Mkutano Mkuu
Leo Hii
mkutano mkuu wa Oktoba 2022


Leo Hii

Nabii wetu aishiye anafanya sehemu yake kwenye kuijaza dunia na Kitabu cha Mormoni. Yatupasa kufuata mfano wake.

Kaka na dada zangu wapendwa, kwenye Kitabu cha Mormoni kirai “leo hii”1 kinarudiwa rudiwa ili kusisitiza ushauri, ahadi na mafundisho. Mfalme Benyamini, katika maneno yake ya mwisho, aliwahusia watu, “Sikilizeni maneno yangu nitakayowazungumzia leo hii; … mfungue masikio yenu ili msikie, na mioyo yenu ili mfahamu, na akili zenu ili siri za Mungu zifunguliwe machoni mwenu.”2 Mkutano Mkuu ni sehemu sawa na hiyo. Tunakuja kusikiliza ushauri kwa ajili ya “leo hii,” ili kwamba tuweze kuwa “wakweli muda wote”3 kwa Bwana na injili Yake. La muhimu mawazoni mwangu “leo hii” ni umuhimu wa kufanya upya nia zetu juu ya Kitabu cha Mormoni, ambacho Joseph Smith alikiita “kitabu sahihi duniani.”4

Picha
Nakala ya Kitabu cha Mormoni ya Mzee Rasband

Nimeshikilia nakala ya Kitabu cha Mormoni. Hii ni nakala ya kale ya mwaka 1970 na ni ya thamani kwangu. Kwa mwonekano wake kimechakaa na kuchanika, lakini hakuna kitabu kingine cha muhimu katika maisha yangu na ushuhuda wangu kama hiki. Kwa kukisoma, nilipata ushahidi kupitia Roho kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu,5 kwamba Yeye ni Mwokozi wangu,6 kwamba maandiko haya ni maneno ya Mungu,7 na kwamba injili imerejeshwa.8 Kweli hizo ziko ndani yangu. Kama nabii Nefi alivyosema, “nafsi yangu hufurahia vitu vya Bwana.”9

Picha
Mzee Rasband na rais wa misheni wake na Mzee Hanks.

Kutoka kushoto: Mzee Ronald A. Rasband, mmisionari kijana; Rais Harold Wilkinson, rais wa misheni ya Eastern States; na Mzee Marion D. Hanks, Kiongozi Mkuu mwenye Mamlaka.

Hii ni historia fupi. Kama mmisionari kijana, nilisikiliza ushauri wa Mzee Marion D. Hanks, ambaye alitutembelea katika Misheni ya Eastern States. Alikuwa rais wa misheni ya Uingereza hapo awali, na wawili wa wamisionari wake wako kwenye jukwaa leo hii: ndugu zangu wapendwa Mzee Jeffrey R. Holland na Mzee Quentin L. Cook.10 Kama vile wamisionari huko Uingereza, alitupatia changamoto ya kusoma nakala ya Kitabu cha Mormoni ambayo haijatiwa alama angalau mara mbili kwa mwaka. Niliukubali wajibu huo. Usomaji wangu wa kwanza ulikuwa na nia ya kuweka alama au kupigia mstari kila kitu kilichoelekeza au kushuhudia juu ya Yesu Kristo. Nilitumia penseli nyekundu, na nilipigia mstari kurasa nyingi. Usomaji wa pili, Mzee Hanks alisema ulikuwa ni kuainisha kanuni na mafundisho ya injili, na wakati huu nilitumia rangi ya bluu kuweka alama kwenye maandiko. Nilisoma Kitabu cha Mormoni mara mbili, kama ilivyopendekezwa, na kisha mara mbili zaidi nikitumia rangi ya njano na nyeusi kuweka alama kurasa ambazo zilikuwa muhimu kwangu.11 Kama muonavyo, niliweka nukuu nyingi.

