Liahona
Tawi la Kwanza la Kanisa la Yesu Kristo Linaanzishwa huko Baraka, Kivu ya Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Julai 2024


Makala

Tawi la Kwanza la Kanisa la Yesu Kristo Linaanzishwa huko Baraka, Kivu ya Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo

Christian Mavinga, rais wa Misheni ya Kigali-Rwanda ya Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho, alifanya safari ya kuchosha ya masaa 8 kwenye njia ya hatari kutoka Bujumbura, Burundi, hadi Baraka, Kivu ya Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ili kuanzisha tawi jipya la Kanisa mnamo Jumapili ya Januari 14, 2024. Aliambatana na Nuru Mirungo Salomon, mshauri wa kwanza katika urais wa Wilaya ya Bujumbura, Lokwa Hoga, rais wa tawi la Kalundu na Désiré Mpawenayo, mkurugenzi wa mawasiliano nchini Burundi.

Kabla ya kuwa tawi mnamo Januari 14, waumini wa kanisa huko Baraka walikuwa wamejikusanya kama kundi (mkusanyiko mdogo unaosimamiwa na tawi) kwa miaka 10. Tawi ni mkusanyiko wa Kanisa unaofanya kazi kikamilifu ukiwa na wenye ukuhani wa Melkizedeki ambao wanaongozwa na rais wa kigingi au, katika suala la Tawi la Baraka, rais wa misheni. Muumini wa kwanza huko Baraka aliongolewa mnamo 2009 na tangu hapo idadi ya waaminifu imekuwa kwa uimara.

Kulingana na waumini wa Kanisa huko Baraka, hii ilikuwa siku isiyosahaulika kwa sababu tawi jipya lilikuwa jibu la sala zao. “Tunasema asante kwa Baba yetu wa Mbinguni kwa baraka hii ya kupendeza ambayo imeshushwa juu yetu baada ya miaka mingi ya ustahimilivu,” alisema muumini.

Wakati wa mkutano, Rais Mavinga aliwaunga mkono viongozi wapya wa Tawi la Baraka.Trésor Amani Amani aliitwa kama rais wa tawi, Isaya Timothée M’mumbeleca kama mshauri wa kwanza, Onda Joseph Asende kama mshauri wa pili, na Venas Ben Rosen Byaombe kama karani wa tawi.

Rais Mavinga alisema: “Tulipokuwa njiani kuja hapa, nilijiuliza swali, kwa nini kuanzisha tawi leo baada ya zaidi ya miaka 10 ya uwepo wa kikundi hapa Baraka? Ninajua kwamba si kwa nguvu zangu bali kwa ustahimilivu wenu na sala zenu vile vile kazi ya umisionari ambayo mmeitimiza, Bwana amejibu sala zenu.”

Aliendelea, “Kanisa hapa lisingeendelea kufanya kazi chini ya usimamizi wa Tawi la Kalundu. Tawi hili linakuja kama jibu la sala zenu na juhudi mliyoiweka katika kazi ya Bwana. Ninawapa ushahidi kwamba Ukuhani ni nguvu ya Mungu. Baba yetu wa Mbinguni ametoa nguvu hii hapa Baraka ili kwamba muweze kutenda katika jina Lake, je, huu si uthibitisho wa upendo Wake? Kupitia ukuhani, mtaliongoza vyema tawi lenu jipya kusonga mbele. Tunawabariki waumini, tunawaponya wagonjwa na ni kupitia ukuhani kwamba tunawaandaa watoto wake kuingia ufalme wa selestia. Ninawasihi muendelee kustahimili katika kutii amri, kusimama imara na daima kuimarisha imani yenu katika Yesu Kristo ili mpokee baraka iliyo kuu ambayo ni uzima wa milele.”

Trésor Amani Amani, rais mpya wa tawi, alielezea kuridhika kwake katika kuona uanzishwaji wa tawi hili. Aliwaambia waumini kwamba wamepigana vita kubwa ya ustahimilivu kwa miaka 13, “ninawahimiza mtoe zaka kwa uaminifu na kwa ukamilifu, mpendane, mbaki wamoja na mshiriki Injili hatimaye kueneza injili hii iliyorejeshwa ya Mwokozi wetu Yesu Kristo.”

“Wapendwa akina kaka na akina dada,” alishuhudia, “ninajua ikiwa tutawatumikia wanadamu wenzetu, tutasonga hadi tuwe na tawi la pili, na la tatu. Ikiwa tutaendelea kushiriki na wengine shangwe katika umoja kupitia imani katika Yesu Kristo, kupitia toba, ubatizo, kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu na kustahimili hadi mwisho, tutapata uzima wa milele. Ninajua kwamba ukuhani ni mamlaka na nguvu ya Mungu, mpendwa Rais wetu Russell M. Nelson ameitwa na Mungu, viongozi wote wa Kanisa vilevile mpendwa rais wetu wa misheni, ninaomba kwamba wakati Yesu Kristo atakaporejea atawakuta waumini wa Baraka wakishangilia.Ninajua pia kwamba ikiwa tutasoma Kitabu cha Mormoni tutabarikiwa sana.”

Chapisha