2023
Mtu Ambaye Anaelewa
Novemba 2023


“Mtu Ambaye Anaelewa,” Rafiki, Nov. 2023, 26–27.

Mtu Ambaye Anaelewa

Marafiki wa Blair hawakuelewa jinsi ilivyo kuwa na ugonjwa wa Crohn (ugonjwa usababishao maumivu makali kwenye utumbo mwembamba na mpana kwa muda mrefu).

Hadithi hii ilitokea huko Marekani.

Picha
alt text

“Siwezi kuja huko leo, Blair alisema. Uso wake ulihisi joto kwa aibu.

Rafiki zake walimkazia macho. “Lakini ulisema ungekuja!” Sammy alisema.

“Ninajua.” Blair alitazama chini miguuni kwake. “Sijihisi vizuri sana. Samahani.”

“Hicho ndicho ulichosema mara ya mwisho,” Jessica akasema.

Blair hakujua nini cha kusema. Alitamani angeweza kwenda nyumbani kwao Sammy. Lakini tumbo lake linauma kweli leo. Alihitaji kwenda nyumbani na kupumzika.

Blair alikuwa na ugonjwa wa Crohn. Ulimfanya tumbo lake liume, na linauma kweli. Siku zingine tumbo linauma lakini angalau linauma kidogo. Lakini baadhi ya siku linauma kuliko siku zingine. Leo ilikuwa miongoni mwa zile siku za maumivu. Alitamani angeweza kuchagua siku gani liume zaidi. Ilionekana kana kwamba tumbo lake linauma zaidi siku yoyote alipotaka kufanya kitu cha burudani.

“Acha twende tu,” Sammy alimwambia Jessica.

Blair alipofika nyumbani, alikunywa dawa zake. Kisha akajaribu kulala. Lakini liliendelea kuuma.

Picha
alt text

Mama na Baba walikuja kumwangalia. Baba alikaa kwenye kitanda chake. “Je, unajisikiaje?”

“SAWA. Dawa zimenisaidia kidogo,” Blair alisema.

“Pole hukuweza kwenda nyumbani kwao Sammy,” Mama alisema.

Blair alihisi machozi machoni mwake. “Sio sawa! Rafiki zangu hawaelewi ninavyoumwa.” Blair alitupa mto wake ukutani. “Ninataka kupona tu.”

Baba alimkumbatia Blair. “Ninajua. Je, ungependa kupata baraka ya ukuhani?”

Blair alikubali kwa kichwa. Baraka kwa kawaida ilimsaidia ahisi amani zaidi.

Picha
alt text

Baba aliweka mikono juu ya kichwa chake, na akampa baraka ili apumzike na ahisi faraja. Ilikuwa baraka nzuri. Ilimsaidia kukumbuka kwamba Baba wa Mbinguni alimpenda. Lakini bado alihisi kuwa mwenye huzuni kuhusu rafiki zake.

Baada ya ile baraka Mama na Baba walimpa Blair busu la usiku mwema. Waliondoka ili aweze kulala.

Blair alirejea kwenye kulala na kufumba macho yake. Baraka ilikuwa imemsaidia, lakini bado alikuwa anaumia.

Alipiga magoti kando ya kitanda chake ili kusali. Mwanzoni ilikuwa kama sala zake nyingi. Alimwambia Baba wa Mbinguni kitu alichokuwa na shukrani nacho na kuomba ahisi vyema. Lakini wakati huu aliendelea kuomba.

Picha
alt text

“Baba wa Mbinguni, ninahisi huzuni kweli. Ninakosa kuwa pamoja na rafiki zangu. “Ninahisi upweke. Hakuna mtu anayeelewa kuwa ninaumwa kila siku. Ninakumbuka hisia ya jinsi nilivyokuwa kabla ya kuumwa.

Kadiri alivyosali kwa muda mrefu, ndivyo alivyokuwa akihisi kwamba Baba wa Mbinguni alikuwa akisikiliza sala yake. Hakuweza kumsikia au kumwona, lakini alihisi upendo Wake. Alijua Yeye anajali kuhusu kile alichokuwa akikisema. Blair hakuwa anataka hisia zile ziishe.

Blair alisali hadi alipokuwa amemwambia Baba wa Mbinguni kila kitu alichokuwa anakihisi. Kisha wazo likamjia akilini mwake. Marafiki wa Blair yawezekana kamwe wasijue inavyokuwa unapokuwa na ugonjwa wa Crohn, lakini Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo walijua. Wao walijua ni kiasi gani anaumia na namna gani anahisi upweke. Daima wangekuwepo pale kwa ajili yake.

Blair alihisi kama vile anapata kumbatio kubwa zaidi. Baada ya kumaliza sala yake, alienda kuwatafuta wazazi wake ili awaambie kile kilichotokea.

“Ulipata ndoto mbaya?” Mama aliuliza.

Blair alitabasamu. “Hapana. Nimekuwa nikisali.”

Mama alionekana kushangaa. “Tulikuambia usiku mwema kitambo. Ulikuwa unasali muda wote huo?”

Imekuwa muda mrefu kumbe? Blair alikubali kwa kichwa. “Ilikuwa kama kupata kumbatio kubwa. Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wanajua jinsi ninavyohisi. Kwa sababu yao, sihitaji kuhisi mpweke!”

Picha
alt text here

Vielelezo na Tammie Lyon

Chapisha