Picha
Kitabu cha Mormoni kilichowekwa alama

Kulikuwa na cha ziada kwenye usomaji wangu kuliko kuweka alama kwenye maandiko. Kwa kila usomaji wa Kitabu cha Mormoni, mwanzo mpaka mwisho, nilijawa na upendo wa dhati kwa Bwana. Nilihisi ushahidi thabiti wa ukweli wa mafundisho Yake na jinsi yanavyotumika “leo hii.” Kitabu hiki kinaendana na kichwa chake “Ushuhuda Mwingine wa Yesu Kristo.”12 Kwa kujifunza huko na ushahidi wa kiroho uliopokelewa, nilikuwa mmisionari wa Kitabu cha Mormoni na mfuasi wa Yesu Kristo.13

“Leo hii,” moja ya wamisonari wakuu wa Kitabu cha Mormoni ni Rais Russell M. Nelson. Wakati akiwa mtume mpya aliyeitwa, alitoa mhandara Accra Ghana.14 Kwenye mahudhurio walikuwepo viongozi wa heshima, ikijumuisha mfalme wa kikabila wa kiafrika ambaye alizungumza kupitia mkalimani. Mfalme alikuwa mwanafunzi wa Biblia mwenye ari na alimpenda Bwana. Baada ya hotuba yake, alijiwa na mfalme, ambaye aliuliza kwa Kiingereza sanifu, “Wewe ni nani?” Rais Nelson alielezea kwamba alikuwa Mtume aliyetawazwa wa Yesu Kristo.”15 Swali la mfalme lililofuata lilikuwa “Ni kipi unaweza kunifundisha kuhusu Yesu Kristo?”

Rais Nelson alichukua Kitabu cha Mormoni na kufungua 3 Nefi 11. Kwa pamoja Rais Nelson na mfalme walisoma mafundisho ya Mwokozi kwa Wanefi: “Tazama, Mimi ni Yesu Kristo ambaye manabii walishuhudia atakuja ndani ya ulimwengu. … Mimi ni nuru na uzima wa ulimwengu.”17

Rais Nelson alimpatia mfalme nakala ya Kitabu cha Mormoni, na mfalme akajibu, “ungeweza kunipa almasi au rubi, lakini hakuna kilicho cha thamani sana kwangu kuliko nyongeza hii ya maarifa kuhusu Bwana Yesu Kristo.”18

Huo si mfano pekee wa jinsi nabii wetu mpendwa hushiriki Kitabu cha Mormoni. Ametoa nakala za Kitabu cha Mormoni kwa mamia ya watu, mara zote akitoa ushuhuda wake wa Yesu kristo. Wakati Rais Nelson akikutana wa wageni, marais, wafalme, wakuu wa nchi, viongozi wa kibiashara na taasisi na wa imani tofauti tofauti iwe kwenye makao makuu ya Kanisa au kwenye sehemu zao wenyewe, kwa upole hushiriki kitabu hiki cha maandiko yaliyofunuliwa. Angeweza kuwapa vitu vingi ambavyo vimefungwa kwenye riboni ambavyo vingeweza kuwa mezani au dawatini au kwenye kabati kama ukumbusho wa matembezi yake. Badala yake, huwapa kilicho cha thamani zaidi, kuliko rubi na almasi, kama alivyoelezea mfalme wa kikabila.

“Kweli za Kitabu cha Mormoni” Rais Nelson amesema, “zina nguvu ya kuponya, kufariji, kurejesha, kusaidia, kuimarisha, kuliwaza, na kufurahisha nafsi zetu.”19 Nimekuwa nikiona nakala hizi za Kitabu cha Mormoni zikiwa zimeshikiliwa mikononi mwa wale ambao wamezipokea kutoka kwa nabii wetu wa Mungu. Hakungekuwa na zawadi kuu yoyote.

Picha
Rais Nelson na mke wa rais wa Gambia

Hivi karibuni ofisini kwake alikutana na mke wa rais wa Gambia na kwa unyenyekevu alimpa Kitabu cha Mormoni. Hakuishia hapo. Alifunua kurasa zake ili kusoma naye, kufundisha na kushuhudia juu ya Yesu Kristo, Upatanisho Wake na upendo Wake kwa watoto Wake wote—kila mahali.

Nabii wetu aishiye anafanya sehemu yake kwenye kuijaza dunia na Kitabu cha Mormoni.20 Lakini hawezi kufungua milango peke yake. Yatupasa kufuata mfano wake.

