2019
Je, Unakosa Sehemu Hii Muhimu ya Kuhudumu?
Oktoba 2019


Kanuni za Kuhudumu

Je, Unakosa Sehemu Hii Muhimu ya kuhudumu?

Kuhudumu ni “kufurahi pamoja nao wafurahio” kama ilivyo “kulia pamoja nao waliao” (Warumi 12:15).

Picha
man at a party holding a tray with people dancing on it

Vielelezo na Augusto Zambonato

Tunapofikiria kuhusu kuhudumu, ni rahisi kuwafikiria wale walio katika uhitaji. Tunazungumza kuhusu kutengeneza bustani kwa ajili ya mjane, kupeleka mlo wa usiku kwa mgonjwa, au kutoa kwa wale wanaosumbuka. Tunakumbuka ushauri wa Paulo wa “kulia pamoja nao waliao,” lakini je, tunafokasi vya kutosha kwenye kipengele cha kwanza cha fungu hilo—cha “kufurahi pamoja nao wafurahio”? (Warumi 12:15). Kufurahi pamoja na wale tunaowatumikia—hiyo ikiwa inamaanisha kusherehekea mafanikio yao au kuwasaidia kupata furaha katika nyakati ngumu—ni sehemu muhimu ya kuhudumu kama ambavyo Mwokozi angehudumu.

Hapa kuna mawazo matatu yanayoweza kusaidia (na moja kuepuka) tunapotazama kwenye kufokasi katika mema Mungu anayoweka katika maisha yetu.

1. Kuwa Mwangalifu

Bonnie H. Cordon, Rais Mkuu wa Wasichana, anatusaidia kuelewa kwamba tunahitaji kuwaona wale tunaowahudumia—kuona si tu mizigo yao na mahangaiko bali pia uwezo wao, talanta, na mafanikio yao. Alisema kwamba tunahitaji kuwa “mshindi, na mwandani—mtu anayejua hali zao na kuwasaidia katika matumaini na matamanio yao.”1

Katika mfano wa kondoo na mbuzi, Mwokozi alisema wale ambao wangekuwa kwenye mkono Wake wa kuume wangeuliza: “Bwana, ni lini tulipokuona una njaa, tukakulisha? au una kiu tukakunywesha?

“Tena ni lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha? (Mathayo 25:37–38).

Akina kaka na akina dada, neno la msingi ni ona,” Dada Cordon alisema. “Wenye haki waliwaona wale walio na mahitaji kwa sababu walikuwa wakiangalia na kutambua. Sisi pia tunaweza kuwa jicho la kuangalia ili kutoa msaada na kufariji, kusherehekea na hata kuota.”2

2. Tafuta Sababu za Kusherehekea

Sherehekea mafanikio makubwa au madogo. Ingeweza kuwa unashinda saratani au kushinda kuachana, kupata kazi mpya au kupata kiatu kilichopotea, kuvumilia mwezi mzima baada ya kumpoteza mpendwa au kuvumilia wiki nzima bila sukari.

Piga simu kwa ajili ya kupongeza, peleka kadi, au toka kwa ajili ya chakula cha mchana. Kwa kushiriki baraka zetu pamoja, kuishi kwa shukrani, na kusherehekea baraka na mafanikio ya wengine, tunakuwa “tumeshangilia kwa shangwe kwa raha ya ndugu zetu” (Alma 30:34).

Picha
woman clapping while people dance

3. Ona Mkono wa Bwana

Wakati mwingine kushangilia pamoja na wengine humaanisha kuwasaidia kuona sababu ya kushangilia—bila kujali magumu yapi au mazuri yapi yanaingia katika maisha yetu. Ukweli rahisi kwamba Baba wa Mbinguni anatufahamu na yu tayari kutuinua unaweza kuwa chanzo cha kupendeza cha furaha.

Unaweza kuwasaidia wengine kuona mkono wa Bwana katika maisha yao kwa kushiriki jinsi ulivyouona katika maisha yako. Kuwa mzoefu vya kutosha kushiriki jinsi Baba wa Mbinguni alivyokusaida kupitia changamoto zako. Ushuhuda huu unaweza kuwasaidia wengine kugundua na kutambua jinsi Yeye alivyowasaidia (ona Mosia 24:14).

4. Usiwekee Ukomo Uwezo Wako wa Kufurahi

Kwa bahati mbaya, tunaweza wakati mwingine kuwekea ukomo uwezo wetu wenyewe wa kufurahi pamoja na wengine, hasa wakati tunapohisi mashaka kuhusu kile tunachopaswa kutoa au pale tulipo katika maisha. Badala ya kutafuta shangwe katika furaha ya mwingine, tunaangukia kwenye mtego wa kujilinganisha. Na kama Mzee Quentin L. Cook wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawilii alivyofundisha: “Kulinganisha baraka hakika ni karibu sawa na kutupilia nje furaha. Hatuwezi kuwa wenye shukrani na wenye wivu kwa wakati mmoja.”3

“Ni kwa jinsi gani tunaweza kushinda tabia hiyo ambayo ni ya kawaida sana karibu kwa kila mmoja wetu?” aliuliza Mzee Jeffrey R. Holland wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili.”… Tunaweza kuhesabu baraka zetu nyingi na tunaweza kushangilia mafanikio ya wengine. Kizuri zaidi ya yote, tunaweza kuwatumikia wengine, zoezi zuri kuliko yote la moyo ambalo limewahi kuelezewa kabla.”4 Badala ya kujilinganisha, tunaweza kuwasifia wale tunaowatumikia. Kwa uhuru shiriki kile unachopendezewa nacho kuhusu wao au wanafamilia wao.

Kama Paulo anavyotukumbusha, sisi sote ni viungo katika mwili wa Kristo, na wakati “kiungo kimoja kikitukuzwa, viungo vyote hufurahi pamoja nacho” (1 Wakorintho 12:26). Kwa msaada wa Baba wa Mbinguni, tunaweza kujua uzoefu wa watu wengine, kufurahia mafanikio makubwa na madogo, kuwasaidia kutambua mkono wa Bwana, na kushinda wivu ili kwamba tuweze kufurahia pamoja kwenye baraka, talanta, na furaha ya wengine.

Muhtasari

  1. Bonnie H. Cordon, “Kuwa Mchungaji,” Liahona, Nov. 2018, 75.

  2. Bonnie H. Cordon, “Kuwa Mchungaji,” 75.

  3. Quentin L. Cook, “Furahi!” Ensign, Nov. 1996, 30.

  4. Jeffrey R. Holland, “Mpotevu Mwingine,” Liahona, Mei. 2002, 64.

Chapisha