2017
Kuwahudumia Wengine katika Imani
April 2017


Vijana

Kuwahudumia Wengine katika Imani

Picha
boys with shovels

Rais Uchtdorf anatuambia sisi kwamba imani yetu kwa Mungu lazima “iambatane na matendo.” Wakati imani yetu “imefungwa nira pamoja na tendo endelevu,” anaelezea, “huijaza … nafsi kwa amani na upendo.” Pamoja na ahadi ya baraka hii, sisi tunaweza kuleta tofauti, na tunaweza kuona hili katika maisha yetu kama tunachukua muda wetu kufanya huduma iliyojaa-imani. Unaweza kuomba kila asubuhi ili kumwomba Bwana msaada katika kuwatumikia wengine. Kwa mfano, muombe Yeye akuonyeshe wakati ndugu zako wanahitaji msaada wa kazi ndogo ndogo au wakati rafiki anahitaji kupongezwa. Kisha, wakati unapopokea msukumo utendee kazi! Kama ukiyafanya maombi na huduma hii kuwa tabia, ndipo, matendo yako ya uaminifu na endelevu yatabariki maisha yako na maisha ya wengine. Rais Uchtdorf ameahidi kwamba wewe “unaweza kuwabadilisha watu, familia, mataifa, na ulimwengu.”

Chapisha