2019
Kusonga Mbele baada ya Kujua juu ya Matumizi ya Ponografia ya Mchumba Wangu
Oktoba 2019


Kidijitali Pekee: Vijana Wakubwa

Kusonga Mbele baada ya Kujua juu ya Matumizi ya Ponografia ya Mchumba Wangu

Mchumba wangu hatimaye alikiri kwamba alikuwa na tatizo la ponografia. Je, bado ningeweza kuolewa naye?

Mwandishi anaishi French Polynesia.

Nilikutana na mume wangu wakati sote tukiwa washauri wa EFY. Nilivutiwa kwa ushuhuda wake imara na jinsi alivyofundisha na kuchangamana na vijana.

Tulipoanza kuwa na miadi, tulihisi kana kwamba Bwana alihitaji jambo kutoka kwenye uhusiano wetu. Uhusiano wetu ulipoendelea, hata hivyo, alikuwa zaidi mwenye kusisitiza katika jinsi alivyoonyesha mapenzi. Nilianza kuwa na shaka kwamba alikuwa na shida ya ponografia, lakini tulipoliongelea, alikana kwamba alikuwa na tatizo hilo.

Tulianza kuweka sheria kali zaidi ili kujilinda wenyewe. Wakati aliponichumbia, nilikubali na mambo yalikuwa mazuri—mpaka siku moja wakati, tena, alianza kusisitiza kunionyesha ananipenda katika njia ambazo zilinifanya nisijisikie vizuri.

Bado nilikuwa na shaka kuhusu matumizi yake ya ponografia, hivyo siku moja nilimwambia kuhusu mmoja wa wamisionari wenzangu ambaye alipambana na ponografia kabla ya misheni yake. Nilijitahidi kadiri niwezavyo kuonekana kuelewa, mwenye upendo, na kutokuhukumu, kwa sababu alikuwa kweli mtu mzuri. Kisha nilimuuliza tena kama alikuwa anatawaliwa na ponografia, na hatimaye aliniambia alikuwa anatawaliwa.

Kuumia na Kupona

Mwanzo, ilikuwa vigumu kwangu kuzungumza naye na kumtazama machoni. Hisia zangu zilikuwa karibu kutovumulika kwa sababu nilihisi kwamba Bwana alikuwa ameniambia kwamba mwanaume huyu angekuwa mwenza wangu wa milele. Lakini japokuwa niliumia, nilijua nilitakiwa kufanya kazi ili kumsamehe, na nilihisi kupata msukumo wa kutokata tamaa kwenye uhusiano wetu.

Nilisali sana na kusoma mahubiri kuhusu msamaha na matumizi ya ponografia. Nilisoma makala nyingi na shuhuda nyingi za wanandoa ambao wenza wao walipambana na sumu hii. Niliposoma, nilihisi upendo wa Mwokozi kwa ajili yangu na mchumba wangu, na nilipata hakikisho lingine kwamba mwanaume huyu alikuwa kweli mwenza wangu wa milele. Nilijifunza pia kipengele tofauti cha Upatanisho wa Mwokozi—jinsi anavyoweza kuponya nafsi (ya mchumba wangu) na moyo (wangu) uliochubuliwa.

Kipengele muhimu katika safari yetu kilikuwa kuzungumza na askofu wa mchumba wangu. Mwongozo wake ulitusaidia kupona na kuwa karibu kama wenza. Alikuwa mvumilivu wakati mume wangu aliporudia uraibu wake, na mfano wake wa kupenda kama Kristo, ulinipa msukumo na kunisaidia kusamehe na kufanyia kazi tatizo hili pamoja na mchumba wangu.

Kwa muda, ilikuwa vigumu sana kwa mume wangu kuniona nikiteseka kwa sababu ya chaguzi zake kwamba karibu aahirishe kunioa! Lakini baada ya kushirikiana pamoja kwa miezi ili awe msafi, hatimaye alihisi kwamba wote mimi na Bwana tulikuwa tumemsamehe kwa dhati.

Hatimaye, tulifunga ndoa, na uhusiano wetu sasa ni imara kuliko mwanzo. Uzoefu huu umetusaidia kutokuona aibu kuzungumza sisi wenyewe kuhusu matatizo yetu. Na japokuwa hajihusishi tena na ponografia, bado tuko makini sana na tunawajibika kwa kila mmoja.

Uhusiano Wako Unaweza Kufanikiwa

Ikiwa uhusiano wako umetiwa sumu kwa matokeo ya ponografia, jua kwamba inawezekana kusamehe. Inawezekana kuendelea kupendana na kushirikiana kutafuta suluhisho na kuishinda. Sote tuna haki ya uponyaji wa Upatanisho wa Mwokozi. Tunapaswa kukubali kwamba tunaumia na kwamba kwa usaidizi wa Mwokozi pekee tunaweza kuponywa kikamilifu.

Kila hadithi ya mtu ni ya kipekee, na kila uhusiano ni wa kipekee. Kwa baadhi ya watu, kusitisha uhusiano kunaweza kuwa kitu sahihi kufanya. Lakini ninatumaini hadithi yetu inaweza kuwasaidia wengine katika hali sawa na hizo. Kwa sababu nilipokea uthibitisho huo kutoka kwa Roho Mtakatifu, na kwa usaidizi wa Mwokozi na Upatanisho Wake, niliweza kumsamehe mchumba wangu na kuendeleza uhusiano wetu. Najua kwamba ulikuwa uchaguzi sahihi kwangu.

Ikiwa unapitia hali sawa na hiyo, kwa sala fikiria hali zako za sasa na kile wakati ujao unachoweza kuwa nacho. Ikiwa utapokea uthibitisho kutoka kwa Roho kwamba kuendeleza uhusiano wako ni jambo sahihi kufanya na unahisi kuwa na ujasiri, jua kwamba kwa juhudi zenu wote wawili na kumtegemea Baba wa Mbinguni, uhusiano wako unaweza kuimarika.

Mume wangu ni mtu mzuri, na ninampenda kuliko wakati wowote! Siwezi kumshukuru Bwana vya kutosha kwa kutusaidia kupona na kufanya iwezekane kwetu kuoana. Bwana ametusaidia kukua pamoja kama wanandoa ambao wako tayari kukabiliana na chochote ambacho Yeye amepanga kwa ajili ya maisha yetu pamoja.

Chapisha