Nikitiwa msukumo na mfano wake, nimekuwa nikijaribu kwa unyenyekevu na kwa utulivu kushiriki Kitabu cha Mormoni.

Picha
Mzee Rasband na rais wa Msumbiji

Hivi karibuni nilipewa jukumu huko Msumbiji. Wananchi wa nchi hii nzuri wanasumbuliwa na umaskini, afya duni, ukosefu wa ajira, tufani na machafuko ya kisiasa. Nilipata heshima ya kukutana na rais wa nchi, Filipe Nyusi. Kufuatia ombi lake, nilisali kwa ajili yake na taifa lake; nilimwambia tulikuwa tukijenga hekalu la Yesu Kristo21 nchini mwake. Mwisho wa ziara yangu, nilimpatia nakala ya Kitabu cha Mormoni ya Kireno ambayo ni lugha yake. Wakati akikubali kitabu kwa furaha, nilishuhudia kuhusu tumaini na ahadi kwa ajili ya watu wake, zipatikanazo kwenye maneno ya Bwana kwenye kurasa zake.22

Picha
Mzee Rasband na mfalme na malaika wa Lesotho

Kwenye tukio lingine, mimi, pamoja na mke wangu, Melanie tulikutana na Mfalme Letsie III wa Lesotho na mke wake nyumbani kwao.23 Kwetu sisi, cha muhimu kwenye ugeni wetu ilikuwa kuwapa nakala ya Kitabu cha Mormoni na kisha kushiriki ushuhuda wangu. Wakati tukikumbuka uzoefu huo pamoja na mwingine, mstari toka maandiko ya watakatifu wa siku za mwisho hunijia mawazoni: “utimilifu wa injili yangu uweze kutangazwa na watu walio dhaifu na wa kawaida hata mwisho wa dunia, na mbele ya wafalme na watawala.”24

Picha
Mzee Rasband na Balozi Pandey
Picha
Viongozi wa Kanisa na Mtakatifu Patriaki Bartholomew

Nilishiriki Kitabu cha Mormoni na Balozi wa India katika Umoja wa Mataifa huko Geneva, Indra Mani Pandey25; na Mtakatifu Patriaki Bartholomew26 wa Kanisa la Eastern Orthodox; na wengine wengi. Nimemhisi Roho wa Bwana pamoja nasi wakati mimi binafsi nikiwapa wao hili “jiwe la katikati la tao la dini yetu”27 na kutoa ushuhuda wangu juu ya Yesu Kristo, jiwe kuu la pembeni la imani yetu.28

Sasa, akina kaka na akina dada, si lazima uende Msumbiji au India au kukutana na wafalme na watawala kumpa mtu kitabu hiki cha mafundisho na ahadi takatifu. Ninawaalika, leo hii, kuwapa marafiki na familia zenu Kitabu cha Mormoni, wafanyakazi wenzenu, kocha wa timu yenu ya mpira wa miguu, au mzalishaji sokoni kwenu. Wanahitaji maneno ya Bwana yapatikanayo kwenye kitabu hiki. Wanahitaji majibu ya maswali ya maisha ya kila siku na ya maisha ya milele yajayo. Wanahitaji kujua juu ya njia ya agano iliyowekwa mbele yao na upendo endelevu wa Bwana kwao. Vyote viko kwenye Kitabu cha Mormoni.

Wakati ukiwapa Kitabu cha Mormoni, unafungua mawazo na mioyo yao kwa ajili ya neno la Mungu. Huna haja ya kubeba nakala zilizochapwa za Kitabu cha Mormoni. Kiurahisi unaweza kukishiriki kutoka kwenye simu yako kutoka kwenye sehemu ya maandiko ya programu ya Maktaba ya Injili.29

Fikiria wale wote ambao wangeweza kubarikiwa na injili katika maisha yao, na kisha kuwatumia nakala ya Kitabu cha Mormoni kutoka kwa simu yako. Kumbuka kujumuisha ushuhuda wako na jinsi kitabu hiki kimebariki maisha yako.

