2023
Mnara wa Imani
Julai 2023


“Mnara wa Imani,” Rafiki, Julai 2023, 10–11.

Mnara wa Imani

Dashanel alitaka imani yake katika Kristo iwe ndefu na imara.

Hadithi hii ilitokea huko Jamaica.

Picha
Ndugu wakibebanisha vikombe wakati wamisionari wakiangalia

Dashanel alimsaidia kaka yake kuondoa mkate wa karanga kwenye oveni. Unanukia vizuri sana!

Kisha akasikia hodi mlangoni. “Wamisionari wamefika!” dada yake aliita.

Dashanel alikimbia mlangoni. Alipenda sana wamisionari walipokuja. Mara zote alikuwa na hisia nzuri wakati wamisionari walipowatembelea. Nyakati zingine walileta michezo kwa ajili ya yeye na ndugu zake kucheza.

“Tyrell ametengeneza tena mkate wa karanga!” Dashanel alisema. Kaka yake alipenda kutengeneza chakula kwa ajili ya wamisionari.

“Natamani nionje,” Mzee Colas alisema. Yeye na Mzee Yusaki waliingia ndani na kuketi sakafuni. Dashanel, kaka na dada yake na mama waliketi mkabala na wamisionari.

“Kipi tunakwenda kufanya kwa ajili ya somo leo?” Dashanel aliuliza.

Mzee Yusaki alitoa rundo la vikombe. “Tunakwenda kujenga mnara wa imani. Kila moja ya vikombe hivi huwakilisha jambo tunaloweza kufanya ili kujenga imani yetu katika Yesu Kristo.

Mzee Yusaki alianza kubebanisha vikombe kutengeneza mnara. Dashanel aliona kwamba vikombe vilikuwa na maneno kama vile “sala,” “kusoma maandiko” na “kanisa” yameandikwa juu yake.

“Haya ni mambo yote mliyotuomba tufanye kama familia,” alisema.

“Hilo ni sahihi,” Mzee Colas alisema. “Unapofanya mambo haya, unajenga imani yako kwa Yesu Kristo.”

Dashanel na ndugu zake walifanya zamu kujenga minara yao wenyewe kwa kutumia vikombe wakati wakisikiliza somo.

Baada ya wamisionari kuondoka, Dashanel alitafakari kuhusu kile walichofundisha. Alitaka imani yake katika Kristo iwe ndefu na imara, kama vile mnara alioujenga.

Kadiri miezi ilivyopita, Dashanel alijifunza zaidi na zaidi kuhusu injili kutoka kwa wamisionari. Alianza kuhudhuria kanisani akiwa na familia yake. Alipata taswira ya mnara wa imani yake ukiwa mrefu zaidi na zaidi.

Siku moja baada ya wamisionari kuondoka, Dashanel alizungumza na mama. “Je, ninaweza kubatizwa?” aliuliza.

“Una hakika uko tayari?” Mama aliuliza.

“Ndiyo,” Dashanel alisema. “Ninataka kumfuata Yesu.”

“SAWA,” Mama alisema. “Ikiwa unataka, unaweza kubatizwa.”

Kaka na dada wa Dashanel walichagua kubatizwa pia. Mama alisema bado hakuwa tayari kubatizwa.

Picha
Mmisionari akimbatiza msichana

Siku ya ubatizo wao, Dashanel na ndugu zake walivalia mavazi meupe. Kila mmoja wao alingojea kwa subira kubatizwa.

Ilipofika zamu ya Dashanel, Mzee Yuki alimsaidia aingie majini. Kisha alisema maneno ya sala ya ubatizo na kumshusha chini ya maji. Wakati Dashanel aliporudi juu, hakusita kutabasamu! Alijihisi mwenye furaha na safi. Hakutaka kamwe kusahau hisia hii.

Dashanel aliendelea kufanya mambo ya kujenga imani yake katika Yesu Kristo. Alisoma maandiko pamoja na familia yake. Alisali kwa Baba wa Mbinguni. Alifanya mambo yenye ukarimu kwa wengine. Na alikumbuka jinsi alivyohisi wakati alipobatizwa. Alitaka Mama apate uzoefu huo pia.

“Mama, kwa nini usibatizwe?” Siku moja Dashanel aliuliza.

Mama alikuwa kimya kwa muda. “Umeweka mfano mzuri kwa ajili yangu. Sasa, ninahitaji kuweka mfano kwa ajili yako,” alisema. “Ninataka kubatizwa pia.”

Kwenye siku ya ubatizo wa mama, Dashanel alikuwa mwenye furaha kubwa. Wakati mama alipoinuliwa kutoka majini, kila mmoja alikuwa akitabasamu. Sasa familia nzima ya Dashanel wangeweza kujenga minara yao ya imani pamoja.

Picha
PDF ya hadithi

Vielelezo na Alyssa Tallent

Chapisha