa akisikiliza sala zangu. Jinsi mashaka yangu yalivyozidi kuwa mabaya, Nilisali mara chache. Niliwaza, kwa nini napaswa kusali wakati sihisi chochote?”

Lakini kisha siku moja, nilitambua kuwa nilikuwa na wasiwasi na Mungu. Siku zote amekuwa Baba yangu wa Mbinguni, msaada wangu mkubwa sana na nguvu. Nilianza kulia. Nilipofika nyumbani siku ile, Nilipiga magoti kusali kwa sababu nilijihisi nimepotea kiroho na kihisia.

Baada ya kusali, nilihisi kufarijika, hisia nzuri, na upendo. Nilijua Alikuwa pamoja nami. Ninajua Baba wa Mbinguni anaona jitihada zetu na anasikia vilio vyetu. Kutoka siku ile na kuendelea, Nilielewa kwamba Ana mipango mikubwa kwa ajili ya familia yangu—mipango ambayo inahitaji ratiba Yake na subira yangu.

Chapisha