Rafiki zangu wapendwa, kama Mtume wa Bwana, ninawaalika kumfuata nabii wetu mpendwa, Rais Nelson, katika kuijaza dunia na Kitabu cha Mormoni. Hitaji hili ni kuu; tunahitaji kufanya hivyo sasa. Ninaahidi mtakuwa mkishiriki kwenye “kazi kuu duniani,” kuikusanya Israeli,30 wakati mkipata msukumo kuwafikia wale ambao “wametengwa na ukweli kwa sababu hawajui wapi pa kuupata.”31 Wanahitaji ushuhuda wenu na ushahidi wa jinsi kitabu hiki kimebadilisha maisha yenu na kuwasogeza karibu na Mungu, amani Yake,32 na habari Yake “njema ya furaha kuu.”33

Ninashuhudia kwamba kwa mpango matakatifu Kitabu cha Mormoni kiliandaliwa huko Amerika ya kale ili kuja kutangaza neno la Mungu, kuleta nafsi kwa Yesu Kristo na injili Yake ya urejesho “leo hii.” Katika jina la Yesu Kristo, amina.

Muhtasari

  1. Ona Yakobo 2:2–3; Mosia 2:14, 30; 5:7; Alma 7:15; na mstari mingine mingi katika Kitabu cha Mormoni.

  2. Mosia 2:9.

  3. Alma 53:20

  4. Teachings of Presidents of the Church: Joseph Smith (2007), 64. Kauli kamili iliyotolewa na Joseph Smith November 28, 1841 kwenye baraza la Mitume Kumi na wawili: “Niliwaambia ndugu kwamba Kitabu cha Mormoni ndicho kitabu sahihi duniani, na ndicho jiwe la katikati la teo la dini yetu, na kuwa mwanadamu angemkaribia Mungu zaidi kwa kufuata mafundisho yake, zaidi ya kitabu kingine.” Rejeleo la msingi la “sahihi” linaweza kuhusishwa na ufunuo uliopokelewa katika tafsiri yake na mafundisho toka kwenye Kitabu cha Mormoni ambayo huuleta ukweli zaidi ya kitabu kingine chochote kweli za injili “wazi na thamani (ona 1 Nefi 13:40).

  5. Ona “Kristo aliye Hai: Ushuhuda wa Mitume,” tamko la Urais wa Kwanza na Mitume Kumi na Wawili, Januari 1, 2000: “Tunatoa ushuhuda, kama Mitume Wake waliotawazwa—kwamba Yesu ni Kristo Aliye hai, Mwana wa Mungu. Yeye ni Mfalme Immanuel, ambaye anasimama mkono wa kuume wa Baba Yake. Yeye ni nuru, uzima, na tumaini la ulimwengu. Njia Yake ni njia ambayo inaelekeza kwenye furaha katika maisha haya na maisha ya milele katika ulimwengu ujao.” Mungu ashukuriwe kwa ajili ya zawadi isiyolinganishwa ya Mwanaye mtukufu” (ChurchofJesusChrist.org).

  6. Ona Isaya 49:26; 1 Nefi 21:26; 22:12; Mafundisho na Maagano 66:1.

  7. Neno la Mungu hupatikana kwenye maandiko. Kwa mfano, kwenye Kitabu cha Mormoni, Lamani na Lemuel waliuliza, “Fimbo ya chuma hummanisha nini?” ukirejelea ono la Lehi. Nefi alijibu “ilikuwa neno la Mungu; na yeyote atakayesikiza hilo neno la Mungu, na alizingatie, hataangamia; wala majaribu na mishale ya moto ya adui kuwalemea na kuwapofusha, ili kuwaelekeza kwenye maangamio” (1 Nefi 15:23–24).

