Liahona
Kweli Mbili Ambazo Zinanisadia Nielewe Unyenyekevu
Julai 2024


“Kweli Mbili Ambazo Zinanisadia Nielewe Unyenyekevu,” Liahona, Julai 2024.

Vijana Wakubwa

Kweli Mbili Ambazo Zinanisaidia Nielewe Unyenyekevu

Unyenyekevu unaweza kutusaidia kwenye kiburi na hisia ya kutokutosheleza.

Picha
vijana wakubwa wa kiume wakiwa katika darasa kanisani

Picha ya waumini huko Paraguay na Leslie Nilsson

Ukweli: Mimi ni mtoto wa Mungu. Na hiyo ni habari nzuri sana na ni ukweli mtakatifu.

Ukweli muhimu unaofanana na huo: Kwa vile kila mtu mwingine duniani pia ni mtoto wa Mungu, wote pia ni wa kupendeza na viumbe wa kiungu.

Kweli hizi zote mbili inawezekana zinaonekana ni dhahiri, lakini imenichukua muda kuzikubali na kuelewa zinamaanisha nini katika maisha yangu. Wakati mwingine nahisi mwenye hatia kwa kuikabili hali kwa kiburi, nikidhania njia yangu ndio njia sahihi au kwamba mimi nina uwezo zaidi kuliko watu wengine. Nyakati zingine ninafanya kinyume chake, nikijihisi kwamba mimi ni mwenye thamani pungufu kuliko wengine wanaonizunguka.

Jibu kwa mapambano yote mawili ni moja:

Unyenyekevu

Je, Mimi Sikutosha?

Tukio moja ambalo kweli lilininyenyekeza lilitokea nikiwa kwenye misioni yangu. Ninafikiri wamisionari wengi zaidi wanapambana na hisia ya kutotosheleza wakati wanapojaribu kuwaleta watu kwa Yesu Kristo. Kwenye misioni yangu, nilitumia saa kadhaa kwa siku nikijaribu tu kutafuta mtu wa kumfundisha na nilikataliwa tena na tena. Sikuhisi kuwa mwenye mafanikio. Sikuhisi kuwa juhudi zangu zilikuwa za kutosha. Mwishowe, nilianza kuhisi kwamba Mimi sikuwa mwenye kufaa.

Wakati inaweza isionekane kama unyenyekevu ndicho kitu nilichohitaji, wakati nilipoelezea hisia zangu kwa rais wangu wa misheni, yeye alinisaidia kuona kwamba sehemu ya tatizo langu ilikuwa ni kudhani nilikuwa nimesamehewa kutokana na matatizo ambayo wamisionari ulimwenguni kote wanakabiliwa nayo. Lakini mimi siyo mmisionari wa kwanza kuhisi kukataliwa, na kwa hakika sitakuwa wa mwisho.

Kwa namna fulani nilijithibitishia mwenyewe kwamba magumu yangu yalikuwa kosa langu mimi mwenyewe tu, licha ya ukweli kwamba baadhi ya wamisionari bora katika historia—kama wale mitume Kumi na Wawili wa mwanzoni, wana wa Mosia, na Alma Mdogo—walikabiliwa na kukataliwa kubaya zaidi na mateso kuliko niliyoyapata mimi.

Badala ya kujisikitikia mwenyewe, nilianza kuhisi kwamba nilikuwa nimesimama bega kwa bega na Yesu Kristo katika mapambano yangu. Na wakati nilipohisi aibu ya mapungufu ya juhudi zangu, nilikumbuka kitu ambacho Rais Jeffrey R. Holland, Kaimu Rais wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili, alikifundisha: “Upatanisho [wa Kristo] utawabeba wamisionari pengine hata kwa umuhimu zaidi kuliko utakavyowabeba wachunguzi. Unapopambana, unapokataliwa, … unasimama kwa maisha bora zaidi ambayo ulimwengu huu kamwe haujapata kuyajua, maisha pekee safi na makamilifu ambayo yamewahi kuwepo.”

Bado ninavuta taswira ya uzoefu huu pale ninapohitaji kukumbuka kuwa mnyenyekevu na kutumaini katika Bwana.

Somo la Unyenyekevu

Nilijifunza mengi kuhusu utambulisho wangu kama mtoto wa Mungu wakati nilipokuwa katika misioni yangu. Lakini baada ya kurudi nyumbani, niligundua kwamba bado kulikuwa na mengi ya kujifunza kuhusu umuhimu wa kukumbuka kwamba watu wengine pia ni watoto wa Mungu.

Punde baada ya kurudi nyumbani, niliwekwa kwenye wito mgumu na kupewa kusimamia tukio muhimu. Nilizidiwa, na sikuweza kuwapata watu ambao walikuwa wanapaswa kunisaidia. Nilituma barua pepe ambayo ilikuwa, kwa kweli, yenye maneno makali sana.

Nilikuwa sahihi kwamba ule wito ulikuwa muhimu na kwamba nilihitaji usaidizi zaidi, lakini kwa haraka niligundua kwamba pengine hii haikuwa njia bora zaidi ya kuwahamasisha watu. Nilihitaji unyenyekevu; nilihitaji kukumbuka kwamba watu wengine pengine walikuwa na mambo yao wenyewe ambayo yaliwasonga.

Kama Mzee Steven E. Snow alivyofundisha wakati alipokuwa mshiriki wa Sabini, “Kama tutajinyenyekeza wenyewe, sala zetu zinajibiwa; tunafurahia amani ya akili; tunahudumu kwa tija zaidi katika miito yetu; na kama tunaendelea kuwa waaminifu, mwishowe tutarudi kwenye uwepo wa Baba yetu wa Mbinguni.”

Kwa kweli, nimehisi shangwe zaidi katika wito wangu na katika maisha yangu kadiri nilipojifunza kuwa mnyenyekevu zaidi.

Kuwekea Uwiano Kweli Hizi Mbili

Kwangu mimi, kujifunza unyenyekevu wa kweli kumekuwa kuhusu kuweka uwiano wa kweli hizi mbili:

Mimi mtoto wa Mungu. Na nimezungukwa na watoto wengine wa Mungu.

Kadiri nilivyojifunza zaidi kuhusu unyenyekevu, nimegundua kwamba kitu ambacho Mzee Quentin L. Cook wa Akidi ya Mitume Kumi na Wawili alifundisha ni cha kweli: “Unyenyekevu sio mafanikio fulani makubwa yanayotambulika au hata kushinda changamoto kubwa. … Ni kuwa na utulivu wa kujiamini kwamba siku hadi siku na saa baada ya saa tunaweza kumtegemea Bwana, kumtumikia Yeye, na kufanikisha madhumuni Yake.” Nimejifunza kwamba hakika ninaweza kufanikisha madhumuni ya Bwana—pale tu ninapoyageuza matakwa yangu Kwake na kutumaini kwamba Yeye anajua lililo bora.

Ninajua kwamba tunapojitahidi kuwa zaidi wanyenyekevu na kama Kristo, Baba wa Mbinguni atatubariki sisi katika jitihada zetu.

Mwandishi anaishi huko Frankfurt, Ujerumani.

Muhtasari

  1. Jeffrey R. Holland, “Kazi ya Umisionari na Upatanisho,” Ensign, Machi 2001, 15.

  2. Steven E. Snow, “Kuwa Mnyenyekevu,” Liahona, Mei 2016, 36.

  3. Quentin L. Cook, “Umilele wa Kila Siku,” Liahona, Nov. 2017, 54.

Chapisha