Liahona
Ushuhuda wa Ndoa
Julai 2024


Makala

Ushuhuda wa Ndoa

Mimi ni muumini wa Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, kata ya DIALA kigingi cha Kolwezi. Ningependa kushiriki ushuhuda wangu wa tangu miaka yangu ya shule ya upili nilipowatamania wanandoa wachanga ambao kwa kipindi hicho walikuwa wakiishi kwa furaha. Baada ya kuanza masomo yangu ya chuo, nilifanya uamuzi wa kuoa kabla ya kumaliza masomo, na leo nimebarikiwa na familia yenye furaha.

Msukumo wa uamuzi huu umejikita katika imani kwamba sehemu sahihi ya kukuza nuru na ukweli ni katika nyumba zetu. Familia inachukuliwa kama karakana ya Bwana ambapo tunajifunza na kuishi injili. Kila mwanafamilia ana jukumu la kusaidia kuimarisha wengine kiroho. Familia na nyumba za milele zilizojaa Roho haziji tu kwa bahati nasibu! Zinahitaji jitihada za dhati, muda na ushiriki wa kila mtu.

Ingawa kila nyumba ni ya kipekee, ni muhimu kwamba kila mtu atafute ukweli ili kusaidia kuleta utofauti. Hivi leo, shangwe yangu kuu ni kwamba mimi na familia yangu tumeunganishwa katika Hekalu la Kinshasa kwa maisha haya na milele yote. Tunatoa shukrani zetu kwa Mungu, Baba yetu wa Mbinguni, na Mwanawe, Yesu Kristo, kwa baraka zilizowekwa juu yetu. Ndoa yetu ni ya mafanikio, na kwa dhati tunaamini kwamba kila kitu kinaweza kutokea isipokuwa kutengana. Familia ya Mutoba ni yenye shukrani na imeungana.

Chapisha