  8. Ona “Urejesho wa Utimilifu wa Injili ya Yesu Kristo: Tangazo kwa Ulimwengu la Maadhimisho ya Miaka Mia Mbili,” ambalo linajumuisha yafuatayo “Tunatangaza kwamba Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, lililorejeshwa mnamo Aprili 6, 1830, ni Kanisa la Kristo la urejesho la Agano Jipya. Kanisa hili lina nanga katika maisha makamilifu ya jiwe lake kuu la pembeni, Yesu Kristo, na katika Upatanisho Wake usio na mwisho na Ufufuko wake halisi. Yesu Kristo kwa mara nyingine tena amewaita Mitume na amewapa mamlaka ya ukuhani. Anatualika sote kwenda Kwake na kwenye Kanisa Lake, ili kupokea Roho Mtakatifu, ibada za wokovu, na kupata shangwe ya kudumu. … Kwa furaha tunatamka kwamba Urejesho ulioahidiwa unasonga mbele kupitia ufunuo endelevu. Dunia kamwe haitabaki kama ilivyo, kwani Mungu “atavijumlisha vitu vyote katika Kristo” (Waefeso 1:10)”(ChurchofJesusChrist.org).

  9. 2 Nefi 4:16.

  10. Ona Quentin L. Cook, “Be Not Weary in Well-Doing” (Brigham Young University devotional, Aug. 24, 2020), speeches.byu.edu; “This Week on Social: How to Develop a Love for the Lord, Yourself and Others,” Church News, Saturday, July 17, 2020.

  11. Usomaji kwa mara ya tatu, njano: giologia ya giografia; usomaji kwa mara ya nne, nyeusi: hadithi ya Kitabu cha Mormoni.

  12. Maandishi “Ushuhuda Mwingine wa Yesu Kristo” yaliongezwa kama kichwa cha habari saidizi kwenye matoleo yote ya Kitabu cha Mormoni Viongozi wa Kanisa walifanya mabadiliko ya jina ili kusisitiza zaidi dhumuni la kitabu kama ilivyosemwa kwenye ukurasa wa jina: “Na pia kuwathibitishia Myahudi na Myunani kwamba Yesu ndiye Kristo, Mungu wa Milele, anayejidhihirisha kwa mataifa yote.”

  13. Kuwa mfuasi wa Yesu Kristo ni kielelezo cha upendo wetu Kwake. Wafuasi wakiwa wamebatizwa; wanachukua juu yao jina la Yesu Kristo, wanajitahidi kumfuata kwa kushikilia sifa Zake kama inavyoelezewa na Mtume Petro: “Mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema; na katika wema wenu maarifa; na katika maarifa yenu kiasi; na katika kiasi chenu saburi; na katika saburi yenu utauwa; na katika utauwa wenu upendano wa ndugu; na katika upendano wa ndugu, upendo” (2 Petro 1:5–7; ona pia Hubiri Injili Yangu: Mwongozo katika Huduma ya Umisionari (2019),121–32 [2019], 121–32).).

  14. Rais Russell M. Nelson akijulikana kimataifa kama mtaalamu wa moyo kabla ya wito wake kwenye Akidi ya Mitume Kumi na Wawili mnamo 1984, alizungumza katika shule ya tiba huko Accra, Ghana mnamo 1986 kuhusu historia ya upasuaji wa moyo. Akihojiwa baadaye na vyombo vya habari, alielezea kwamba alikuwepo pale kama “mtumishi wa Bwana ili kuwasaidia [watu] kuwa wananchi bora, kujenga familia imara, na kupata furaha ya kweli na kufanikiwa kwenye nchi.” Alirudi Accra, Ghana mnamo Novemba 16, 2001 kwa ajili ya uchimbaji ardhi wa hekalu la Accra Ghana (ona “Ground Broken for First Temple in West Africa,” Church News, Nov. 24, 2001, thechurchnews.com).

  15. Ona Kitabu cha Maelezo Jumla: Kuhudumu katika Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, 5.1.1.1: “Katika siku yetu Bwana huwaita watu kupitia Rais wa Kanisa kutawazwa Mitume na kutumikia katika Akidi ya wale Kumi na Wawili (ona Mafundisho na Maagano 18:26–28).”

  16. Ona Russell M. Nelson, “Kitabu cha Mormoni: Maisha Yako Yangekuwaje Bila Hicho?Liahona, Nov. 2017, 60.

  17. 3 Nefi 11:10–11.

  18. Russell M. Nelson, “Kitabu cha Mormoni: Maisha Yako Yangekuwaje bila kuwa nacho?” 61.

  19. Russell M. Nelson, “Kitabu cha Mormoni: Maisha Yako Yangekuwaje bila kuwa nacho??” 62.

  20. Ona Musa 7:62.

  21. Hekalu la Beira Mozambique lilitangazwa mnamo Aprili 4, 2021 na Rais Russell M. Nelson. Zaidi ya watu nusu milioni wanaishi Beira, ambayo iko kwenye pwani ya bahari ya Hindi

  22. Mifano ya tumaini na ahadi zipatikanazo kwenye Kitabu cha Mormoni hujumuisha 2 Nefi 31:20; Yakobo 4:4–6; Alma 13:28–29; 22:16; 34:41; Etheri 12:32; Moroni 7:41; 8:26.

  23. Mzee na Dada Rasband walikutana na familia ya kifalme Februari 10, 2020 wakati wakiwa kwenye jukumu huko Afrika kuweka wakfu Hekalu la Durban Afrika Kusini.

  24. Mafundisho na Maagano 1:23.

  25. Mzee Rasband alikutana na Balozi Indra Mani Pandey, Mwakilishi wa Kudumu wa India katika Umoja wa Mataifa na Mashirika ya Kimataifa mengine huko Geneva, wakati akiwa kwenye jukumu katika Jukwaa la Dini Mchanganyiko huko Bologna Italia, mnamo Septemba 17, 2021.

  26. Mzee Rasband alikutana na Mtakatifu Patriaki wa Kanisa la Eastern Orthodox, wakati akiwa kwenye jukumu katika Jukwaa la Dini Mchanganyiko huko Bologna Italia, mnamo Septemba 13, 2021.

  27. Teachings: Joseph Smith, 64. Jiwe la katikati la tao ni jiwe lililo na umbo la kabari lililoko juu ya tao ambalo linashikilia mawe mengine pamoja. Nabii Joseph alielezea Kitabu cha Mormoni kama “jiwe la katikati la teo la dini yetu” kutokana na umuhimu wake katika kuunganisha Kanisa kupitia kanuni na ibada. Kitabu cha Mormoni hutumika kama “jiwe la kati la teo” kwenye maisha ya waumini, kikiwasaidia kubakia imara kwenye njia ya agano.

  28. Ona Waefeso 2:19–20. Yeye ni jiwe kuu la pembeni la Kanisa letu, ambalo linabeba jina Lake. Kama vile kuweka jiwe kuu la pembeni kwenye hekalu ni ishara ya jiwe kuu linalotengeneza kona ya msingi wa nyumba ya Mungu, Yesu Kristo ni jiwe la pembeni la imani yetu na wokovu. Alitoa maisha yake kwamba tupate kuishi; hakuna aliye saw na Yeye katika nguvu, dhumuni na upendo.

  29. Unaweza ukashiriki kupitia simu yako. Njia mojawapo ni kwa kufungua programu ya Maktaba ya Injili, kisha kwenda kwenye “Maandiko”, na kisha kubofya “Shiriki Sasa” kwa juu. Au kwenye programu ya Kitabu cha Mormoni, unaweza kubofya ikoni ya “Shiriki” ambayo huonyesha kodi ya QR ambayo rafiki anaweza kiurahisi kuitumia kupitia simu yake.

  30. Russell M. Nelson, “Tumaini la Israeli” (mkutano wa ibada wa vijana ulimwenguni kote, Juni 3, 2018), HopeofIsrael.ChurchofJesusChrist.org. “Mnamo Juni 3, 2018 Rais Russell M. Nelson na mkewe, Wendy W. Nelson, waliwaalika vijana ‘kujiunga na kikosi cha vijana wa Bwana’ na kuchukua nafasi katika ‘changamoto kuu, dhumuni kuu na kazi kuu hapa duniani.’ Na changamoto kuu ni ipi? Kuikusanya Israeli” (Charlotte Larcabal,“A Call to Enlist and Gather Israel,” New Era, Mar. 2019, 24).

  31. Mafundisho na Maagano 123:12.

  32. Ona 2 Nefi 4:27; Mosia 4:3; 15:18; Alma 46:12.

  33. 1 Nefi 13:37.

Chapisha